Friday, January 2, 2015

MFUMO WA BVR UMEONYESHA MAFANIKIO MAKUBWA--NEC


Mwenyekiti wa tume hiyo ,Jaji Mstaafu Damian Lubuva akizngumza na wanahabari mapema leo juu ya zoezi hilo
Tume ya taifa ya uchaguzi Tanzania NEC imesema kuwa sasa Tanzania inaweza kutumia mfumo mpya wa uandikishwaji wa daftari la kudumu la wapiga kura wa BVR kutokana na mfumo huo kuonyesha mafanikio makubwa baada ya kuufanyia majaribio katika maeneo kadhaa nchini.


           Akizungumza na wanahabari jijini Dar es salaam mwenyekiti wa tume hiyo ,Jaji Mstaafu Damian Lubuva amesema kuwa tume hiyo ilifanya majaribio ya kutumia mfumo huo mpya wa uandikishwaji katika majimbo matatu ambayo ni KAWE,KILOMBERO NA KATAVI  ambapo mfumo huo ulionyesha kufanya kazi kwa uhakika na kujiridhisha kuweza kuutumia katika zoezi la nchi nzima mapema mwaka huu.

            “Tunasema kuwa tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa kwa sababu matokeo ya jumla yanaonyesha kuwa idadi ya wapiga kura waliojitokeza kujiandikisha ilikuwa kubwa na kuvuka malengo waliyokadiriwa kuandikishwa”amesema lubuva

             Katika takwimu zinaonyesha kuwa kwa mkoa wa dar es salaam kata ya bunju wapiga kura 15,123 waliandikishwa kati ya 27,148 na kata ya mbweni wapiga kura 6200 walianndikishwa kati ya 8278,mkoa wa morogoro kata ya ifakara kakingiuka ipangala,na viuwanja sitini wapiga kura walioandikishwa ni 19,188 wakati makisio yalikiuwa watu 17,790 na mkoa wa katavi halmashauri ya milele kata ya ikuba,usevya na kibaoni wapiga kura walikuwa 11,210 walioandikishwa wakati makisio yaklikuwa  watu 11,394  ambapo amesema kuwa matokjeo hayo yanaonyesha ni jinsi gani wananchi wamekuwa na muamko wa kutumia mfumo huo na vifaa hivyo vilifanya kazi vizuri.
Aidha jaji LUBUVA amesema kuwa zoezi hilo kwa nchi nzima litaanza mapema kwani daftari hilo ndilo litakalotumika katika kuipigia kura katiba mpya katika kura ya maoni pamoja na uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka huu.

             Pamoja na hayo jaji LUBUVA amewataka watanzania kujitokeza kwa wingi katika zoezi hilo pindi lityaka[poanza nchi nzima kwa lengo la kujiandikisha katika daftari hilo kwani litawasaidia katika kuipigia kura katiba mpya na uchaguzi mkuu ujao.

 TAARIFA YOTE YA TUME IKO HAPA-----


Ndugu Waandishi wa Habari, Mkurugenzi wa Uchaguzi, Watendaji wa Tume, Mabibi na Mabwana.
Kwa niaba ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi, napenda kuchukua fursa hii kuwakaribisheni kwa mara nyingine katika Mkutano huu. Nawashukuru kwamba, pamoja na majukumu mengi mliyo nayo, mmeweza kuupa umuhimu wa pekee mkutano wetu huu na kuhudhuria kwa wingi. Kwa niaba ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi, nasema Ahsanteni na Karibuni sana.
Katika mkutano huu, Tume inalenga kutoa taarifa kuhusu tathmini ya utekelezaji wa zoezi la majaribio ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura (Pilot Registration) kwa mfumo wa Biometric Voters Registration (BVR) zoezi ambalo lilikamilika wiki iliyopita.
Ndugu Wanahabari,  
Tume ya Taifa ya Uchaguzi, imepewa jukumu la kisheria Kuandikisha Wapiga Kura katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na kuliboresha Daftari hilo kwa ajili ya Uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wabunge na Madiwani. Kwa mujibu wa Sheria ya Kura ya Maoni, Daftari hili la Kudumu pia litatumika katika Kura ya Maoni kuhusu Katiba Inayopendekezwa.

Ndugu Wanahabari; mtakumbuka kuwa, Tume ya Taifa ya Uchaguzi imekuwa katika mchakato wa Maandalizi ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa kutumia Teknolojia Mpya ya ”Biometric Voter Registration” (BVR) na mara kwa mara imekuwa ikiomba kukutana nanyi ili kuwapa taarifa kuhusu hatua mbalimbali ambazo Tume imekuwa ikizipitia.

Kwa kuwa Uboreshaji huu ulihusisha matumizi ya vifaa vya teknolojia ya kisasa, vifaa ambavyo vilikuwa havijawahi kutumika katika Uboreshaji nchini, tuliona si vyema kuagiza vifaa vingi kabla ya kuvifanyia majaribio. Zoezi la majaribio lilifanyika ili kuwa na uhakika kuwa vifaa hivi vya Biometric Registration vina uwezo wa kuandikisha Wapiga Kura katika mazingira ya nchi yetu. Zoezi hili liliangalia uwezo wa watendaji kutumia BVR katika uandikishaji na pia uwezo wa vyombo vyenyewe katika Software na Hardware kwenye uandikishaji. Katika zoezi hili tuliangalia changamoto zilizojitokeza ili kuzipatia ufumbuzi kabla ya kuanza Zoezi halisi la Uandikishaji wa nchi nzima.
Ndugu Wanahabari,  
Kama nilivyosema, Tume inakutana nanyi ili kuwapa taarifa kuhusu Tathmini ya Utekelezaji wa zoezi la Majaribio la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura lililofanyika kwa siku saba (7) katika Kata za Bunju na Mbweni katika Jimbo la Kawe, Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es salaam; Kata za Ifakara, Kakingiuka, Ipangala, Mlabani na Viwanja Sitini katika Jimbo la Kilombero Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero, mkoani Morogoro; na Kata za Ikuba, Usevya na Kibaoni katika Jimbo la Katavi, Halmashauri ya Wilaya ya Mlele mkoani Katavi.

Tume kwa namna ya pekee, inawashukuru sana Waandishi wa Habari kwa kujitokeza na kufuatilia zoezi hili la majaribio ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura. Waandishi wa Habari wamesaidia sana katika kuhamasisha Wananchi wa Majimbo husika kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura. Vilevile, Waandishi wa Habari wamesidia katika kutoa taarifa za maendeleo ya zoezi hili kitu ambacho kimesaidia kufanikisha zoezi hili.
Jumla ya BVR Kits 250 zilitumika katika Uboreshaji huo kwa mgawanyo ufuatao:- Halmashauri ya Kilombero BVR Kits 80, Halmashauri ya Wilaya ya Mlele BVR Kits 80 na Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni BVR Kits 90. Vituo katika Kata zote vilikuwa vinafunguliwa saa 2.00 asubuhi na kufungwa saa 12.00 jioni.

Ndugu Waandishi wa Habari, Tume inapenda kuwafahamisha kuwa zoezi hilo la Majaribio ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura katika majimbo matatu yaliyotajwa limefanyika na kukamilika kwa mafanikio makubwa. Changamoto zilizojitokeza hapa na pale zimetusaidia kupata ufumbuzi ambao utatusaidia wakati wa Uandikishaji wenyewe nchi nzima.

Tunasema mafanikio makubwa kwa sababu matokeo ya jumla yanaonyesha kuwa idadi ya wapiga kura waliojitokeza kujiandikisha ilikuwa kubwa na kuvuka malengo ya waliokadiriwa kuandikishwa.

Mkoa wa Dar es salaam, Kata za Bunju Wapiga Kura 15,123 waliandikishwa kati ya 27,148 na Kata ya Mbweni Wapiga Kura 6,200 waliandikishwa kati ya 8,278. Takwimu hizi za waliondikishwa inatokana na makisio ya watu tuliyokuwa tumejiwekea kutokana na matokeo ya sensa mwaka 2012. Mkoa wa Morogoro Kata za Ifakara, Kakingiuka, Ipangala, Mlabani na Viwanja Sitini Wapiga Kura walioandikishwa ni 19,188 wakati makisio yalikuwa watu 17,790 na Mkoa wa Katavi Halmashauri ya Mlele kata za Ikuba, Usevya na Kibaoni Wapiga Kura 11,210 waliandikishwa wakati makisio yalikuwa watu 11,394. Matokeo haya yanadhihirisha kuwa vifaa vya uandikishaji vilifanya kazi vizuri na hivyo vinaweza kutumika katika Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa nchi nzima.

Pamoja na mafanikio hayo, kama ilivyo kawaida katika majaribio yoyote kwani ndiyo lengo la kufanya majaribio, zilikuwepo changamoto kadhaa wakati wa utekelezaji wa zoezi hilo. Changamoto hizo zinaweza kuwekwa katika makundi makubwa matano kama ifuatavyo:- i. Matatizo yaliyotokana na ’Settings’ za BVR Kits; • Baadhi ya ”BVR Kits” zilitumia camera iliyo katika Laptop badala ya camera iliyowekwa kwa ajili ya kupiga picha. • Uchukuaji wa alama za vidole (Automatic Process settings) ilisababisha Mfumo kusimama (Crash). • Tatizo la kuchukua picha iwapo viwango vya ICAO vya ubora wa Picha havijafikiwa kama • Unrecognise face, • Unrecognise eye, • Stretch photo, • Un even light. • Uwepo wa Majina yenye ”apostrophe”. ii. Matatizo yaliyosababishwa na Software; • Fingeprint Scanner kusababisha Mfumo wa Uandikishaji kusimama (Crash) kutokana na SDK na za vifaa finger print scanner. • Kuharibika kwa baadhi ya file (File Corruption) kutokana na d11 ya finger print scanner. iii. Matatizo ya hardware; • Komputa (Laptop) Kupata Joto kutokana na Bati liliwekwa kuzuia kuibiwa Laptop kwa urahisi ambapo mahitaji kuwezesha mzunguko wa hewa ndani ya ”BVR Kit”. • FlashDrive ya pili (Drive G) kutoonekana hivyo kuhitaji kubadilishwa na kuwa SD card. • Uharaka wa uchukuaji alama za vidole ambapo ilibidi kufanya mabadiliko. iv. Matatizo ya lojistiki na matatizo ya Watendaji wa zoezi la Uandikishaji. • ”BVR Kit” kuchelewa kufikishwa katika Vituo. • Vurugu wakati wa uandikishaji ambao unahitaji Ulinzi kuwepo. • Baadhi ya ”BVR Operator” kutokuwa na uwezo au kuwa makini katika utumiaji wa ”BVR Kits” hivyo kuhitaji elimu zaidi kwa ”BVR Kit Operator”. • ”BVR Kit Operator” kubadili Kits kwa tatizo dogo linaloweza kutatulika kwa urahisi. • ”BVR Kit Operators” kutokuwa na uelewa wa matumizi ya ”Solar Panel” kwani baadhi ziliwekwa chini ya mti au kutogeuzwa kadri muda ulivyokuwa unakwenda. Mbali ya changamoto hizo zilikuwepo pia changamoto nyingine za kimiundombinu na kibinadamu. Miongoni mwa changamoto hizo ni pamoja na Hali ya Hewa hususan katika jiji la Dar es salaam na Morogoro. Mtakubaliana nami kuwa pamoja na kuwa jiji la Dar es salaam kwa kawaida lina hali ya hewa ya joto lakini kwa takribani mwezi mmoja hivi uliopita kumekuwa na ongezeko la joto hali iliyosababisha hata baadhi ya vifaa vya kuandikishia hususan ’BVR Kits’ wakati mwingine kushindwa kufanya kazi inavyotakiwa na hivyo kusababisha shughuli za uchapishaji wa Kadi za Kupigia Kura kuchelewa. Aidha, ushirikiano mdogo kutoka kwa Wananchi nao ulikuwa changamoto iliyosababisha zoezi hilo kwenda taratibu. Baadhi ya wananchi kushindwa kuzingatia maelekezo yaliyokuwa yakitolewa na BVR Kit Operators kutokana na uelewa duni kwani ilibainika pia kuwa bado kuna idadi kubwa ya wasiojua Kusoma na Kuandika. Hali hiyo ilifanya zoezi la Uchukuaji wa alama za Vidole (Fingerprint) na Utiaji wa Saini kuwa mgumu.
Kadhalika kumekuwepo na mwamko mkubwa kwa wananchi kujitokeza kwa wingi ili kujiandikisha. Hivyo, kulikuwepo na watu wengi sana katika vituo vya Uboreshaji wa Daftari hilo la Kudumu la Wapiga Kura. Changamoto zote zilizojitokeza kuhusiana na settings tuliweza kwa ushirikiano na watengenezaji wa vifaa hivyo, kuzipatia suluhisho wakati zoezi linaendelea. Pia chanagamoto za ’software’ nazo zimekwishapatiwa suluhisho. Changamoto kuhusu hardware zitarekebishwa wakati wa utengenezaji wa BVR Kits 7,750 ambazo zilikuwa hazijaanza kutengenezwa kusubiri matokeo ya zoezi hili la majaribio. Marekebisho hayo ya hardware pia yatafanywa katika BVR Kits 250 zilizoletwa kwa ajili ya majaribio. Changamoto kuhusu fedha na lojistiki zinaendelea kushughulikiwa kwa ushirikiano na Serikali. Kuhusu changamoto za Watendaji tunaendelea kuzishughulikia kwa kuhakikisha Watendaji tutakaowatumia wanakuwa na utaalam unaotakiwa kuziendesha BVR Kits hizo.
Ndugu Waandishi wa Habari, Napenda pia niongelee baadhi ya masuala yanayohusu zoezi la Uboreshaji wa Majaribio kwa ujumla. Kwanza ni vyema ieleweke wazi kuwa kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 na kwa ajili ya Kura ya Maoni ya Katiba Mpya, Mpiga Kura atatumia Kitambulisho cha Mpiga Kura alichopatiwa na Tume baada ya kuandikishwa katika mfumo huu tu na si vinginevyo. Vitambulisho vilivyotolewa katika uboreshaji huu wa majaribio ni vitambulisho halisi hivyo kila aliyejiandikisha katika zoezi hili la majaribio ni muhimu atunze kadi yake kwa ajili ya matumizi yaliyotajwa kwa kuwa taarifa zake tayari zimeingia katika Kanzi data ya Tume hivyo hataweza tena kujiandikisha kwa mara nyingine hata kama atabadilisha kituo cha kujiandikishia.
Ndugu Wanahabari, Pili, ni muhimu wananchi wakapata taarifa hizi kwa usahihi kwa vile wapo baadhi ya Watu wanaodhani kuwa kwa kuwa hilo lilikuwa ni zoezi la majaribio basi watakuwa na fursa nyingine ya kujiandikisha wakati wa zoezi la nchi nzima. Napenda nisisitize hapa kuwa kwa yeyote aliyejiandikisha katika zoezi hili, hatatakiwa tena kujiandikisha labda tu kwa yule ambaye atahitaji kubadilisha taarifa zake kutokana na sababu kama zilivyofafanuliwa na Tume.
Ndugu Wanahabari. Napenda nisisitize pia kuwa, Tume ya Taifa ya Uchaguzi inayo dhamira ya dhati ya kukuza demokrasia kwa kuandaa na kuendesha chaguzi zake katika mazingira rafiki na wazi yatakayotoa fursa kwa kila raia wa Tanzania aliyetimiza umri wa miaka 18 kutumia haki yake ya kikatiba ya kuchagua viongozi wake. Tume itakuwa tayari kupokea maoni na ushauri kutoka kwa wadau mbalimbali

No comments: