Thursday, November 16, 2017

SOMA HAPA TAMKO LA ACT WAZALENDO KWA SERIKALI YA AWAMU YA TANO

CHAMA cha ACT-Wazalendo kimeainisha mambo tisa ambayo Serikali ya awamu ya tano  imefanya vibaya katika miaka miwili ya uongozi wa Rais John Magufuli.
Picha inayohusiana

Mwenyekiti wa chama hicho, Yeremia Maganja, akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam amesema  mambo hayo yamegawanywa katika mafungu makuu matatu.

“Leo tutatoa tathmini yetu ya miaka miwili ya utawala huu, tathmini hii ni zao la utafiti husika uliofanyika nchi nzima. Tathmini yetu itaainisha mambo 9 ambayo tunaamini hayakufanywa vizuri kabisa na Serikali,” amesema Maganja.

“ACT Wazalendo inao wajibu wa kujihusisha na masuala ya watu, tunatimiza wajibu huo kwa tathmini hii ya kuangazia mambo haya risa ambayo ni mapungufu ndani ya miaka miwili hii ya utawala huu,”ameongeza.

Amesema mambo hayo yamefanya vibaya kiasi cha kuleta athari nchini, kisiasa, kiutawala na kiuchumi.

Ametaja maeneo hayo kuwa ni ya, Haki za Msingi  Usimamizi wa Uchumi na Uendeshaji wa Nchi.

Haki za Msingi 
Maganja amesema  kumekuwepo na uminywaji wa uhuru wa Vyama vya Siasa Kufanya mikutano ya hadhara, uhuru wa Vyombo vya habari, pamoja na Uhuru wa Kujieleza, Kuminywa kwa haki ya wazanzibari kuchagua viongozi wao na Kupuuzwa kwa matakwa ya Katiba Mpya.


Usimamizi wa Uchumi wa Nchi

Amesema kumekuwepo kwa hali ya Kusinyaa kwa Uchumi wa Nchi, Kudhohofishwa kwa Sekta Binafsi,  Mazingira Mabaya ya Biashara Nchini, pamoja Kupaa kwa Deni la Taif.

Mengine ni kutelekezwa kwa kilimo na utekelezaji wa miradi mikubwa bila kuzingatia maslahi ya umma.

Uendeshaji wa nchi

Mwenyekiti huyo amesema katika kipengele hiki serikali hii imefanya vibaya kwa uvunjaji wa misingi ya Sera ya Mambo ya Nje, unyanyasaji wa watumishi wa umma na utawala unaovunja taasisi za kikatiba na kisheria kutoakana na kwamba utawala huu umekuwa wa mtu mmoja.

No comments: