Wednesday, October 12, 2022

RAIS SAMIA MGENI RASMI KATIKA MJADALA WA KITAIFA WA NISHATI UTAKAOFANYIKA NOVEMBA 1-2, 2022 DAR ES SALAAM

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa Mgeni rasmi katika mjadala wa kitaifa wa utaokuja na suluhu ya namna watanzania watakavyohamasika na matumizi ya Nishati mbadala na kuachana na nishati isiyofaa. 

Mkutano huo utakaofanyika Novemba 1-2, 2022  katika Kituo cha cha Kimataifa cha Mikutano cha Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam utaratibiwa na Wizara ya Nishati.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Oktoba 12, 2022. Waziri wa Nishati Januari Makamba amesema kuwa mkutano huo utawakutanisha wadau mbalimbali kutoka sekta za Afya, Nishati, Mazingira, Jinsia, Usawa watunga sera pamoja na sheria mbalimbali ili kuweza kujadiliana namna gani wanaweza kupunguza au kuondoa kabisa matumizi ya nishati ya isiyo safi na salama. 

Amesema Sera ya Nishati ya 2015 inayosimamiwa na wizara ya nishati inaelekeza Wizara ya Nishati kuchukua hatua za kuwawezesha watanzania kupata nishati safi na salama na kwa gharama wanayoimudu ili kuboresha ustawi wa watanzania kwa kiasi kikubwa. 

Waziri makamba amesema kuwa Mjadala huo utaratibiwa na wizara ya Nishati ili kupata majibu ya kudumu ya kuondokana na matumizi ya nishati ya kupikia ya Mkaa na kuni nchini pamoja na kupata uelewa wa pamoja juu ya suala nishati ya kupika hapa nchini.

Amesema kuwa katika mkutano huo watangazi katika mlengo wa kiuchumi, Kijinsia afya Usawa na mazingira kwa namna ambavyo tunapika hapa nchini kwa kutumia Nishati safi na Salama. 

Waziri Makamba amesema mjadala huo utapelekea kutambua Changamoto za kutumia kuni na Mkaa, athari zilizipo na kuangalia matokeo yake ni nini. 

Amesema Mifumo ya Kisera Sheria, Kikodi, Kifedha na Utawala itawekwa kwaajili ya kupambana na hali ya namna tunavyopika na kuwaondoa watanzania kutumia nishati inaathiri Afya na Maisha. 

Akizungunzia kuhusiana na madhara yanayojitokeza katika jamii juu ya matumizi ya kuni, Mkaa na nishati nyingine zisizo safi na salama Waziri Makamba amesema Vituo vya afya Nchini vimeelemewa na mzigo Mkubwa wa utoaji huduma za afya za mfumo wa upumuaji zinazotokana na namna tunavyopika.

Amesema Watanzania zaidi ya elfu 33 wanafariki dunia kwa mwaka kutokana na kuvuta moshi wa namna tunavyopika chakula hivyo hii inaendelea kuathiri akina mama na watoto wa kike kwa  kupoteza muda mwingi kwenye kutafuta nishati ya kupikia ya kuni na Mkaa. 

Asilimia 70 ni magonjwa yasiyoambukiza ikiwemwo magonjwa ya mfumo wa upumuaji.

"Wanapokuwa wanatafuta nishati hiyo wanapunguza muda wa kutafuta elimu au kufanya shughuli nyingine za uzalishaji mali huko polini wanakutana na dhahama na matukio ya unyanyasaji wa kijisia.

Pia Nishati  isiyo safi na salama inaleta utofauti au kutokuwa na usawa kati ya wanawake na wanaume, watu wa mjini na vijijini wenye kipato na wasio na kipato." Amesema  Waziri Makamba

Kwa Upande wake Daktari Bingwa wa Magonjwa ya mfumo wa Upumuaji, kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili, Pauline Chale ameeleza kuwa Matumizi ya Nishati isiyo safi na salama  inasababisha changamoto nyingi hasa katika Afya na matibabu yake ni gharama kubwa 

Dkt. Pauline ameeleza kuwa mgonjwa wa Mfumo wa Upumuaji yanaondoa watu. Pia amesema matumi ya kuni, Mkaa na Mavi ya wanyama yanasumu zaidi ya 200 ndio maana watu wengi wanakuwa na macho mekundu kutokana na sumu hizinazopatikana kwenye moshi.

Wednesday, October 5, 2022

Kamati ya Kutafuta Mdundo wa Taifa yakamilisha kuchukua maoni Katika Mkoa wa Dar es salaam

Na Moshi Saidi Dsm.

Kamati ya Mdundo wa Kitaifa iliyoundwa hivi karibuni na Waziri Tamaduni Sanaa na Michezo  Mohamedi Mchengrwa imepokea maoni  Kutoka kwa Wadau mbalimbali wa muziki ikiwemo watayarishaji wa muziki,watunzi,watangazaji wa vyombo vya habari pamoja wasanii wa ngoma za asili lengo ni kupata vionjo vitakavyotumika kutengeneza Mdundo wa kitaifa.

Wajumbe wa Kamati ya kutafuta Mdundo wa Kitaifa wakiendelea kukusanya maoni.
Wakitoa maoni katika Mdahalo uliofanyika Jijini Dar es salaam Mkurugenzi kikundi cha muziki (Kay wa Mapacha) Levison Kasuhuwa alisema tangu nchi  imepata  uhuru haijawahi kuwa na mdundo wa kulitambulisha Taifa hivyo wasanii wa muziki wameiga Midundo ya za nje kutengeneza muziki yao hivyo sasa kwakuwa serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassani kupitia kamati iliyochaguliwa lazima ije na mdundo utakaokwenda kubadilisha taswira za watu kuondokana na kutumia Midundo isiyo ya asili yao   

"Tunakubali kuwa ukoloni umetuathiri kwa kipindi kirefu kwa kuacha Tamaduni zetu kuna usemi asiyependa kwao ni mtumwa hivyo tumechoka kuwa watumwa kutumia Midundo ya kigeni Sasa ni wakati wa kuwa na mdundo wetu wa asili ambao utatutambulisha "alisema Levision

Sixmondi Mneka kutoka  chama cha muziki wa Reggae dansi nchini amewasihi na kuwaomba Watanzania kuacha  ushabiki wa makabila na badala  yake kushirikiana Kwa pamoja kuunganisha vionjo vya  makabila mbalimbali ili kutengeneza mdundo wa Taifa utakaotambulisha asili ya mtanzsnia katika mataifa mbalimbali Duniani 

"Watanzania wanatabia ya kuibua jambo lakini hatufiki mwisho hivyo tufanye vitu Kwa Makubaliano ambapo naisihi kamati yenu(kamati ya Mdundo wa Taifa) kuendelea kuifanya kazi hiyo iwe endelevu kulingana na mahitaji ya muziki wetu kwasasa ili kuendelea kuulinda Utamaduni wa kitanzania kupitia Sanaa hiyo ya Burudani."amesema Mneka.
Meneja wa Sisi Tambala Bendi Bw. Kibiriti akitoa maoni yake mbele ya wajumbe wa Kamati ya kutafuta Mdundo wa Kitaifa. 
Nae Meneja wa Sisi Tambala Bendi Bw. Kibiriti Nanjuja ameshauri kuwa ngoma za asili za makabila mbalimbali zenye vionjo vya kuvutia ndizo zitumike katika kutengeneza mdundo wa Kitaifa ,nakwama Jamii isipuuzie ngoma za asili kwani ndio utambulisho halisi wa Utamaduni wa Mtanzania kupitia Sanaa hiyo .

Akizungumza na Waandishi wa habari mara baada ya mdahalo huo Makamu Mwenyekiti kamati ya Mdundo wa asili Tanzania Masoud Masoudi ambaye ni Manju Muziki amesema kwamba zoezi la kutengeneza mdundo wa Kitaifa unatokana na nia ya Rais Samia Suluhu Hassan ambaye amenuia kulinda Mila na Tamaduni za Mtanzania kwani zimekuwa zikisahaulika tangu Tanzania ipate uhuru..

" Tumekubali kwa maoni ya wadau ambao wanaonekana wanakubaliana na dhana nzima ya Mdundo wa Taifa,wamekubali kwamba mdundo wa Taifa ni Muhimu,hivyo kuelewa mdundo wa Taifa ni hatua Moja kubwa sana" Amesema Masoud ambaye pia ni Mtangazaji wa TBC 

Tuesday, September 20, 2022

Viongozi wa Siasa Wakumbushwa Kuacha Kuwagawa Wananchi Kwa Maslahi yao Binafsi.

Na Vicent Macha

Wito umetolewa kwa Wanasiasa nchini kuacha tabia ya kuwagawa wananchi nabadala yake waendeleze misingi ya Aamani,Umoja na Maendeleo iliyoachwa na Muasisi wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Wito huo umetolewa leo Dar es salaam na Jaji Mstaafu Joseph Sinde Warioba kwenye kikao cha kubadilishana Uzoefu na Ujuzi kilichoandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere nakuwakutanisha wadau mbalimbali ikiwemo viongozi wa vyama vya siasa,lengo likiwa  ni kujadili misingi iliyoachwa na viongozi wa Taifa tangu kupata uhuru mwaka 1961.

Amesema kuwa viongozi wa kitaifa walifanya imani kuwa wananchi wote ni sawa ,nakwamba baada ya kupata uhuru viongozi hao  hawakuona umuhimu wa nchi kuwa huru huku wananchi wakiwa hawako huru,hivyo walihakikisha wanasimamia misingi ya Amani,Umoja na Maendeleo ili kulifanya Taifa la Tanzaia kuwa na Umoja.

"Tusiwagawe wananchi,tuhakikishe tunalinda misingi ya amani,umoja na maendeleo iliyoachwa na Viongozi wetu wa kitaifa waliopambana hadi tukapata uhuru,hivyo tunapaswa kuwa na nchi huru yenye watanzania huru."amesema Jaji Warioba.

Awali Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Joseph Butiku amesema kwamba Hayati baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere enzi ya uhai wake amekuwa akisimamia misingi ya Amani,Umoja na Maendeleo hivyo viongozi wa vyama vya siasa hawana budi kushirikiana kwa pamoja kuondoa changamoto zinazowakwaza watanzania katika kuwaletea maendeleo.

Kwa upande wake kadhalika Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM ) Bara Christina Mndeme amewambia waandishi wa habari kuwa mdahalo huo ulioandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere umewasaidia kupata mawazo ya namna yakuendeleza  misingi ya amani,Umoja na Maendeleo iliyoachwa na Hayat baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
\
                                                                   Habari Picha.
Jaji Mstaafu Joseph Sinde Warioba akiongea na Baadhi ya Wajumbe kutoka vyama mbalimbali katika Kongamano liliandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere mapema leo Mkoani Dar es salaam.
Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Joseph Butiku akiongea katika Kongamano lililoandaliwa na Taasisi hiyo.
Baadhi ya Viongozi wa dini wakifuatilia matukio katika Kongamano lililoandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere mapema leo mkoani Dar es salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM ) Bara Christina Mndeme akiongea katika kongamano la kubadilishana uwezo kati ya Viongozi wa vyama mbalimbali vya Siasa na Asasi za Kijamii.
Kongamano likiendelea.




\



Friday, September 9, 2022

TALGWU yaiomba Serikali kufanya Mabadiliko Tozo Miamala ya Kibenki

Na Isaac Thadeo

CHAMA cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa Tanzania (TALGWU) kimeiomba Serikali kufanya mabadiliko katika sheria ya tozo za miamala ya kibenki ili kuepuka malipo ya mara mbili kwenye mshahara wa mtumishi wa umma. 
Mkuu wa Idara ya Habari na Uhusiano wa Kimataifa wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa Tanzania (TALGWU) Shani Kibwasali akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam.
Ombi hilo limetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Idara ya Habari na Uhusiano wa Kimataifa-TALGWU Shani Kibwasali akizungumza na waandishi wa habari kuhusu taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Chama kwa kipindi cha Januari hadi Juni 2022.

Shani amesema tozo hizo zinazidi kumbebesha mzigo na kumkandamiza mfanyakazi huku ikizingatiwa mishahara wanayopata haikidhi mahitaji ya kila Siku na familia zao. 

“Pia naomba nizungumzie suala la tozo za kibenki lililoanza kutekelezwa hivi karibuni. Tozo hizi zinawaathiri sana wanachama Wetu. Ikumbukwe kwamba watumishi wa umma kila mwezi wanalipa Kodi kwa kukatwa katika mishahara yao,” amesema Kibwasali na kuongeza kwamba,

“Lakini sasa kuanza kuanza kutekelezwa kwa tozo ya Serikali kwa miamala ya kutoa na kuhamisha fedha katika benki inamfanya mtumishi wa umma kutozwa zaidi ya mara mbili katika Pato moja kwa mwezi,”.

Kuhusu suala la nyongeza ya mishahara, amesema ni ukweli usiofichika kwamba wanachama wao ambao ni wahanga wakubwa kwani bado wanamanung’uniko na TALGWU kama msemaji wao hawajaridhika kabisa kwa jinsi nyongeza ya mshahara ilivyofanyika.

“Ila naomba niwatoe hofu wanachama wetu kwamba suala hili linashughulikiwa na Chama kwa kushirikiana na shirikisho la vyama huru vya Wafanyakazi nchini (TUCTA),” ameeleza Kibwasali.

Akizungumzia kuhusu mafanikio ya TALGWU kwa kipindi cha Januari hadi Juni mwaka huu, amesema kwamba hadi kufikia Juni 2022 walikuwa na jumla ya kesi 140 ambapo mawakili wa Chama wanasimamia kesi 100, mawakili wa nje wanasimamia kesi 13, na rufaa zilizopo Tume ya Utumishi wa Umma ni 27.

Kwamba Chama kiliandaa utetezi kwa watumishi 12 waliokuwa wamepewa mashataka na waajiri. Hivyo amesema kati ya kesi 140 walizonazo zilizoisha zilikuwa ni 39 na chama kimeshinda jumla ya kesi 35 na kushindwa kesi nne huku kesi nyingine zikiendelea Mahakamani.

Kibwasali amebainisha kuwa katika kipindi hicho pia TALGWU ilikuwa na jukumu jingine kubwa la kushughulikia haki na stahiki za wanachama ambazo kimsingi zipo kwa mujibu wa sheria ya Utumishi wa Umma na kanuni zake.

Hivyo amesema TALGWU inajivunia kuona Serikali imetekeleza maombi yao katika maeneo ya upandiahaji vyeo na mishahara, malipo ya malimbikizo ya mishahara na utawala Bora.

Friday, August 19, 2022

NSSF yajipanga kukusanya Trioni 7.3 katika Mwaka wa fedha 2022/2023

Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umepanga kukusanya kiasi Cha shilingi trioni 7.3 katika Mwaka wa fedha 2022 / 2023 Kutoka katika vyanzo vyake mbalimbali.

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Bw. Masha Mshomba akiongea na Waandishi wa habari mapema leo jijini Dar es salaam.

Kauli hiyo imetolewa leo Agosti, 19 jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa huo Bw. Masha Mshomba, alipokua akizungumza na waandishi wa habari, akitoa Taarifa ya Utendaji wa Mfuko pamoja na Vipaumbele vya Mfuko kwa mwaka wa Fedha  2022/23.

Amesema kuwa, ukuaji huo ni mkubwa tofauti na miaka miwili ya nyuma iliyopita ambapo thamani ya Mfuko ilikuwa ni Shilingi Trilioni 4.3 na kuwa ukuaji huo umechangiwa na ongezeko la makusanyo ya michango.

"Tumepata mafanikio makubwa katika suala zima la ukuaji wa Mfuko na hii imesababishwa na sababu kadhaa ikiwemo kuweka misingi imara na madhubuti ya ukusanyaji wa mapato" amesema Mshomba.

Ameongeza kuwa, katika mwaka wa fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2022, Mfuko ulikusanya zaidi ya Shilingi Trilioni 1.42 kwamba makusanyo hayo ni zaidi ya hata bajeti ambayo walijipangia iliyokuwa Shilingi Trilioni 1.38, ambapo pia Mfuko umeboreshaji sana udhibiti wa matumizi jambo ambalo limechangia ukuaji wa NSSF.

Amesema kuwa, mafanikio mengine yaliyopatikana, ni pamoja na uboreshaji wa huduma hasa kwa kutumia mifumo mbalimai ya TEHAMA ambapo sasa mwanachama na wadau wanaweza kupata huduma popote walipo bila ya kufika katika ofisi za NSSF kwa kutumia mifumo ya waajiri na wanachama yaani Employer Potal na Member Potal.

Mshomba alisema Mfuko pia unapata matokeo mazuri sana katika Uwekezaji hasa ukizingatia kuwa wanawekeza katika maeneo salama ambapo katika kipindi cha miaka miwili uwekezaji umeleta mapato makubwa.

"Ilikuwa haijafikiwa NSSF kuweza kupata mapato ya mwaka zaidi ya Shilingi bilioni 500 lakini katika mwaka huu wa fedha umepata zaidi ya Shilingi bilioni 600,matokeo haya ya uwekezaji yametokana na Mfuko kujikita zaidi katika uwekezaji kwenye maeneo ambayo yanaleta faida kwa Mfuko na kuhakikisha wanaudhibiti wa fedha"amesema Mshomba.

Hata hivyo, amesema chachu kubwa ya mafanikio ya NSSF imechagizwa na kasi ya utendaji wa Rais Samia Suluhu Hassan kwa sababu amekuwa chachu ya ongezeko kubwa la wawekezaji hapa nchini hususan katika sekta binafsi kutokana na kufungua fursa za uwekezaji.

Kuhusu waajiri kutowasilisha michango alisema wameweka mikakati mbalimbali kwa kushirikiana na taasisi nyingine za Serikali ili kupata orodha kamili ya waajiri ambao watawafikia na kufuatilia michango ya wanachama.

Mshomba aliwahamasisha Watanzania wote kushiriki katika zoezi zima la Sensa ya Watu na Makazi ifikapo tarehe 23 Agosti, 2022 ili waweze kuhesabiwa.

Thursday, August 18, 2022

Wiki ya AZAKI Kuzinduliwa leo Agost 18, 2022 jijini Dar es salaam

Na vicent Macha Dar es salaam.

Sekta binafsi zimetakiwa kushirikiana na Asasi za Kiraia (AZAKI,) Ili kusaidia kutatua changamoto zinazoikabili Jamii kwa kuwafikia wananchi kufahamu mahitaji yao na kuyapatia ufumbuzina kuleta maendeleo ya ya Taifa kwa ujumla.

Zoezi la Uzinduzi wa wiki ya Azaki likiendelea mapema leo jijini Dar es salaam.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Abdulmajid Nsekela wakati akifungua wiki ya AZAKI inayotarajiwa kufanyika kuanzia tarehe 24 hadi 28 Oktoba mwaka huu.

Aliyaongea hayo leo Agosti 18 jijini Dar es Salaam ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni “Maendeleo ya Watu, Habari Fanikiwa za Watu” na Maadhimisho ya mwaka huu yatafanyika jijini Arusha.

Aidha Nsekela amesema kuwa matokeo chanya yatapatikana kupitia wiki ya AZAKI na inaonekana dhahiri tangu kuanzishwa kwake mwaka 2018 licha ya changamoto lakini kumekua na kuongezeka kwa umoja na mshikamano miongoni mwa wadau.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Abdulmajid Nsekela.

‘’Suluhisho ya changamoto zinazoikumba jamii yetu inahitaji ushirikiano baina ya wadau ikiwemo mashirika, taasisi, sekta binafsi, Asasi za kiraia na Serikali kwa ujumla, ushirikiano na AZAKI na sekta binafsi ni hafifu tukishirikiana tutafika mbali zaidi katika kujenga uchumi wa jamii na Taifa kwa ujumla.’’ Amesema. Nsekela

Sanjari na hayo Mkurugenzi amesema, Ushirikiano baina ya AZAKI na sekta binafsi utasaidia kutatua changamoto kwa kiasi kikubwa kuwafikia wananchi wengi zaidi mjini na vijijini.

Nsekela amewasisitiza washiriki hao kuainisha njia mbalimbali mpya za kuwafikia wananchi na maendeleo kwa kuzingatia ushirikiano baina ya AZAKI hizo na sekta binafsi hasa katika uwekezaji utakayosaidia kuzalosha ajira

‘’Tujadili uwekezaji wa manufaa ya kiuchumi na kuwapa watanzania utulivu wa kiuchumi kwa kutoa wigo kwa ushirikiano baina ya sekta binafsi na AZAKI katika sekta mbalimbali ikiwemo elimu, afya na sekta nyingine za uwekezaji.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Foundation for Civil Society (FCS,) Bw. Francis Kiwanga amesema katika wiki hiyo ya AZAKI wanataraji matokeo chanya hasa katika kuimarisha ushirikiano baina ya Serikali, sekta binafsi na Asasi za kiraia katika ujenzi wa Taifa na ushiriki wa wananchi katika kuleta maendeleo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kituo cha Haki za Binadamu (LHRC,) Anna Henga amesema kusanyiko hilo la wana AZAKI tangu kuanza kwakwe 2018 limekuwa na malengo ya kufikia maendeleo endelevu pamoja na kubadili mtazamo wa wananchi na kutambua mchango wa Asasi za kiraia.

Hata hivyo amesema ni muhimu sekta binafsi kushiriki kikamilifu katika wiki hiyo muhimu hasa katika kupanua wigo wa kuwafikia wananchi, kutambua changamto za na kuzipatia suluhu na kuishukuru Benki ya CRDB kwa kuonesha ushirikiano tangu kuanzishwa kwa kusanyiko la Asasi za kiraia mwaka 2018.

Amesema, wiki ya AZAKI kwa mwaka 2022 itakuwa tofauti na licha ya kueleza mafanikio na maendeleo yaliyofikiwa wana AZAKI watatawanyika katika maeneo mbalimbali, kukutana na wananchi na kueleza huduma ambazo AZAKI zinatoa kwa wananchi.

Wednesday, August 17, 2022

Watanzania wahamasishwa kuchangamkia fursa ya Uwekezaji na

Na Vicent Macha, Dar es salaam

Kituo Cha Uwekezaji Tanzania ( TIC) imewaomba Watanzania ambao wana nia ya kufanya Uwekezaji katika sekta mbalimbali, wachangamkie  fursa hizo nasio kuwachia wawekezaji kutoka mataifa mengine  kuja kuwekeza hapa nchini.
Kaimu Mkurugenzi wa Kituo Cha Uwekezaji Tanzania ( TIC) Jonh Mnali.

Rai hiyo imetolewe na Kaimu Mkurugenzi wa Kituo hicho Jonh Mnali wakati akizungumza na  Waandishi wa habari Kuhusu Mafanikio ya TIC katika kipindi Cha Mwaka 2021/ 2022,ambapo amebainisha kuwa watananzani bado hawajitokezi kuwekeza katika fursa  mbalimbali za Uwekezaji zilizopo.

" Naomba kutoa wito kwa watanzania wajitokeze kuchangamkia fursa za Uwekezaji katika maeneo yao,waondokane na dhana ya kufikiria kwamba Uwekezaji unawahusu watu kutoka nje ya nchi pekee,bali watambue uwekezaji unawahusu wawekezaji wa ndani na nje ya nchi" amesisitiza Mnali

Amendelea kusema kuwa TIC imefanikisha Uwekezaji kwa kufanya maboresho ya kituo Cha utoaji wa huduma za mahali pamoja " One Stop Facilitation Centre ya TIC" nakwamba taasisi zipatazo 12 za  serikali kwa sasa zinatoa huduma katika kituo cha mahali pamoja ambapo taasisi hizo ni Wizara ya Kazi,Wizara ya Ardhi,Uhamiaji,NIDA,NEMC,TRA,BRELA,TBS,TMDA,OSHA, TANESCO pamoja na TIC wenyewe.

Amesema kuwa TIC inaendelea kuhamasisha uwekezaji wa ndani na nje kwa kushirikiana na ofisi za kibalozi na ofisi za wakuu wa Mikoa, ambapo TIC inaendelea kupokea wawekezaji wenye nia ya kuwekeza nchini,hatua hiyo ni kutokana na serikali  kuendelea kuboresha mazingira ya Uwekezaji na Ujenzi wa Miundombinu wezeshi kama vile barabara,reli,bandari,viwanja vya ndege na umeme.

" Katika kipindi cha kuanzia Juni 2021 hadi 2022 uhamasishaji uwekezaji wa nje umeendelea kufanyika kupitia makongamano ya uwekezaji yaliyofanyika Qatar,Doha na ushiriki wa TIC kwenye kongamano na maonesho haya yameleta matokeo chanya ambapo wawekezaji mbalimbali walifika nchini kukutana na wataalamu wa sekta ambazo wanahitaji zaidi kuwekeza" amesema Mnali.

Kaimu  Mkurugenzi Mtendaji huyo wa TIC ameongeza kuwa wawekezaji wa ndani wameendelea kutembelea kituo cha Uwekezaji kutafuta fursa ,huku TIC pia imeendelea kusaidia wawekezaji hao kuratibu uwasilishwaji wa miradi ya watanzania katika majukwa mbalimbali yanayohusu uwekezaj.

Hata hivyo amefafanua kwamba Serikali imechukua hatua mbalimbali kuhakikisha inarahisisha utoaji huduma kwa kuondoa urasmu ,kutumia teknolojia ya mawasiliano ,na kuweka vigezo vinavyotumika kutoa huduma Kama vile cheti cha uwekezaji ambacho kimefanya uboreshaji ya utendaji kazi wa ndani,mtirirko was nyaraka na mafaili,utoaji maamuzi wenye tija,pamoja na kuweka vigezo na viwango vya utoaji huduma kwa wawekezaji.
 
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TIC Jonh Mnali, amesema kipindi cha mwezi Juni 2021 hadi 2022 jumla ya miradi 274 imesajiliwa ikilinganishwa na miradi 234 iliyosajiliwa katika kipindi hicho Mwaka 2020/ 2021 ambayo ni sawa na ongezeko la asilimia 14.6 ,miradi iliyosajiliwa katika kipindi hicho inatarajiwa kuzalisha ajira 43,925 ukilinganisha na ajira 36,470 zilizoripotiwa kipindi hicho mwaka 2020/ 2021.

Tuesday, August 16, 2022

TRA Kukusanya Shilingi Trilioni 23.65, Mwaka wa fedha 2022/2023

 

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Richard Kayombo akizungumza na waandishi wa habari Leo kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo jijini Dar es Salaam kuhusu mkakati wa makusanyo ya Kodi mwaka 2022/23.

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Richard Kayombo, amesema mamlaka hiyo kwa Mwaka wa Fedha wa 2022/2023, inatarajia kukusanya Shilingi Trilioni 23.65, ikiwa ni sehemu ya bajeti kuu ya Serikali ya Shilingi Trilioni 41.48, ambapo kwa mwaka wa fedha uliopita wa 2021/2022, walikusanya kiasi cha shilingi Trilioni 22.99.

Bw. Kayombo amesema kufuatia ongezeko la makadirio ya makusanyo hayo, TRA inaendelea kutoa elimu ya ulipaji kodi kwa wafanyakazi na wafanyabiashara, ya kuhusu sheria mbalimbali za kodi, tozo na ada zilizofanyiwa marekebisho ili kuhakikisha wanakuwa na uelewa sawa na kurahisisha ukusanyaji na ulipaji kodi kwa hiari na kutimiza majukumu na malengo yaliyowekwa katika utekelezaji wa bajeti ya mwaka huu wa fedha.

Ameyasema hayo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam, kuhusu utekelezaji wa Bajeti ya Serikali ya mwaka wa fedha 2022/2023 ambapo amewataka watanzania kulipa kodi inavyostahili ili kujenga uchumi wa nchi.

*“Katika mwaka wa Fedha 2022/2023 tumeanza kwa kasi ya kuelimisha watumishi wetu na wafanyabiashara kote nchini juu ya mabadiliko mbalimbali ya sheria mbalimbali za kodi, tozo na ada zinazosimamiwa na TRA pamoja na taratibu za ukusanyaji na usimamiaji wa mapato ya Serikali.”* Amesema Bw. Kayombo.

Aidha amebainisha kuwa, marekebisho na mabadiliko ya sheria za kodi yamefanyika kwa lengo la kuongeza kasi ya kufufua uchumi na kuimarisha sekta za uzalishaji kwa ajili ya kuboresha maisha ya wananchi, ambapo miongoni mwa mabadiliko ni pamoja na sheria ya usimamizi wa kodi ambayo inamtaka kila mwananchi mwenye Namba ya Kitambulisho cha Taifa (NIDA) kupata Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN).

“Katika mabadiliko ya sheria ya usimamizi wa kodi, Sheria ya sasa inamtaka kila Mwananchi mwenye Namba ya Kitambulisho cha Taifa (NIDA) kusajiliwa na kupata Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN) ili kumwezesha katika shughuli zake za kila siku”.* Amesema Bw. Kayombo.

Amesema katika mwaka wa fedha uliopita wa 2021/2022, Mamlaka hiyo ilifanikiwa kutatua changamoto za walipakodi, kuweka mazingira mazuri ya kulipa kodi, kuongeza kasi ya kusajili walipakodi wapya, kuwekeza kwenye TEHAMA na kutoa elimu na kuhamasisha

Ripoti ya ya wafanyabishara wa Mipakani yazinduliwa leo jijini Dar es salaam.

Liberty sparks ni Shirika lisilo la Kiserikali, lilojikita katika elimu na tafiti, linalotekeleza mradi wa urahisi wa kufanya biashara nchini Tanzania ambao unafadhiliwa na taasisi ya Atlas Network”.

Mradi huu unategemea kuleta maboresho katika mazingira ya biashara kwa kutazama uboreshaji viashiria vya kiuchumi vinavyo tolewa na riport mbalimbali ikiwemo Ripoti ya Benki kuu ya dunia mwaka 2020. 

Mradi huu chini ya kampeni ya Ujirani mwema ,ambapo hapa tuna angaliautaratibu, muda na gharama katika utumaji na uingizaji wa bidhaa mipakani kwa kuzingatia muda,taratibu na gharama zilizowekwa kisheria.

Kama think tank, tumegundua sehemu ya biashara za mipakani kwa sasa Tanzania imekuwa haifanyi vizuri sana ukilinganisha na nchi nyingine zilizopo chini ya Jangwa la Sahara kama Mauritius, Rwanda, Kenya, Botswana, Burundi na nchi nyinginezo katika urahisi wa kufanya biashara.

Ingawa Tanzania ilipanda kwa ngazi tatu kwenye ripoti ya benki kuu ya dunia mwaka 2019 -2020 bado kuna huitaji mkubwa wa kuhakikisha tunafanya vizuri zaidi, hili litatusaidia kutangaza na kuvutia wawekezaji nchini na kuwezesha vijana wetu kujiajiri wanapomaliza vyuo vikuu.

Naibu waziri wa Uwekezaji, Biashara na Viwanda Exaud Kigahe akizungumza wakati wa uzinduzi wa ripoti ya Wafanyabisahara wa Mipakani Mapema leo jijini Dar es salaam.

Liberty sparks inatambua mchango mkubwa wa serikali wa kuboresha mazingira rahisi na rafiki ya ufanyaji biashara pamoja na kutambua mchango mkubwa wa wadau katika kuchochea maendeleo ya nchi,na kutoa nafasi ya kufanya tathmini ya vipaumbele vya sera kwa kulinganisha na nchi na chumi zilizofanikiwa duniani kwa kuwa na mazingira bora ya ufanyaji biashara za mipakani na ukuaji wa uchumi katika kupambana na umaskini.

Katika kampeni hii tumefanikiwa kufanya tafiti ilayofanywa na Daktari Sauti Magai kutoka (College of Business) chuo kikuu cha Dar es Salaam. Tafiti hii inalenga kuboresha biashara za mipaka kama nilivyosema awali kwa kuzingatia taratibu,muda na gharama.

Sasa ili kufikia malengo hayo, tumeita wadau kutoka sekta binafsi pamoja na serikali na kuunda kikosi kazi kilichotoa mapendekezo ya pamoja kwa kuzingatia utendaji na uwakilishwaji wa moja kwa moja. 

Ni mategemeo yetu kupitia ripoti hii iliyotolewa leo na mgeni rasmi kuwa Mh Exaud Kigahe yataumika katika kufanya maboresho ya kisera na kuweka mazingira bora na rafiki yaufanyaji biashara Tanzania.

Tunaamini kwamba kila mtanzania akipata nafasi na kuweza kufanya biashara kwa urahisi, tutaweza kabisa kupunguza tatizo la umasikini na ajira kwenye kaya zetu kwa sehemu kubwa.

Hili litasaidia kuchochea maendeleo ya jumla na kuondokana na utegemezi. Hatua hii ya kuwaleta serikali na sekta binafsi kwa pamoja itasaidia kutoa mapendekezo yenye mchango chanya kwenye mpango wa muda mrefu wa Tanzania (TDV 2025), Mpango wa maendeleo wa miaka mitano (2021/2022 - 2025/2026) na maendeleo endelevu ya Dunia 2030.

Wadau walioshiriki leo ni kutoka serikalini na sekta binafsi ni kama wafuatao; 

Ni matengemeo yetu Taasisi za kiserikali , waandishi wa habari, wabunge, wanazuoni na wadau wengieneo wa maendeleo watatuunga mkono katika kampeni hii ya kuboresha mazingira ya biashara Tanzania.

Matokeo ya mda mrefu na mfupi ya mradi huu ni kuona mazingira ya biashara yakichochea maendeleo ya nchi na watu kwa pamoja.

Baadhi ya Wajumbe wakufuatilia matukio yanayoendelea katika Uzinduzi wa ripoti ya Wafanyabiashara wa Mipakani.

Saturday, July 23, 2022

Waziri Ndalichako Atoa Maagizo kwa Mifuko ikiwemo NSSF na PSSSF Kuwalipa wastaafu mafao yao.

Na Muandishi wetu.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Ajira ,Vijana na Watu wenye Ulemavu Profesa Joyce Ndalichako ameagiza Mifuko ya mafao kwa wastaafu ikiwemo NSSF na PSSSF kuhakikisha wanawalipa Wastaafu wote wanaodaia  ikiwemo wanaodai kiinua mgongo,fidia,na Waliopunjwa.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Ajira ,Vijana na Watu wenye Ulemavu Profesa Joyce Ndalichako akizungumza na wazee waliyofika katika ukumbi wa NSSF Ilalal Boma jijini Dar es salaam.

Agizo hilo amelitoa leo Dar es salaam katika Mkutano aliouandaa Kwa ajili yakukutana na wastaafu wa Mkoa wa Dar es salaam kwa lengo ni kusikiliza malalamiko yao ,ambapo amedai kuwa tangu ameingia kwenye Wizara hiyo takribani miezi sita  amebaini wastaafu wengi wamestaafu  lakini bado hawajalipwa stahiki zao na wanaishi maisha magumu hivyo waje na vielelezo ili wafanyiwe mchakato wa kulipwa.

"Wastaafu hawa wanaodai madai yao wapo katika makundi tofautitofauti ikiwemo mapunjo ambapo mafao ya mtu yamekokotolewa kwa kutumia mshahara ambao ni mdogo kuliko mshahara halisi wa mfanyakazi alipostaafu na kusababisha mafao ya mkupuo anayopewa ni kidogo kuliko ilivyotakiwa"amesema Profesa Ndalichako.

Hata hivyo Waziri Ndalichako amesema kwamba amefuatilia na kubaini kuwepo kwa kesi za wastaafu ambazo  ziko wazi nakwamba suala lililopo  nikwenda tu kurekebishiwa mapunjo yao na kulipwa kwa kuzingatia mshahara wake wa mwisho ,nakusisitiza wastaafu  hao warudishiwe stahiki zao zote walizokuwa wanapunjwa.

Aidha amesema kwamba kuna baadhi ya Wastaafu vikokotoo vyao viko sawa lakini walikuwa hawana Elimu juu ya Vikokotoo hivyo,ambapo wamepatiwa Elimu na kujiridhisha kwamba hawajapunjwa mafao yao.
Zoezi la kuwasikiliza wazee likiendelea.

Kadhalika  Waziri Ndalichako amesema kumekuwa na makosa ya kiutendaji kutoka kwa baadhi ya watendaji wa mifuko ya pensheni kutokusikiliza malalamiko ya wastaafu wanaokuja kudai stahiki zao hivyo ameagiza watendaji hao kuacha tabia hiyo kwani wao ni watishi wa Umma.
 
Kwa upande wake Kassim Mafanya Mkazi wa Dar es salaam ambaye alikuwa Mtumishi  Chuo cha askari  Magereza Ukonga  amesema anashukuru kupata nafasi kusikilizwa kwani wastaafu wengi wamekuwa wanaishi kwa msongo wa mawazo na maisha yao hayaeleweki hawajui kesho yao  wamekuwa wakiahidiwa kupata nyongeza lakini hakuna kinachoendelea wengine wanafariki bila hata ya kufaidi chochote kutokana na jasho lao.

Naye Mtumishi Mstaafu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na watoto Chuki Kashaija mwenye ulemavu wa miguu  amesema alianza kazi tangu mwaka 1973 nakustaafu mwaka 2014,ambapo  amesema mpaka sasa hajapata mafao yake takribani miaka 8 sasa.

Wizara hiyo imepanga kufanya zoezi la kusikiliza malalamiko ya Wastaafu nchi nzima ikiwa ni Utekelezaji wa  agizo la rais Samia Suluhu Hassan aliloliagiza siku ya wafanyakazi Duniani( Mei mosi) iliyofanyika mwaka huu Jijini Dodoma.

Wednesday, July 20, 2022

Chuo kikuu cha Arusha chawashauri vijana kusoma kozi zitakazowawezesha kujiajiri.

Chuo Kikuu cha Arusha kinachomilikiwa na kanisa la Waadventista (Wasabato)kimewashauri wanafunzi wote wanaotarajia kujiunga na Elimu ya  juu kusoma huku wakitambua changamoto ya ukosefu wa ajira siyo ya Tanzania pekee bali ya dunia nzima hivyo wanapswa kupata maarifa ya kujiajiri kupitia fursa za masomo wanazozipata.

Mwenyekiti wa jimbo Kuu la Kusini mwa Tanzania Askofu Mark Malekana ambaye pia ni Mkuu wa Chuo Kikuu cha Arusha akizungumza na wanahabari kwenye banda la chuo hicho katika maonesho ya 17 ya Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU).
Hayo yamesemwa na Mkuu wa Chuo hicho ambaye pia ni Mwenyekiti wa jimbo Kuu la Kusini mwa Tanzania Askofu Mark Malekana wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye  Maonesho ya 17 ya Elimu ya Juu,Sayansi na Teknolojia yaliyoandaliwa Wizara ya Elimu Sayansi na teknolojia kupitia tume ya vyuo vikuu Tanzania (TCU) yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es  salaam. 

"Chuo chetu kina  falsafa yakipekee katika utoaji wa Elimu, tunamtayarisha Mwanafunzi  kiroho,kisaikolojia,kiuchumi na katika nyanja zote za maisha  kwa kufanya hivyo tunategemea mhitimu hata akikosa ajira atajiajiri mwenyewe bila kutegemea kuajiriwa"amesema Askofu Malekana.

Aidha amesema kwamba kupitia maonesho hayo wameamua kuzungumzia kwa kina na wazazi au walezi wanaofika kwenye Banda la chuo hicho kwenye viwanja vya Mnazi ili kuwashauri waweze kujiunga na masomo chuoni hapo wapate maarifa mazuri yatakayoweza kuwasaidia kujiajiri.
Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Chuo Kikuu cha Arusha Elisha Lomay ( wa kwanza kulia) akiwa na maafisa udahili wa chuo hicho katika Banda la Maonesho la chuo hicho .
Awali Mkuu wa Kitengo Cha Masoko wa Chuo hicho  Elisha Lomay  amewambia waandishi wa habari kwamba chuo hicho kinatumia falsafa ya kumjenga mwamanafunzi akue katika maadili ya kiroho ,Kimwili, pamoja na kitaaluma ambapo wahitimu wengi wamekuwa wakifanikiwa kufanya kazi Kwa weledi mkubwa.

Amendelea kufafanua kuwa  chuo hicho ambacho kipo Wilayani Meru Mkoani Arusha kimekua kikidahili wanafunzi bure kupitia njia ya mtandao,nakwamba baada ya wanafunzi kujiunga na chuo hicho wanalipia ada ambazo Wanaweza kuzimudu ambapo zinalipwa kwa awamu.

" Chuo chetu kinatoa ufadhili( Scholarship ) Kwa wanafunzi wanaotaka kusoma nje ya nchi kwa kushirikiana na wasabato wenzetu wanaoishi nje ya nchi ikiwemo Marekani,hivyo tunawakaribisha wazazi na walezi kuwaleta watoto wao kujiunga na chuo chetu kwani kina mazingira rafiki yakujisomea na gharama za ada na malazi ni nafuu" amesema Lomay.

Aidha amesema kwamba program wanazofundisha chuoni hapo ni pamoja na  Shahada za kidini,Utawala wa Biashara na Uhasibu,Sanaa ,Ualimu  pamoja na ngazi ya cheti na Astashahada ya Elimu ya Dini(Diploma) katika nyanja mbalbali.

Monday, July 18, 2022

Chuo Kikuu cha Katoliki Ruaha (RUCU) kimekuja na mambo haya mazuri katika maonyesho ya 17 ya Vyuo vikuu.

Mkurugenzi wa Kozi za Shahada na zisizokuwa za Shahada wa Chuo Kikuu cha Katoliki Ruaha( RUCU) Dkt Wille Migodela (wakatikati) akifuatilia maelekezo yanaoyotolewa na mmoja wa maafisa wa udahili wa Chuo hicho Kwa mwanafunzi aliyetembelea banda hilo kwenye maonyesho ya 17 ya Tume ya Vyuo Vikuu Nchini( TCU), yanayofanyika Viwanja vya  Mnazi Mmoja Jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi wa Kozi za Shahada na zisizokua za Shahada wa Chuo Kikuu cha Katoliki Ruaha( RUCU) Dkt Wille Migodela (wa kwanza kutoka kushoto) akitoa maelekezo kwa baadhi ya Wanafunzi waliotembelea banda la Chuo hicho kwenye maonesho ya 17 ya Tume ya Vyuo Vikuu Nchini (TCU) yanafofanyika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es salaam.

Chuo Kikuu cha Katoliki Ruaha (RUCU) katika kuhakikisha kinakabiliana na changamoto zinazoikabili Jamii kimejikita kutoa Elimu kwa wanafunzi Kwa kufanya ubunifu wa tafiti mbalimbali Kwa ajili ya kukabiliana na changamoto za kimazingira Kama vile Mbu wanaoambukiza Ugonjwa wa Malaria.

Magonjwa Mengine ni magonjwa ya ngozi( Fangasi) na Kikohozi,ambapo wanafunzi wanafanya tafiti kupitia mimea ya asili nakutengeneza dawa ambazo zinasaidia kukabiliana na magonjwa hayo.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Kozi za Shahada na zisizo za Shahada wa Chuo hicho Dakt Wille Migodela wakati akizungumza na Waandishi wa habari kwenye maonyesho ya 17 ya Elimu y juu Sayansi na Teknolojia yaliyoandaliwa na Tume ya Vyuo Vikuu Nchini ( TCU).

Aidha amesema kwamba chuo hicho kinatoa program za Kozi mbalimbali lakini Elimu ya utafiti wa Ubunifu imekua ikipewa kipaumbele ili kumsaidia mwanafunzi anaehitimu kuondokana na zana ya kutemea kuajiliwa na badala yake aweze kujiajiliwenyewe.

Hata hivyo amendelea kusema kwamba Wanafunzi hao wamefanikiwa kubuni kifaa kinachopima uzito wa mizigo inayobebwa na magari ambapo kifaa hicho kinafungwa kwenye gari na gari hiyo haitapita kwenye mzani Kwa ajili ya kupimwa, badala yake kifaa hicho kitaonyesha ukomo wa  uzito kamili unaohotajika kubebwa na gari hilo.

"Magari yanatumia muda mrefu kukaa kwenye foleni ya mzani kupima uzito wa mzigo,sisi kama RUCU tumekuja na suluhisho la kubuni kifaa Cha kisayansi kitakachoonyesha ukomo wa uzito wa mzigo unaotakiwa kupakiwa" amesema Dkt Migodela

Nakuongeza kuwa "kuhusu Faculty of Arts and Social  science ,tumetengeneza kifaa kinaitwa "Analogy wheel" kazi yake ni kupima umbali kwenye tambarare(horizontal distance) wakati wa kufanya Survey(upembuzi).
Kifaa kinafanya kazi mbadala wa Chain(mnyororo) ambao kwa mda mrefu umekuwa ukishindwa kutupa vipimo halisi kwasababu ya masikio(oval shape) yanayo uunganisha na pia chain inatumia mda mrefu kupima urefu ardhini.

Amesema kwamba Kwa mwaka huu wa masomo 2022/ 2023 wanatarajia kudahili  wanafunzi wapatao 1400 ambapo wanafunzi wa Cheti na Diploma ni 700 na wengine 700 ni Shahada(Digree),ambapo amesisitiza kwamba mazingira ya kujisomea Kwa wanafunzi ni mazuri.

Chuo kikuu SUZA kuja na Shahada ya Uzamivu kwenye Sayansi ya Teknolojia ya Habari(IT)

Mkuu wa Kitengo Cha Uhusiano na Masoko wa Chuo Kikuu cha Taifa Cha  Zanzibar( SUZA) Khadija Sadiq Mahumba ( mwenye kitambaa cheupe kichwani)akitoa maelekezo Kwa baadhi ya Wanafunzi waliotembelea Banda la chuo hicho kwenye maonyesho ya 17 ya Tume ya Vyuo Vikuu Nchini ( TCU) katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es salaam.
Baadhi ya watu waliotembelea Banda la Chuo kikuu cha Tifa Zanzibar SUZA wakisikiliza maelekezo kutoka kwa Maafisa Udhahili wa chuo hicho wenye Tshirt za rangi ya bluu.

Chuo Kikuu cha Taifa Cha Zanzibar(SUZA) kinaendelea kuunga mkono sekta ya elimu nchini Kwa kuanzisha kozi mpya ambazo ikiwemo ya  Shahada ya Uzamivu kwenye Sayansi ya Teknolojia ya Habari(IT) katika mwaka wa Masomo 2022/ 2023.

Ameyazungumza hayo Mkuu wa Kitengo Cha Uhusiano na Masoko wa SUZA Khadija Sadiq Mahumba wakati akizungumza na Waandishi wa habari kwenye Maonyesho ya 17 ya Elimu ya Juu,Sayansi na Teknolojia yaliyoandaliwa na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia kupitia Time ya Vyuo Vikuu Nchini( TCU) Mnazi mmoja jijini Dar es salaam.  

Aidha amesema kwamba chuo hicho kinatarajia kudahili wanafunzi wapatao 2000 Kwa programu mbalimbali zikiwemo za Elimu,Afya,Kilimo kwa ngazi mbalimbali ikiwemo  Cheti,Astashahada( Diploma) Shahada(Degree),Shahada ya Uzamili na Uzamivu.

Amesema kuwa kwa mwaka huu wa masomo chuo hicho pia kinatarajia kutoa programu ya Shahada ya Uzamivu( Phd) ya Lugha ya kiswahili ,na kwamba amewaomba wanafunzi wanaotaka kujiunga na SUZA wachangamkie fursa hizo.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Uhusiano na Masoko SUZA amesema kwamba Chuo hicho kinatoa programu za Kozi za Utalii ambapo wanafunzi watakaosoma kozi hizo watapata fursa ya kusoma lugha mbalimbali za kigeni ikiwemo lugha ya Kireno,Kichina ,Kifaransa,Kijerumani,na kwamba chuo hicho pia kinatarajia kuanza kufundisha Programu ya lugha ya Kikorea.

Hata hivyo amebainisha kuwa wakati wa udahili wa dirisha la pili wanatarajia kudahili wanafunzi kwa program mpya za Shahada ya Uzamili ya Benki na Fedha( MSc Benking & Finance) pamoja na Shahada ya Uzamili ya  Utawala wa Fedha na Biashara ( MBA-Finance).

" Ningependa kuwaomba wazazi wawalete wanafunzi  kwenye banda letu hapa Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam wajionee kozi tunazofundisha ili wafanye maamuzi sahihi yakujiunga na chuo chetu chenye fursa ya kupata ajira nje na ndani ya nchi" amesema Khadija.