Monday, May 22, 2017

NIMEFANYIWA UPASUAJI MARA TISA (9) LAKINI BADO,WATANZANIA NISAIDIENI.

 
Habari Ndugu Mtanzania Mzalendo,Kwa majina Naitwa Exaud Mtei,Mwandishi wa Habari nchini Tanzania,kwa Masikitiko makubwa Imebidi niwe Balozi wa Kusambaza Ujumbe huu ambao nimeupata kutoka kwa mwalimu wa shule ya Kawe Ukwamani akinieleza Kuhusu maisha ya mwanafunzi wake wa Kidato cha Nne ambaye anashindwa kundelea na masomo kutokana na Matatizo yanayomkumba-

HUU NI UJUMBE WA MWALIMU HUYO--
HABARI KAKA-Kuna mwanafunzi wangu anaitwa Mariam Ibrahimu Mwema wa shule ya sekondari Kawe ukwamani kidato cha 4 mwenye umri wa miaka 16 tu ana matatizo makubwa ya tumbo. Alifanyiiwa opereshen ya kwanza  akiwa darasa la 3. Baadae  upasuaj uliendelea takriban mara 9.    
                   
Hali yake kiafya imezorota tena baada ya kuimarika katika miezi 2 Iliyopita kufuayia operation aliyofanyiwa pale Muhimbili .Ilikuwa ni operation ya kumi kwa huyu binti mwenye umri chini ya miaka 18                       
Dogo kwa sasa ni wa kutapika tu, tumbo limevimba tena na kitu kiumizacho zaidi ni kuwa FAMILIA YAKE IPO TAABANI KIUCHUMI KWA SASA...!                     Anaumwa kiukweli dogo hata kukaa hawez..!                       

Pleeeeease wadau hebu kila mmoja wetu afikirie nini anachoweza kumfanyia malaika huyu kunusuru kiza  kinene cha mustakabali wake kimaisha. Kiukweli wazazi wake wamefikia hatua ya kutokujua hatma ya mtoto wao kipenzi. 
                      
Wazazi hawana kitu imebaki ni kumtazama tu, mtoto Analia wazazi wanalia basi ni tafrani Inaumiza sana pale Mariam anapokuambia japo kama ingekuwa inawezekana basi yeye akupatie nafsi yake nawe umpatie yako japo kwa masaa 2 ( dakika 120) japo naye apumzike maumivu kwa muda huo.
  
Msaada unaohitajika kwa sasa ni Matibabu ya haraka nje ya nchi kwa mujibu wa maelezo ya madaktari. Na kwa msaada wa madaktari wa Tmj, Sanitas na Shree Hindumabdal hospital tulifanikiwa kupata mawasiliano, hospital na daktari ambaye alitupatia gharama za natibabu ya tatizo la mtoto wetu sambamba na gharama nyingine kuwa ni takriban dola elfu nane ( 8000) za marekani.                
    



Please wadau hata kwa kuwashirikisha watu wengine na taasisi mnazozifahamu tumnusuru huyu MALAIKA...!  SANAHANI KWA MAKALA NDEFU. NI MIMI MWALIMU MLEZI WA MARIAMU IBRAHIMU MWEMA. Kwa mawasiliano zaidi piga namba hii ya mama yake 0685379888 ASANTENI 
                      
Picha nilizoambatanisha ni Picha za Mariamu Ibrahimu Mwema siku chache kabla ya upasuaji kwa mara ya kumi.!

TUUNGANE KUSAMBAZA UJUMBE HUU NA KUMCHANGIA KWA HALI NA MALI KUFANIKISHA SWALA HILI

Kwa mawasiliano Zaidi—

Mama wa Mtoto -0685379888

Mwalimu wa mtoto huyo Kawe Ukwamani- 0683916283

Au ukihitaji Zaidi Kuwasiliana na Msambaza Ujumbe huu ni 0712098645



ASANTEN TUSAIDIANE KUOKOA UHAI WA MTOTO MARIAM.
Mariam Ibrahimu Mwema wa shule ya sekondari Kawe ukwamani akiwa amelala Kitandani,anahitaji msaada wa Watanzania wote kwa sasa.

No comments: