Wednesday, November 19, 2014

PATACHIMBIKA,DAMU ITAMWAGIKA,KIKWETE MKONO YAKE ITALOWA DAMU AJIANDAE NA TAULO LA KUFUTA DAMU--CUF WAPIGA MKWARA MZITO UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA

Naibu katibu mkuu wa chama hicho bara bi MAGDALENA SAKAYA akizngumza na wanahabari muda huu jijini dar es salaam
Chama cha wananchi CUF kimesema patachimbika pamoja na damu kumwagika endepo kama serikali itaendelea na vurugu na mchezo mchafu unaochezwa katika maandalizi ya kuelekea chaguzi za serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu.

Akizungumza na wanahabari muda huu jijini dare s salaam naibu katibu mkuu wa chama hicho bara bi MAGDALENA SAKAYA chama chake kinasikitishwa sana na jinsi ya serikali ya chama cha mapinduzi kuvuruga uchaguzi wa serikali za mitaa kwa makusudi kwa kuandaa machafuko kwa kutunga kanuni mbaya isiyotekelezeka kanuni mwongozo mbovu wa uchaguzi huo.

Amesema kuwa hii ni dalili kuwa serikali ya chama cha mapinduzi  ilikurupuka katika kuandaa uchaguzi huo na haikuwa na mpango kamilifu wa kufanya uchaguzi huo ndani ya kpindi hiki kama ambavyo kumekuwa na kauli zinazokinzana kati ya Rais KIKWETE pamoja na waziri mkuu MIZENGO PINDA kuhusu tarehe za kufanyika uchaguzi huo.
Baadhi ya maneno ya kutisha yanayopatikana katika tamko la CUF LEO
Akitaja mapungufu hayo ya uchaguzi huo ni pamoja na kutoa mwongozo wa utekelezaji wa kanuni za uchaguzi ambapo maelezo yake yanakinzana ambapo katika kanuni ibara ya 15 kifungu cha 1 kimejieleza vizuri na kutoa fursa kwa mtiririko wa namna ya kuweka pingamizi hadi kujadiliwa kwa rufaa na kila jambo limetengewa muda wake wa utekelezaji lakini katika mwongozo mtoririko huo haupo badala yake unaelekeza maeneo mawili tu ambayo hayaendemio sambamba muda wa kuwakilisha pingamizi kwa msimamizi msaidizi ambapo ni siku nne na muda wa kamati ya rufaa kusikiliza rufaa ambapo ni siku nne na imetajana tarehe zake za utekelezaji nov 26 hadi 29 lakini wakati huo huo hakuna muda wa kusikiliza pingamizi hiyo kwa msimamizi msaidizi hakuna muda wa kukata rufaa kama hujaridhika na maamuzi ya msimamizi msaidizi.
Wanahabari wakisikiliza kwa makini
SAKAYA amesema kuwa malalalamiko hayo pamoja na mengine mengi wamekwisha yafikisha katika ngazi husika na kamwe hawatakubali kuona wanachezewa mchezo mchafu na kama serikli haitaacha mchezo huo patachimbika


No comments: