Mwanachama wa chama cha Democrasia na maendeleo Chadema jimbo la ilala Bwana MUSLIM HASSANAL leo ametangaza rasmi nia yake ya
kumngoa katika kiti cha ubunge mbunge wa jimb o la ilala mh MUSA ZUNGU katika
uchaguzi ujao mwishoni mwa mwaka huu.
Hayo ameyasema muda huu Jijini Dar es salaam wakati
akirudisga Form ya kugombea ubunge katika jimbo hilo la ilala tukio
lililofanyika katika ofisi za kanda za chama hicho zilizopo kinondoni Jijini
Dar es salaam.
MUSLIM HASSANAL akionyesha FORM ambayo tayari amekwishaijaza na kuirejesha leo |
Akizungumza na wanahabari mara baada ya kurejesha
Form hiyo Bwana MUSLIM amesema kuwa lengo lake ni kuhakikisha kuwa Jimbo la
ilala linarudi katika hadhi yake ya kuwa jimbo la mfano katika majimbo yote ya
Dar es salaam ukizngatia kuwa jimbo hilo ndilo linalobeba Jina la Dar es salaam
kwa kuwa na ofisi mbalimbali na kubwa za serikali.
“Ukizngumzia uchafu Dar es salaam lazima uitaje
ilala,ukigusia ubivu wa miundombinu lazima uitaje ilala,ukitaja wananchi kuishi
kwa hali duni lazima uitaje ilala,sasa sisi kama chama tumeamua kuhakikisha kuwa
hali hii inafutika na tutalirejesha jimbo la ILALA mikononi mwetu kama ukawa
watanipa nafasi ya kugombea katika jimbo hilo”alisema mtia nia huyo
anayeonekana kujiamini sana.
MUSLIM HASSANAL akimkabidha form hiyo mratibu wa kanda ya pwani Bwana CASIMIR JUMA Mara baada ya kumaliza taratibu zote za ujazaji wa foem hiyo |
Ameongeza kuwa ukimtizama unawezaa k,udhani yeye sio
mtanzania ila kwa ufupi yeye ni mzaliwa wa Tanzania na maisha yake yote
amekulia kariakoo,hivyo anajua matatizo ya wananchi wa ilala kwa ujumla,na
amejipanga kuhakikisha kuwa anashirikiana na chama chake kwa kupitia ukawa
kuwasaidia wananchi hao.
MUSLIM HASSANAL akizngumza na wanahabari kuhusu lengo lake kwa wana ilala. |
Bwana MUSLIM HASSANAL aliwahi kugombea ubunge katika
jimbo la kigoma kaskazini uchaguzi uliopita lakini hakufanikiwa kupita ambapo
DAVID KAFULILA wa NCCR-MAGEUZI alishinda,ambapo akizunguzimzia hilo amesema
kuwa kigoma ndipo walipo babu zake na ndio maana aliwahi kugombea huko lakini
kwa sasa anadhani ni muda wa kumuunga mkono KAFULILA kwani bado anastahili
kuongoza jimbo hilo.
MTANDAO HUU UTAKUWA UNAKUPA KILA KITU AMBACHO KINAENDELEA
KATIKA VYAMA MBALIMBALI KIPINDI HIKI CHA UCHAGUZI.
No comments:
Post a Comment