Thursday, November 13, 2014

TAMASHA LA TIGO WELCOME PACK KUWASHA MOTO MWANZA JUMAMOSI HII,WASANII KIBAO WATAKUWEPO

Meneja bidhaa wa kampuni hiyo EDWIN MGOA akizungumza na wanahabari muda huu jijini Dar es salaam
 Kampeni  kubwa inayoendeshwa na kampuni ya mawasiliano ya TIGO Tanzania maarufu kama TIGO WELCOME PACK mwishoni mwa wiki hii litakuwa mkoani mwanza ambapo wasanii mbalimbali nchini Tanzania watatumbuiza katika tamasha litaklalofanyika mkoani humo siku ya jumamosi.
Akizungumza na wanahabari mapema leo jijini Dar es salaam meneja bidhaa wa kampuni hiyo EDWIN MGOA amesema kuwa kampeni hiyo ya WELCOME PACK inayoendelea kwa muda wa mwezi mmoja sasa imekwisha fanyika kwa mafanikio makubwa katika mikoa mingine huku akiitaja mikoa hiyo kuwa ni    kagera,Kilimanjaro,arusha,iringa,Dodoma,na mbeya ambapo imewapa fursa maelefu ya wateja wake kupata huduma zaa tigo kwa karibu ikiwemo kufurushi cha WELCOME PACK.
FID Q akizungumza 

YOUNG KILLER MSODOKI atakuwepo siku hiyo ya Jumamosi
 Ameongea kuwa tamasha hilo limeandaliwa kwa ajili ya kusherehekea huduma hiyo mpya mahususi kwa wateja wao na kwa safari hii tigo Tanzania imeamua kwenda kutikisa jiji la mwanza baada ya kufanya vizuri katika mikoa kadhaa nchini Tanzania.

Msanii kutoka kundi la origino komed akizingumza na wanahabari  
Baadhi ya wasanii watakaotikisa mkoani mwanza ni pamoja na kindi maaruifu la vichekesho Tanzania ORIGINO KOMED,na wasanii kama FID Q,YOUNG KILLER,pamoja na MWANA FA.ambapo kwa pamoja wameahidi burudani ya aina yake siku hiyo ya tamasha.
Tamasha hilolitafanyika siku ya jumamosi kuanzia saa 6 mchana,ambapo kiingilio katika tamasha hilo ni kuwa na laini ya tigo tu.
Kampeni ya TIGO WELCOME PACK itakuwepo kwa miezi mitatu ambapo misafara zaidi ya 70 ikiwemo basi la tigo la kidigital lenye malengo ya kuwaelimisha wateja kuhusu huduma za tigo za kidigital litatembea  miji zaidi ya 70  na vijiji zaidi ya 100ndani ya mikoa 10 tofauti nchini Tanzania.
PICHA NYINGINE ZA MKUTANO HUO NA WANAHABARI ZIPO CHINI HAPO








No comments: