Friday, September 16, 2016

MATUKIO MBALIMBALI BUNGENI WAZIRI MKUU AKILIAHIRISHA BUNGE MPAKA NOVEMBA 1, 2016

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akilihutubia Bunge kabla ya kutoa kauli ya kuliahirisha bunge hilo mpaka tarehe 1 Novemba 2016 ambapo mbali na mambo mengine amesema serikali itaendelea kutekeleza yale iliyoyaahidi na kuwashukuru wadau mbalimbali wanaoendelea kujitolea kuwasaidia waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera, wakati wa kikao cha nane cha Bunge la kumi na moja la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wakiimba wimbo wa taifa baada ya Waziri Mkuu kuliahirisha Bunge hilo mpaka tarehe 1 Novemba 2016, Leo Mjini Dodoma.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai akitoka katika ukumbi wa Bunge baada ya Waziri Mkuu kuliahirisha Bunge hilo mpaka tarehe 1 Novemba 2016, Leo Mjini Dodoma.

Baadhi ya Wabunge wakibadishana mawazo na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa baada ya kuliahirisha Bunge hilo mpaka tarehe 1 Novemba 2016, Leo Mjini Dodoma.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akiteta jambo na Mbunge wa Jimbo la Ubungo Mhe. Said Kubenea, baada ya Waziri Mkuu kuliahirisha Bunge hilo mpaka tarehe 1 Novemba 2016, Leo Mjini Dodoma.

No comments: