Monday, May 30, 2016

KAULI YA KWANZA KUTOKA ACT WAZALENZO BAADA YA ZITTO NAYE KUSIMAMISHWA KUINGIA BUNGENI


Story kubwa iliyofunga siku kwa leo ni sakata la kusimisa kwa wabunge kadhaa wa upinzani kushiriki kwa shighuli za bunge kwa vipindi tofauti,Mbunge wa kungoma Mjini ZITTO KABWE ni miongoni mwa wabunge waliopo katika List hiyo ya wabunge saba ambao inasemekana chanzo ni kuchochea Vurugu Bungeni,Baada ya Zitto Kutajwa Chama anachokiongozi cha ACT WAZALENZO wametoa kauli yao ya kwanza Ambayo Nimeinukuu kutoka kwa Ado Shaibu
Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mawasiliano .nimekuwekea hapa
CHAMA Cha ACT Wazalendo kimesikitishwa na kitendo cha ugandamizaji wa demokrasia kilichofanywa na wabunge wa CCM kwa kuwasimamisha ubunge wabunge wa upinzani akiwemo kiongozi wa chama chetu ndg. Zitto Kabwe.

Katikati ya masikitiko hayo tunafarijika kuona wabunge hao wameondolewa kwa sababu ya misimamo yao ya kutetea maslahi ya wananchi
Tungesikitishwa zaidi kama mashujaa wetu hawa wangeondolewa bungeni kwa sababu ya ulevi au wawe sehemu ya wagonga mihuri ya masuala ya hovyo hovyo yanayosimamiwa na serikali ya chama cha Mapinduzi (CCM)
Kwa sababu hiyo ya kusimamia maslahi ya wananchi sisi kwetu ni mashujaa na kwa maana hiyo Chama chetu kinaandaa maandamano makubwa jijini Dar Es Salaam kuwapokea mashujaa wa wananchi

Show more reactions
Comment

No comments: