Saturday, November 8, 2014

UKWELI KUHUSU MISS TANZANIA SITTI MTEMVU KUJIVUA TAJI HUU HAPA


Tangu Sitti Mtemvu atangazwe mshindi pale Mlimani City kumekua na malalamiko kutoka kwa baadhi ya Watanzania yalifuatia kutokana na umri wake,pamoja na taarifa nyingine ambazo yeye alizikanusha na kusema ni uzushi ikiwemo ya kuwa na mtoto.

Baada ya haya yote Novemba 8, 2014 Kamati ya Miss Tanzania imekutana na waandishi wa habari Dar es salaam na kutangaza kwamba Sitti Mtemvu ameandika barua kwa hiari yake yeye mwenyewe, kwamba amelivua taji hilo , hivyo kamati hiyo ikamtangaza ambaye atashikilia taji hilo kwamba ni mshindi namba mbili wa Miss Tanzania 2014 Lilian Kamazima

No comments: