Wednesday, July 1, 2015

MWANAMUZIKI MUZAMAMOYO APANIA KUPAA KIMATAIFA,AELEZA MIPANGO YAKE

Mwanamuziki wa kizazi kipya nchini mwenye asili ya kitaliano Kris Muzamamoyo wa kwanza kulia  akiwa na kundi lake la Fantastic Seven,kushoto nyuma Man ngingo(mwnye kepu) Ainea mwenye  (Tshit nyekundu),na kulia ni Bs Master.Picha na Mpiga picha wetu.

MWANAMUZIKI wa muziki wa kizazi kipya nchini Tanzania  mwenye asili ya kitaliano Christian Revbaer 'Muzmamoyo' amesema kuwa 
bajeti nzuri walizonazo wanamuziki wa kimataifa akiwemo Sean 
Comb 'P Didy' ndiyo sababu zinazowafanya waonekane bora 
hivyo yupo radhi kutumia fedha nyingi ili kufikia kiwango cha 
kimataifa.

Hayo ameyasema leo alipokuwa akizungumza 
na Mwandishi wa Habari24 blog Dar es salaam aliyetaka kujua  mpango wan mwanamuziki huyo ambapo amemueleza kuwa yupo radhi kuwekeza pesa nyingi ili kufanya kazi yenye ubora.

Amesema kuwa kuna haja ya wadhamini nchini zikiwepo kampuni za vinywaji pamoja na makampuni ya simu kuwekeza fedha za kutosha katika tasnia ya muziki kwa kuwa  ni eneo linalotoa ajira nyingi kwa vijana wa sasa badala ya kutazama tu mpira wa miguu.

Hata hivyo ameongeza kuwa mpaka sasa ni muzik pekee ndio anayeipeperusha bendera bendera ya Tanzania katika mataifa mengine.

No comments: