Friday, May 2, 2014

USIPITWE NA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI MAY 03, 2014



HIVI NDIVYO UKAWA ILIVYOFUNIKA PEMBA LEO

Kiongozi wa UKAWA Freeman Mbowe, akihutubia katika mkutano wa hadhara katika viwanja vya Gombani ya Kale, Chake Chake Pemba.
Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi James Mbatia, akihutubia katika mkutano wa hadhara katika viwanja vya Gombani ya Kale, Chake Chake Pemba. 

Mwenyekiti wa CUF Prof. Ibrahim Lipumba, akihutubia katika mkutano wa hadhara katika viwanja vya Gombani ya Kale, Chake Chake Pemba.
Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad, akihutubia katika mkutano wa hadhara katika viwanja vya Gombani ya Kale, Chake Chake Pemba.

MALAWI YAWASILI, KIINGILIO 5,000/

Timu ya Taifa ya Malawi (Flames) imewasili jijini Mbeya tayari kwa mechi ya kirafiki dhidi ya Taifa Stars itakayochezwa Jumapili (Mei 4 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine.

Flames ikiwa na msafara wa watu 31 imewasili jana (Mei 1 mwaka huu) saa 1 jioni kwa njia ya barabara, na imefikia hoteli ya Manyanya. Nayo Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ipo jijini Mbeya tangu Aprili 27 mwaka huu kujiandaa kwa mechi hiyo.

Kiingilio katika mechi hiyo kitakuwa sh. 5,000 wakati tiketi zitauzwa siku ya mchezo kuanzia saa 2 asubuhi katika vituo vya Uyole, Mwanjelwa,, Mbalizi, Stendi Kuu, Holiday Inn na Uwanja wa Sokoine.

Magari yatakayoruhusiwa kuingia uwanjani ni ya wachezaji, gari la wagonjwa, gari la zimamoto na gari la waamuzi pekee.


BONIFACE WAMBURA

OFISA HABARI NA MAWASILIANO

SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)


PICHA-MBIO ZA MWENGE WA UHURU ZAZINDULIWA RASMI HUKO KAGERA,TAZAMA PICHA MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AKIWASHA MWENGE


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwasha Mwenge wa Uhuru wakati wa Sherehe za uzinduzi wa mbio za Mwenge huo zilizofanyika kwenye Uwanja wa Kaitaba, mjini Bukoba Mkoa wa Kagera leo Mei 2, 2014. Mwenge huo unatarajia kuhitimisha mbio zake Oktoba 14 mkoani Tabora, ambapo zinatarajia kufungwa na mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete.

HAWA NDIO WALIOJITOKEZA LEO NA KUMTAKA RAIS AFUTE KIKUNDI CHA UAMSHO MARA MOJA


Hamad Tao
    Na Exaud mtei
         
       Rais wa jamhuri ya muungano Tanzania dk JAKAYA MRISHO KIKWETE ametakiwa  kuchukua hatua kali  dhidi ya kikundi cha mihadhara ya kiislam Tanzania maarufu kama UAMSHO ikiwa ni pamoja na kikifuta kikundi hicho kwa kile kinachodaiwa kuwa ni kikundi hatari na hakiitakii mema nchi ya Tanzania
        
           Hayo yamesemwa leo jijini dar es salaam na bw HAMAD TAO ambaye ni mwenyekiti wa taasisi inayojihusisha na kujenga undugu kati ya dini ya CHRISTIAN AND MUSLIM BROTHER HOOD SOCIETY  ambapo katika mkutano na wanahabari mapema leo taasisi hiyo imesema kuwa kikundi cha uamsho hawana lengo nzuri na nchi ya Tanzania kuutokana na  matamko yake ambayo imekuwa ikiyatoa ya vitisho dhidi ya watu mbalimbali pamoja na dini nyingine ambapo amesema kikundi hicho kinasababiosha uhasama baina ya dini na dini.
          
       HAMAD TAO ambaye ni mwenyekiti wa taasisi hiyo amesema kuwa kikindi cha uamsho hakina tofauti na vikundi vingine vya kidaidi duniani huku akienda mbali na na kukifananisha na vikundi kama ALCAIDA,BOCO HARAM NA ALSHABABU.

         “sisi tumekuja hapa kwa upendo na kuipenda nchi yetu tunaiomba serikali ya Tanzania isiwafungie macho hawa watu wanaounda kikundi hiki kwani ni hatari kwa amani tuliyonayo”alisema TAO

         Aidha taasisi hiyo imesema kuwa tangu kuanzishwa kwa kikundi hicho matukio ya kigaidi Zanzibar kama kumwagiana tindikali,makanisa kuchomwa moto na ugaidi mwingine umekuwa ukiongezeka kwa kasi huku wakikwepa kuwahusisha uamsho moja kwa moja kuhusika na uhalifu huo,

MIGOGORO NDANI YA WIZARA YA MALI ASILI NA UTALII MCHUNGAJI MSIGWA AIBUKA,SOMA ALICHOZUNGUMZA NA MTANDAO HUU



    Na Karoli Vinsent

         SIKU moja kupita Baada ya Ikulu ya Rais Jakaya Kikwete kupuuza maoni ya Kamati ya bunge ya Ardhi,Maliasili na mazingira ,kwa kitendo chake cha kumrudisha ofisini, Mkurugenzi wa Wanyama Pori,Profesa Alexander Songorwa,

       Ambaye, aliyetimuliwa kazi na Waziri wa maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu miezi miwili iliyopita,kwa madai ya kushindwa kutekeleza Majukumu yake ipasavyo,

EXCLUSIVE INTERVIEW------TANESCO NA SONGAS SASA HAKUELEWEKI,SONGAS WATISHIA KUZIMA MITAMBO YAKE,TANESCO WAIBUKA WAJIBU-SOMA KISA KIZIMA



Na Karoli Vinsent
         
       SIKU chache Kupita Baada,Kampuni ya kufua umeme kwa njia ya Gesi,Songas limited kutishia kuzima mitambo yake,kutokana na ilichokiita.shirika la umeme Nchini(TANESCO) kushindwa kulipa deni linaofikia Dola za Kimarekani 72.8 milioni(karibu sh 116.4 bilioni za kitanzania).
         
      Naye,Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umeme Nchini(TANESCO) Eng Felchesmi J Mramba,ameibuka na kusema  Songas wamevunja makubaliano kwa kitendo chake ,cha kutumia vyombo vya Habari kudai deni hilo.
      

Thursday, May 1, 2014

MAGAZETI YA LEO IJUMAA MAY 02, 2014,YAPO HAPA KWA UNDANI WAKE


HUZUNIIIII.....MEI MOSI YAINGIA DOSARI, MFANYAKAZI WA IKULU AFIA UWANJANI JIONEE HAPA

 Baadhi ya jamaa aliyoambatana nao wakimwangalia mara baada ya kufikishwa chumba cha huduma ya kwanza.

MAADHIMISHO ya Siku ya Wafanyakazi Kitaifa, maarufu kama Mei Mosi yaliyofanyika leo jijini Dar es Salaam yameingia dosari baada ya mmoja wa wafanyakazi kufariki dunia uwanjani kwa ghafla akiwa katika maadhimisho hayo.

TAARIFA MUHIMU KWA MASHABIKI WOTE WA YANGA

Uongozi wa klabu ya Young Africans unapenda kuwajulisha wanachama wake, wapenzi wa soka na wadau kwa ujumla kuwa taarifa za kuhama kwa wachezai wake Didier Kavumbagu na Frank Domayo kwenda kujiunga na Azam FC zisiwakatishe tamaa, ni mapenzi ya wachezaj wenyewe kwani walishakubaliana na uongozi kila kitu juu ya kuendelea kuitumikia Yanga kabla ya siku mbili hizi kuonekana wakiwa wamejiunga na wana ramba ramba.

VIDEO LIVE---IKIWA LEO NI SIKU YA WAFANYA KAZI DUNIANI--KUMBUKA HOTUBA HII YA BABA WA TAIFA 1995 SIKU KAMA YA LEO

SHEREHE ZA MEI MOSI MWANZA ZAFANA

Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa wakipita ya mgeni wa heshima Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Eng.Evarist Welle Ndikilo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi mkoa wa Mwanza ,matembezi hayo yalihitimishwa kwenye uwanja wa CCM Kirumba.
Wafanyakazi wa Mkemia Mkuu wa Serikali wakiingia uwanjani CCM Kirumba Mwanza wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi mkoa wa Mwanza .
Wafanyakazi wa Idara ya Maliasili wakiingia uwanjani CCM Kirumba katika kuhitimisha siku ya wafanyakazi..
Mahakama ya Tanzania wakiingia uwanja wa CCM Kirumba huku wakitanguliza ujumbe mzito.
Kibanda cha Veta kilikuwa moja ya vibanda vilivyovutia kwenye maonyesho ya Siku ya Wafanyakazi zilizofanyika kwenye Uwanja wa CCM Kirumba mkoani Mwanza.
Wafanyakazi wa Hospitali ya Bugando wakielekea kuingia kwenye matembezi ya mshikamano katika kusheherekea siku ya Wafanyakazi kwenye Viwanja vya CCM Kirumba.
Wafanyakazi wa Halmashauri ya Jiji Mwanza wakipita ya mgeni wa heshima Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Eng.EvaristWelle Ndikilo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi mkoa wa Mwanza ,matembezi hayo yalihitimishwa kwenye uwanja wa CCM Kirumba.

MAADHIMISHO YA SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI YAFANYIKA ZANZIBAR

DSC_0025  
Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohd Shein kushoto anaepunga mkono akiyapokea maandamano ya Wafanyakazi wa Sekta mbalimbali katika Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (May Day) yaliofanyika Hoteli ya Bwawani Mjini Zanzibar.DSC_0033DSC_0034 Mashirika mbalimbali yakipita mbele ya Mgeni Rasmi hayupo pichani katika Maadhimisho ya siku ya Wafanyakazi Duniani (May Day) yaliofanyika Hoteli ya Bwawani Mjini Zanzibar.