Monday, July 10, 2017

MSTAHIKI MEYA WA JIJI LA DAR ES SALAAM ISAYA MWITA AMTEMBELEA KARDINAL PENGO

MSTAHIKI Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita amtembelea Askofu wa Jimbo kuu Katoliki la Dar es salaam Mwadhama Polycarp Kardinal Pengo ofisini kwake leo, Kanisa la Mtakatifu Joseph jijini leo baada ya kutoka nje kwa matibabu. Kardinali Pengo alirejea nyumbani mwezi uliopita akitokea Marekani.

Mstahiki Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita akisalimiana na Askofu Mkuu wa jimbo Katoliki la Dar es Salaam Mwadhama Polycarp Kardinal Pengo alipomtembelea ofisini kwake mapema leo

Askofu Mkuu wa jimbo Katoliki la Dar es Salaam Mwadhama Polycarp Kardinal Pengo akizungumza na Mstahiki Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita kuhusu hali ya afya yake alipomtembelea leo ofisini kwake katika Kanisa la Mtakatifu Joseph.

Mstahiki Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita akipata baraka kutoka kwa Askofu Mkuu wa jimbo Katoliki la Dar es Salaam Mwadhama Polycarp Kardinal Pengo alipomtembelea ofisini kwake leo.



No comments: