Monday, March 7, 2016

WAKAZI MTWARA WAMEFANYA HILI WALIPOMWONA NAIBU WAZIRI WA MAJI

Wakazi wa kijiji cha Nangoo jimbo la Ndanda wilaya ya Masasi wamelazimika kusimamisha msafara wa naibu waziri wa maji, Eng Isack Kamwele kutikana na kukosekana na maji kijijini hapo kwa muda mrefu ingawa ingawa mradi wa Mbwinji unaanzia kijijini hapo na kuelekea wilayani Nachingwea mkoa wa Lindi.
 
Wananchi hao walibeba mabango yaliyoelezea kukosekana kwa maji na mengine kuuziwa bei ya Sh500 katika vioski ambavyo vingi vimefungwa hivyo wananchi wengine kutumia maji ya visima yasiyo salama.

Akitoa malalamiko kwa niaba ya wanakijiji Bakari Amani alisema kuwa gharama za maji zimekuwa kubwa kuanzia kuunganishiwa pamoja na matumizi ya kila siku.
"Lugha ya wakala wa Mwanawasa inatukera eti anasema tunapata maji kwa huruma..pia bei ya maji kwa unit moja ni kubwa mno wapo wanaolipa Sh 1,000 na Sh 2,000 kwa unit,"alisema Amani
Hata Hivyo Naibu Waziri Eng  Kamwelwe ameahidi kurudi kijijini hapo na kutoa ufafanuzi baada ya siku moja kutokana na kuwa nyuma ya ratiba iliyowekwa.

"Hiki mlichonipa Mheshimiwa mbunge tayari amenieleza na mimi nitaifanyia kazi lakini kabla lazma nije kuongea na nyinyi Kwa sababu ya Ratiba nakimbia Nanyumbu Kesho asubuh naamkia Masasi,"alisema Eng Kamwelwe
Hata hivyo mbunge wa Jimbo hilo Cecil Mwambe aliwaomba wanakijiji hao kuruhusu msafara huo kuondoka kutokana na ahadi ya Naibu wazir huyo ambayo ilionekana kuleta matumaini ya upatikanaji wa maji kijijini hapo.
"Tunaomba mruhusu msafara tunakuja kufanya mkutano na nyinyi kesho kujadili maswala ya maji,"alisema Mwambe

No comments: