Friday, June 19, 2015

PICHA 50--LOWASA AWEKA HISTORIA MBEYA,YA ARUSHA YAJIRUDIA TENA

 Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akitoka nje ya Uwanja wa Ndege wa Songwe na kulakiwa na umati wa WanaCCM wa Mkoa wa Mbeya
 Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akisalimiana na Kijana Mwenye ulemavu, Ernest Mhagama aliekuja kumpokea katika Uwanje wa Ndege Songwe, Jijini Mbeya leo Juni 19, 2015.

 Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akiwapungia wanaCCM wa Mkoa wa Mbeya.

 Shangwe kwa wanaCCM wa Mji wa Mbalizi, Mbeya Vijijini.
 Mh. Lowassa akiteta jambo na Katibu wa CCM Wilaya ya Mbeya Vijijini.
 Umati wa wanaCCM wa Mji wa Mbalizi jijini Mbeya.
 Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akipokea fomu za WanaCCM zaidi ya elfu tisa wa Wilaya ya Mbeya Vijijini kutoka kwa Katibu wa CCM wa Wilaya hiyo, Mary Kalinze.
 Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akizungumza na WanaCCM wa Wilaya ya Mbeya Vijijini, kwenye mji Mdogo wa Mbalizi wakati aliposimama kuwasalimia.
  Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akiwasalimia wanaCCM na Wananchi wa Mji wa Mbalizi jijini Mbeya waliojitokeza kumlaki.
 
Hivi ndivyo hali ilivyokuwa njiani.
 "Hamjambo wanaMbeyaa....."
 Umati wa watu wa CCM Mkoa wa Mbeya.
Umati wa WanaCCM pamoja na Wananchi wa Mkoa wa Mbeya, wakiwa wamemzunguka, Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa (katikati), wakati alipowasili kwenye Ofisi za CCM Mkoa wa Mbeya leo Juni 19, 2015, kukabidhiwa fomu zitakazomuwezesha kupata ridhaa ya Chama chake kuwania Urais kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015. Mbeya wamevunja rekodi udhamini kwa Mh. Lowassa ya mikoa yote aliyopita, amepata wadhamini 53,156 kwa mkoa wa Mbeya pekee.
 Furaha ya Mh. Edward Lowassa kwa wanaCCM na Wananchi wa Mkoa wa Mbeya, hata haikujificha pale alipata mapokezi makubwa ambayo hata yeye hakuyategemea.
 Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akipunga mkono kwa Umati wa WanaCCM pamoja na Wananchi wa Mkoa wa Mbeya, waliofurika kwa wingi wao kwenye Uwanja wa Ofisi za CCM Mkoa wa Mbeya, wakati alipowasili kwenye Ofisi hizo leo Juni 19, 2015, tayari kwa kupokea fomu za WanaCCM 53,156 wanaliomdhamini ili apate ridhaa ya Chama chake kuwania Urais kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015.
 Hakuna kwa kukanyaga, ukitoa mguu mwingine kaweka.





 Muimbaji wa nyimbo za Injili, Bahati Bukuku akiwasalimia wanaCCM wa Mkoa wa Mbeya.

 Katibu wa CCM Mkoa wa Mbeya, Mwangi Kundya akizungumza machache.
 Katibu wa CCM Wilaya ya Mbeya Mjini, Kulwa Milonga akisoma idadi ya wanaCCM waliomdhamini Mh. Edward Lowassa Mkoa wa Mbeya.
 WanaCCM wa Mkoa wa Mbeya wakifatilia kwa makini.
 Shangweeeeee....
  Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania, Mh. Edward Lowassa akizungumza machache na kutoa shukrani kwa WanaCCM na Wananchi wa Mkoa wa Mbeya waliofurika kwa wingi kwenye Uwanja wa Ofisi za CCM Mkoa wa Mbeya, leo Juni 19, 2015.


 Mh. Lowassa akisalimiana na Mkuu wa Machifu wa Mkoa wa Mbeya.
 Akisalimiana na wazee Machifu wa Mkoa wa Mbeya.
 Mkuu wa Machifu wa Mkoa wa Mbeya akitoa baraka zake kwa Mh. Lowassa.
Picha ya Pamoja na Machifu wa Mkoa wa Mbeya. 
 Picha ya Pamoja na Wamasai wa Mkoa wa Mbeya.


PICHA NA HABARI CREDIT MICHUZI BLOG

No comments: