Tuesday, August 18, 2015

Kampuni ya Swala yaahidi makubwa, mwaka mmoja baada ya kuingia katika soko la hisa

    Mkurugenzi Mtendaji wa  Kampuni ya Mafuta na Gesi ya Swala (Tanzania) PLC, David Mestres Ridge (kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam, kuhusu kampuni yake kutimiza mwaka mmoja tangu iingie katika soko la hisa (IPO) ambapo Swala iliingiza jumla ya hisa za kawaida 9,600,000, kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa ARCH Financial $ Investment Advisory Limited,Iyen Nsemwa. 

Kampuni ya uchimbaji mafuta na gesi ya Swala Energy leo imetimiza mwaka mmoja tangu kuingia katika soko la hisa (IPO) huku ikiahidi makubwa katika sekta hiyo.
Swala Energy ni kampuni ya kwanza ya uchimbaji nishati hizo kuingia katika soko la hisa la Dar es Salaam (DSE) na kuwapa nafasi Watanzania kuweza kununua hisa na kuwa wamiliki wa kampuni hiyo.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa Swala Energy Bw. David Mestres Ridge, Swala Energy ambayo hivi karibuni iliuza asilimia 25 ya hisa zake kwa kampuni ya Tata Petrodyne Ltd, mbali ya hilo mwanzoni mwa mwezi August kampuni ya Swala ilipewa kibali na Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini (TPDC) ili kuvuna asilimia 50 ya mapato katika leseni zake za Kilosa na Pangani.

Kwa mujibu wa Bw. Ridge, kinachosubiriwa kwa sasa ni ruhusa kutoka Tume ya Ushindani isiyofungamana na upande wowote (FCC) ili kuanza utekelezaji huo, “tuna imani ya kwamba ridhaa kutoka FCC itakuja hivi karibuni ili tuanze utekelezaji wa mipango yetu.”


Chini ya makubaliano haya, TPL itazalisha kwa niaba ya Swala ambapo mikakati yote itakuwa tayari kutekelezwa, “ninawashukuru sana Wizara ya Nishati na Madini kwa kuturuhusu kufanya utafiti na kuchimba nishati hizi, tunaahidi kuwafanyia Watanzania makubwa zaidi pindi tukianza uchimbaji.”

No comments: