Wednesday, June 17, 2015

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGA RASMI MATANGAZO YA TELEVISHENI YA MFUMO WA ANALOJIA.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akibofya kitufye cha Lap Top kuashiria kufunga rasmi Matangazo ya Televisheni ya Analojia, baada ya kufikia ukomo rasmi hii leo Juni 17, 2015 baada ya kufanikiwa kuzima mitambo ya Analojia kwa nchi nzima. Sherehe hizo za ukomo zimefanyika leo kwenye Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dkt. Fenella Mukangara. Picha an OMR

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Tuzo ya Heshima za Digital Tanzania, Bi. Asteria Kamara, kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, wakati wa sherehe za Ukomo wa Matangazo ya Televisheni ya Analojia, zilizofanyika leo Juni 17, 2015 kwenye ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Prof. Makame Mbarawa. Picha na OMR

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Tuzo ya Ngao ya Heshima za Digital Tanzania, Mkurugenzi Mkuu wa Mawasiliano Tanzania, TCRA, Prof, John Nkoma, wakati wa sherehe za Ukomo wa Matangazo ya Televisheni ya Analojia, zilizofanyika leo Juni 17, 2015 kwenye ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Prof. Makame Mbarawa. (wa pili kulia) ni Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo , Dkt. Fenella Mukangara. Picha na OMR 
- Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati wa sherehe za Ukomo wa matangazo ya Televisheni ya Analojia, zilizofanyika leo Juni 17, 2015 kwenye Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam. Picha na OMR

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, Prof. John Nkoma, wakati wa sherehe hizo. Picha na OMR

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Tuzo ya Ngao ya Heshima za Digital Tanzania, Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Prof, Makame Mbarawa, wakati wa sherehe za Ukomo wa Matangazo ya Televisheni ya Analojia, zilizofanyika leo Juni 17, 2015 kwenye ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam. Wa pili (kulia) ni  Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo, Dkt. Fenella Mukangara. ( kulia) ni Mkurugenzi Mkuu wa Mawasiliano Tanzania, Prof. John Nkoma. Picha na OMR

No comments: