Wednesday, May 25, 2016

MATUKIO KATIKA PICHA BUNGENI DODOMA.


 Mbunge wa jimbo la Nkasi Kaskazini (CCM) Mhe. Allya Kessy akizungumza jambo na Mbunge wa jimbo la Kawe (CHADEMA) Mhe. Halima Mdee nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma leo.
 Mwekekezaji na Msambazaji wa nguzo za umeme nchini kutoka Kampuni ya New Forest iliyoko mkoani Iringa akiwaonesha jambo Mbunge wa Nkasi Kaskazini Mhe. Ally Kessy (kushoto) na Mbunge wa jimbo laKilolo Mhe. Venance Mwamoto kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma.
 Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Prof. Jummanne Maghembe (kushoto) na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Mhandisi Ramo Makani waifuatilia hoja mbalimbali za wabunge wakati wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo Bungeni Dodoma.
  Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Prof. Jummanne Maghembe (kushoto) na
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Mhandisi Ramo Makani
waifuatilia michango mbalimbali ya wabunge wakati wakichangia Hotuba ya
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo Bungeni Dodoma.
 Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Hussein Mwinyi akifuatilia kwa makini mjadala wa Waheshimiwa Wabunge wakati wa kipindi cha maswali na Majibu.
 Mbunge wa Bunda Mjini Mhe. Esther Bulaya akichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii ndani ya Ukumbi wa Bunge mjini Dodoma leo
 Mwenyekiti wa Bunge ambaye pia ni Mbunge wa Bariadi Magharibi Mhe. Andrew Chenge akiongoza kikao cha Bunge leo mjini Dodoma.
Baadhi ya Wananchi kutoka jamii ya Wafugaji waliohudhuria kikao cha Bunge leo mjini Dodoma kushuhudia Michango ya Wabunge wakati wa Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii mjini Dodoma leo.
Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.Hamis Kigwangala akijadiliana jambo na Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa Bunge Bw. Owen Mwandumbya (kulia) na Mwandishi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Bw. Elisha Eliya leo mjini Dodoma.

Picha/Aron Msigwa – MAELEZO

b7
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Selemani Jafo  akiingia ndani ya Bunge mjini Dodoma kuhudhuria vikao vya bunge hilo leo 25 Mei, 2016.
b5Mbunge wa Viti Maalum CCM , Mhe. Halima Bulembo akiwasili viwanja vya Bunge mjini Dodoma kuhudhuria vikao ndani ya bunge hilo leo 25 Mei, 2016.
b4Mbunge wa Bukoba Mjini CHADEMA , Mhe. Wilfred Lwakatare akiwasili viwanja vya Bunge mjini Dodoma kuhudhuria vikao ndani ya bunge hilo leo 25 Mei, 2016.

b3Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage akiingia ndani ya Bunge mjini Dodoma kuhudhuria vikao vya bunge hilo leo 25 Mei, 2016.
b6Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Mhe. Luhaga Mpina (kushoto)  akiwa ameongozana na Wabunge wenzie  wakielekea ndani ya Bunge mjini Dodoma kuhudhuria vikao vya bunge hilo leo 25 Mei, 2016.
b1Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye (kushoto) akiwa ameongozana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah Kairuki wakiwasili katika Viwanja vya Bunge leo Bungeni mjini Dodoma 25 mEI, 2016.
b2Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi (kushoto) akiwa ameongozana na Wabunge wenzie  wakielekea ndani ya Bunge mjini Dodoma kuhudhuria vikao vya bunge hilo leo 25 Mei, 2016.
PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA, MAELEZO, DODOMA.

No comments: