Sunday, November 19, 2017

MATEMBEZI YA HIARI YA KUMUENZI MTUME MOHAMMAD S.A.W YAFANYIKA LEO JIJINI DAR ES SALAM

Watanzania wametakiwa kuwa ni watu wenye upendo, mshikamano na umoja ili kuendelea kuidumisha Amani tuliyonayo ambayo ni kama  Tunu tuliyojaliwa Watanzania.
Hayo yamesemwa mapema leo jijini Dar es salaam na Sheikh Mkuu wa dhehebu la Shia ithanasheria Maulana Hemed Jalala, ikiwa leo ni maadhimisho ya siku ya kumuenzi Mtume Mohammad S.A.W.

Maadhimisho hayo yaliyoadhimishwa kwa kuwa na mtembezi ya hiari yaliyoanzia kituo cha mabasi cha Ilala Boma na kwenda mpaka makao makuu ya Dhehebu la Shia Tanzania yaliyopo eneo la Kigogo Posti jijini Dar es salaam.
Sheikh Jalala alisema kuwa lengo la matembezi hayo ni kukumbuka na kumuhenzi Mtume Mohammad ambaye alifariki miaka takribani 1400 iliyopita, lakini leo hii anakumbukwa kwa mengi mazuri aliyoyatenda akiwa hapa duniani.

Aidha Sheikh Jalala alisema kuwa licha ya kuwa mtume alikuwa ni Nabii na kiongozi wa Waislamu lakini alipendwa na watu wa dini zote kwa kuwa alishirikiana nao na hakuwabagua kutokana na dini zao, kabila, rika wala rangi na alishirikiana nao watu hao katika maisha yake yote mpaka kufa kwake.
Lakini pia hii inatufundisha sisi kama watanzania kupendana kushirikiana kuondoleana visasi pamoja na chuki zisizo na msingi au kutengana kutokana na itikadi za kidini, kuwekea na vikwazo kati ya wakristo na waislamu au watu wa dini nyingine ila tunatakiwa tupendane, tushirikane na tulinde amani yetu kwani sisi sote ni watanzania.

Sheikh huyo aliendelea kwa kusema kuwa mtume alikuwa hapendi kuona mtu yeyote akionewa aidha awe Muislamu, Mkristo, Muyahudi hata Mpagani bali yeye alimtetea kwa kuwa ni mwanadamu, lakini pia alionyesha kuwajari yatima na wajane na kuwapa utetezi ili na wao wawe na amani na furaha kama watu wengine katika dunia.
Na mwisho kabisa Maulana Jalala alipenda kuwashauri viongozi wa dini zote ikiwemo Masheikh, Maimamu, Mapadri, Wachungaji na maaskafu kote nchini kufundisha na kuubiri amani na mshikamano kwa taifa letu ili tuendelee kuilinda Amani yetu tuliyojaliwa na Mwenyezi Mungu kama Tunu yetu.


No comments: