Mkurygenzi mtendaji wa kituo cha sheria na haki za binadamu LHRC Bi HALLEN KIJO BISIMBA akizungumza na wanahabari hao wakati akifungua mafunzo hayo ya siku moja yaliyofanyika jijini Dar es salaam leo |
Ameongeza kuwa bado nchini Tanzania kumekuwa na
matatizo mengi ambayo yamekuwa yakiwakumba wananchi yakiwemo uonevu kutoka
katika vyombo vya dola na sehemu nyingine ambayo yameku yakiwanyima wananchi
haki zao za msingi hivyo akawataka waandishi wa habari kutumia mafunzo hayo kujiingiza
katika kuwasaidia wananchi katika kupata haki za msingi.
Mtangazai wa radio free africa na star tv THOM CHILALA akisikiliza kwa makini katika semina hiyo iliyoandaliwa na LHRC leo jijini Dar es salaam |
EMELDA URIO mmoja Kati ya wawezeshaji wa leo katika semina hiyo akizungumza |
Aidha bi HELLEN amewaasa wanahabari wa Tanzania
kuacha mara moja tabia ya kutumika na watu kwa kupewa pesa ama aina yoyote ya
rushwa ili kuficha madhambi Fulani ambapo amesma kuwa kufanya hivyo ni kinyume
na sheria za nchi na maadili ya uandhishi wa habari.
Katika mafuzo hayo ambayo yameendeshwa kwa siku moja
na kuhudhuriwa na wanahabari kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini mada
mbalimbali zimewasilishwa mezani na kujadiliwa kwa pamoja .
Baadhi ya mada ambazo ziliwasilishwa katika mafunzo
hayo ni pamoja na swala la katiba pendekezwa pamoja na mchakato mzima wa
kupatikana kwake ambapo baadhi ya wanahabari na waliokuwa wanaendesha mjadala
huo wameeleza wasiwasi wao mkubwa juu ya mchakato huo wa kuipata katiba mpya
kwa kile walichodai kuwa umejawa na makosa mengi na hivyo utapelekea kupatikana kwa katiba
mbovu.
Aidha mada nyingine iliyowasilishwa ni sheria ya
kura ya maoni ambayo nayo pia imeeleezwa kuwa na vifungu ambavyo vinaashiria
wazi kuwa vitaleta vikwazo vikubwa katika mchakato wa kupata katiba mpya.
Baadhi ya wanahabari waliopata nafasi ya kuzunguma
na mtandao huu wamekiri kuwa mafunzo haya yamewafungua macho kwa kiasi kikubwa
na yatawasaidia sana katika utendaji wao wa kazi .
KWA PICHA NYINGINE ZA MAFUNZO HAYO ZIPO CHINI
No comments:
Post a Comment