Tuesday, July 5, 2016

LHRC WATOA TATHMINI YA BUNGE LA BAJETI MWAKA HUU,WABAINISHA CHANGAMOTO KADHAA.SOMA HAPA

Kaimu  mkurugenzi wa kituo cha sheria na haki za binadamu nchini Tanzania LHRC Bi IMELDA LULU URIO akifafanua jambo kuhusu Tathmini ya mwenendo wa Bunge la Bajeti lililokuwa linaendelea ambapo kituo chao walikuwa wakifwatilia mwenendo wa bunge hilo kwa ujumla
 Na Exaud Mtei
Wakati bunge la bajeti la Tanzania likimalizika Mjini Dodoma na kushughudia bajeti ikipitishwa hatimaye Kituo cha sheria na haki za binadamu nchini Tanzania LHRC kimetoa tathmini yake juu ya bunge hilo huku ikionyesha baadhi ya kasoro ambazo zilijitokeza huku wakiutaka uongozi wa bunge kuzifanyia kazi kwani zimetia doa shughuli za bunge hilo.

Bunge la mwaka huu limemalizika huku kukiwa na msuguano mkali wa kisiasa na kiuongozi ambapo hadi mwisho wa bunge hilo ulishughudiwa wabunge wa vyama vya upinzani wakisusa kushiriki katika vikao vyake kwa kile walichokiita kutokuwa na Imani na Naibu Spika wa bunge hilo Mh TULIA AKSON.
Akizungumza na wanahabari leo Jijini Dar es salaam Kaimu  mkurugenzi wa kituo cha sheria na haki za binadamu nchini Tanzania LHRC Bi IMELDA LULU URIO ametaja baadhi ya mambo ambayo wao kama wafwatiliaji wa shughuli za bunge hilo yalitia doa katika uendeshaji wa bunge hilo.
Akitaja baadhi ya mambo hayo amesema kuwa swala la haki ya kupata habari lilikuwa ni changamoto kubwa kwa bunge hilo kutokana na kwa mara ya kwanza serikali kusitisha urushwaji wa matangazo ya bunge Live kwa kile walichokiita kubana matumizi jambo ambalo amesema kuwa limekuwa ni moja ya kikwazo kikubwa cha wananchi kupata habari huku akiishauri serikali kufikiria upya swala hilo ili kuhakikisha kuwa wananchi wanapata nafasi ya kupata habari kwa uhuru na uhakika kama ilivyokuwa awali.


Amesema kuwa katika bunge la bajeti pamoja na serikali kuanzisha mfumo mpya wa kurusha matangazo hayo kwa kuyarekodi na kuyarusha wakati wa usiku bado nafasi hiyo sio Rafiki kwa wananchi walio wengi kwani muda wa usiku wananchi wengi wanakuwa hawapati nafasi ya kusikiliza na kuangalia vipindi hivyo huku akiongeza kuwa sio jukumu la bunge kurusha matangazo hiyo ni kazi ya vyombo vya habari na bunge kazi yake ni kuishauri na kuikosoa serikali.
IMELDA ametaja kasoro nyingine ambazo zilionekana katika bunge hilo ni swala la wabunge kutotimiza wajibu wao kwa wananchi,ambapo katika bunge hilo imeonekana wazi kuwa wabunge wengi hasa wa chama tawala wamekuwa wakitetea sana maslahi ya chama chao na kusahau kabisa maslahi ya nchi na kuibua hoja za kuisaidia jamii kwa ujumla.

Amesema pia swala la wabunge wa vyama vya upinzani kugomea vikao vya bunge kwa kipindi chote cha mjadala wa bajeti na kusababisha bajeti ya Tanzania kupitishwa na wabunge 252 kati ya wabunge wa 384  kumewanyima wananchi haki ya uwakilishwa na wawakilishi wao waliowachagua.
Wanahabari mbalimbali wakifwatilia mkutano huo
Mambo mangine ambayo yametajwa kama kasoro katika bunge hilo ni pamoja na kukosekana kwa umoja wa bunge kama muhimili,kukosekana heshima na kuheshimiana baina ya wabunge ambapo mijadala mingi ilitawaliwa na vijembe,matusi na kukashifiana ambapo maswala hayo yamekuwa yakiwaudhi wananchi.


Kukiukwa kwa kanuni za bunge na matumizi mabaya ya muda wakati wa uchangiaji nazo zimetajwa kama changamoto kubwa katika bunge hilo  ambapo kwa mujibu wa kanuni za bunge mbunge ataweza kuchangia mwisho ni muda wa dakika 60 laini katika bunge hilo ilishighudiwa wabunge wakizidisha muda lakini kumekuwa hakuna hatua zilizochukuliwa.
Katika hatua nyingine LHRC wameutaka uongozi wa bunge kupitia kwa spika na Naibu Spika kuhakikisha kuwa wanatatua migogoro iliyowagawa wabunge kwa njia ya Amani huku wakihakikisha kuwa sheria na kanuni za bunge zinafwatwa na wabunge wote wa Tanzania.

No comments: