Tuesday, June 30, 2015

MABERE MARANDO AWAONYA NEC 'KUTOCHEZEA' BVR DAR ES SALAAM, PWANI




Kufuatia Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuutangazia umma kuwa zoezi la uboreshaji wa Daftari la kudumu la wapiga kura liliokuwa lianze tarehe 04/07/2015 kwa Jiji la Dar es Salaam na tarehe 25/06/2015 kwa mkoa wa Pwani kwamba limeahirishwa hadi tarehe itakayotangazwa tena; Chama  cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kanda Pwani (Mikoa ya Temeke, Kinondoni, Ilala na Pwani) kinaitaka Tume ifanye yafuatayo: 


1.Tume ya Uchaguzi itangaze tarehe ya kuanza zoezi la uboreshaji wa Daftari la kudumu la wapiga kura katika Jiji la Dar es Salaam na mkoa wa Pwani baada ya kuahirishwa ili kuwasaidia wananchi kujipanga kwa zoezi zima la uandikishaji. 

2.Tume ya Taifa ya Uchaguzi izingatie mfumo wa kiuchumi na kimazingira uliopo katika  mikoa  hii  unaowafanya  watu  wengi  muda  wa  mchana  kuwepo makazini/katika  shughuli  za  kiuchumi.  Na  kupanga  muda  wakutosha  kwa kuzingatia  idadi  ya wakazi. Hii  ni  pamoja  na  kuzingatia  kuwa Jiji  la Dar  es Salaam na mkoa wa Pwani pekee, kwa takwimu za serikali, vina wapiga kura wapatao asilimia 15 ya wapiga kura wote nchini. 

3.Tume  ya  Taifa  ya Uchaguzi  ihakikishe  changamoto zote zilizotokea sehemu mbalimbali zinapatiwe ufumbuzi kabla ya zoezi halijaanza Dar es Salaam na Pwani. Changamoto hizi ni pamoja na; mashine kuwa mbovu, idadi ya mashine kutokukidhi  mahitaji,  idadi  ya  vituo  kwenye  kata  kutoendana  na  idadi  ya wanaotakiwa  kujiandikisha,  utaratibu  wa  kuchukua  majina  bila  kuzingatia waliopanga mistari, na waandikishaji kutokuwa na uwezo thabiti wa kutumia mashine  za  uandikishaji.  Uzoefu  umeonyesha  kuwa,  changamoto hizi zimeendelea kujirudiarudia katika sehemu nyingi bila kutolewa ufumbuzi wa uhakika na Tume ya Uchaguzi. 

4. Tunaitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuweka wazi mbele ya umma kuwa Jeshila  Polisi halihusiki katika kupanga utaratibu wa BVR hali inayosababishavurugu na ukosefu wa amani vituoni. Uzoefu uliopatikana wakati wa ziara za viongozi wakuu wa chama kukagua zoezi la BVR katika maeneo mbalimbali unaonesha kuwa maeneo yote ambayo polisi hawakuwepo vituoni wakati wa uandikishaji,  utaratibu  ulikwenda  kwa  utulivu  lakini  hali  imekuwa tofauti kabisa kote ambako jeshi hilo limehusika kusimamia uandikishaji

 Mf; Arusha  Tunapeda  kusisitiza  kuwa;  CHADEMA  haitofumbia  macho  mikakati  yoyote itakayoonekana  ina  dhamira  ya  kudhoofisha  zoezi  la  uandikishaji  ambayo itasababisha  kuwanyima  wananchi  haki  ya  kikatiba  ya  kupiga  kura,  maana  bila kujiandikisha mtu hawezi kupiga kura. 
Mwisho,  CHADEMA  inapenda  kuwahamasishwa  wananchi  kujitokeza kwa wingi wakati wa zoezi la uandikishaji litakapoanza katika Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa Pwani. Asanteni! 


IMETOLEWA NA  Mhe. MABAERE N. MARANDO MWENYEKITI WA CHADEMA KANDA YA PW

No comments: