Showing posts with label UZALENDO. Show all posts
Showing posts with label UZALENDO. Show all posts
Saturday, March 3, 2018
Thursday, February 15, 2018
Sunday, February 11, 2018
Meya Mwita aungana na wananchi wa jiji la Dar es Salaam kupima magonjwa ya Kisukari na Presha.
MSTAHIKI Meya wa Jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita leo ameungana na wakazi wa jijini hapa katika kongamano la kupima Magonjwa ya Kisukari na Presha lililoandaliwa na Lions Clubs International kwa kushirikiana na Kituo cha Afya cha Irania kilichopo jijini hapa.
![]() |
Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita akipata kipimo cha Presha kutoka kwa Dokta Mahmod Shahamati ambaye ni Mkurugenzi wa Kituo cha Afya cha Iranian kilichopo jijini hapa.
|
Katika kongamano hilo Meya Mwita amewapongeza waandaaji na kuwaeleza kuwa wasiishie hapo hivyo wafikishe huduma hiyo kwenye halmashauri nyingine za jiji la Dar es Salaam ili wananchi wote waweze kupata huduma hiyo.
Meya Mwita amesisitiza kuwa kuna umuhimu mkubwa wa kucheki afya zao hususani inapojitokeza fursa hizo kwa kuwa baada ya kupata majibu ya vipimo hivyo inawapa urahisi katika kupata matibabu.
Amesema Taasisi hizo zimekuwa na mchango mathubuti kwa wananchi kutokana na uzalendo mkubwa waliokuwa nao na hivyo kuwasihi wananchi kujitokeza kwa wingi kupata huduma hiyo.
![]() |
| Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita akijiandaa kupima Kisukari leo aliposhiriki kongamano la kupima Magonjwa ya Kisukari na Presha |
"Jambo hili ni muhimu sana, ninawapongeza, ombilangu kwenu, angalieni namna ya kuendelea kuwasaidia wananchi wengine katika jiji letu la Dar es Salaam, huduma hii ni ya muhimu sana na kila mwananchi anahitaji kuipata" amesema Meya Mwita.
Awali akimkaribisha Meya Mwita, Rais wa Lions Clubs Shaheen Alam amempongeza na kumueleza kuwa wamekuwa wakitoa huduma hiyo kwa kushirikiana na Kituo cha Afya cha Iranian kwa lengo la kuwasaidia wananchi kutambua afya zao.
Imetolewa leo Februali 11 na Christina Mwagala Afisa Habari Ofisi ya Meya wa Jiji.
Friday, February 9, 2018
BULYANHULU YAKABIDHI HUNDI YA SHILINGI MILIONI 75,649,524 KWA HALMASHAURI YA NYANG’HWALE
| Meneja Mkuu wa Migodi wa Bulyanhulu Benedict Busunzu akifurahia pamoja na wafanyakazi wa Bulyanhulu baada ya kukabidhi hundi kwa halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale. |
Akikabidhi mfano wa hundi hiyo mbele ya madiwani wa halmashauri hiyo Meneja wa Mgodi huo, Benedict Busunzu, alisema kawaida mgodi huo hutoa ushuru kwa Wilaya mbili ya Msalala na Nyangh’hwale kwa ajili ya miradi ya maendeleo.
Aidha alitaja
moja ya miradi mingine
ambayo mgodi huo
umesaidia Wilayani humo
ni pamoja na
mradi wa mkubwa
wa kusambaza maji kwa
wakazi 150,000 wilayani humo,
wenye gharama ya
Shilingi Bilioni 4.5 ambao
unatarajiwa kukamilika mwishoni
mwa mwaka huu.
Aidha kwa
upande wake Katibu tawala wa Mkoa wa Geita, Celestine Gesimba amewataka
madiwani na watendaji wa
halmashauri ya hiyo kuepuka
kutumia fedha zinazotolewa na wadau
mbali mbali kwa ajili ya
miradi ya maendeleo kwa kulipana
posho za vikao,
badala yake zote
zitumike katika miradi kwa
manufaa ya ustawi
wa wakazi wa Wilaya hiyo.
“Ninapenda kuwaonya viongozi
na watendaji ambao mpo hapa Nyangh’wale kuwa
tusitumie hizi fedha kwa
ajili ya kulipana posho
za vikao badala
yake zote zietumike
katika miradi ya
maendeleo kwa jinsi
mtakavyoainisha,”alisema Gesimba.
Aidha Mkurugenzi wa
Wilaya ya hiyo,
Carlos Gwamagobe, pamoja na kushukuru mgodi mgodi
huo kwa kuwapatia fedha
hizo alisema ushuru wa huduma ambayo walikuwa wakipata hapo awali umeshuka kwani kwa kiasi kikubwa kwani walikuwa wakipokea
milioni mia nne kwa miezi sita .
“Tuna imani
kuwa mgodi huu ukianza
shughuli zake kama
ilivyokuwa awali hata
ushuru wa huduma
utaongezeka kwani awali tulikuwa
tukipatiwa kiasi cha
Shilingi Milioni 225
lakini tangu kuibuka
kwa sakata la
Makinikia, ushuru nao
umepungua mara mbili
ya zile za
awali,”alisema Gwamagobe.
Wednesday, February 7, 2018
MCHUNGAJI MSIGWA AIBUKA NA HILI KWA WAZIRI KIGWANGALA
Mbunge wa Iringa Mjini kwa tiketi ya CHADEMA, Mhe. Peter Msigwa amefunguka na kumchana Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangala na kudai kuwa anafanya kazi kwa mizuka na mihemko na kuisumbua sekta ya Utalii na Maliasili nchini.

Msigwa amesema hayo wakatii alipokuwa akichangia bungeni taarifa ya Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii na Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji, mjini Dodoma na kudai kuwa Mawaziri vijana wamekuwa na mihemko.
"Niwashauri hawa Mawaziri vijana fursa 'opportunity is atrracted by talent, skills, perfomance and abillity. Show your talent and abillity,m people will love you'
"Hawa Mawaziri wa zamani hawa kwa mfano Lukuvi, Tizeba tunawaona wakijibu hoja wanajibu hoja siyo za kimihemko kiasi kwamba unaridhika hata Waziri akikujibu unapenda lakini Mawaziri vijana wengi mnaonekana mnayofanya katika Serikali hii kiasi kwamba Serikali ijayo muonekane hamna tija" kwa sababu mna mihemko sana"
Mbali na hilo Msigwa alikwenda mbali zaidi na kumnyooshea mkono Waziri wa Maliasili na Utalii na kudai amekuwa na maamuzi ya ajabu jambo ambalo linapelekea kiongozi huyo kuivuruga Wizara hiyo.
"Utalii huu umejengwa kwa muda mrefu sana na akitokea mtu mmoja anaamua kufanya tu kwa kutafuta umaarufu atauvuruga kwa muda mfupi sana
" Utalii kwenye pato la taifa unaingiza asilimia 20 na forex ni kubwa inatokana na utalii kwa hiyo hicho si kitu kimoja mtu anaweza kuamka leo anasema nimeharibu na hii diplomasia ya kiuchumi inategemea sana na kutabirika, wawezekaji huko nje wanataka kuona kunatabirika wao kufanya biashara zao.
"Haiwezekani huyu Waziri anatoa amri mpaka mapolisi wanamkataa anashindwa hata kuwasiliana na Waziri wake wa Mambo ya Ndani, huyu huyu Waziri anatoa amri anapingana na Waziri wa Ardhi, huyu huyu Waziri mmoja anapingana na Waziri wa Uvuvi hatuwezi kuwa na Mawaziri ambao wanakuwa na mizuka na kufanya kazi kwa mizuka wote kama tunalipenda taifa letu tufanye kazi kwa kupendana" alisisitiza Mchungaji Msigwa
Wednesday, January 31, 2018
NAPE AENDELEA KUICHACHAFYA SERIKALI
Mbunge Nape Nnauye leo Bungeni ameipa changamoto Serikali juu ya gharama za kuunganisha umeme na kuishauri kuendelea kuchaji elfu 27,000 hata baada ya mradi wa REA kupita ambapo wataanza kuchaji 177,000 kuunganisha umeme.

Nape Nnauye ametoa ushauri huo alipopata nafasi ya kuuliza swali la nyongeza Bungeni kwenda kwenye Wizara ya Nishati
"Kwanza niipongeze Serikali chini ya Wizara ya Nishati kwa kazi nzuri wanayofanya ya usambazaji mzuri wa umeme vijijini hasa REA awamu ya 3, kwa kuwa gharama za kuunganisha umeme wakati mradi unaendelea ni elfu 27,000 na mradi ukipita ni 177,000 na kwa kuwa idadi kubwa na nzuri ya watumiaji wa umeme ni biashara nzuri kwa TANESCO kwanini bei hii isiwe moja ya elfu 27" alisema Nape Nnauye
Hata hivyo Nape Nnauye aliendelea kusisitiza kuwa kama jambo hilo halitawezekana basi REA waendelee na uwekaji wa nguzo na miundombinu na TANESCO wafanye kazi moja ya kupeleka umeme na kukusanya kodi baada ya kupeleka umeme.
Naibu Waziri Wizara ya Nishati alijibu hoja hiyo na kudai kuwa amepokea ushauri huo wa Mbunge wa Mtama na kuwa atapeleka katika ngazi zingine na kuona Serikali nini itafanya
"Wazo alilosema Kaka yangu Nape Nnauye linapokelewa na litafanyiwa kazi kwani ni la msingi kwa sababu Wizara yetu na shirika letu la TANESCO na wadau wengine wa nishati tunauza bidhaa hii hivyo ni vema tunapouza tupate wateja wengi ili tupate mapato na kuendesha shughuli mbalimbali na uwekezaji mpya wa maeneoya nishati"
Sunday, January 28, 2018
DKT. SHENI "SIWEZI KUONGEZA MUDA WA UTAWALA, MUDA WANGU UKIISHA NTAONDOKA MAPEMA TU".
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohammed Shein amesema hayupo tayari kuongeza muda wa uongozi kutoka miaka mitano hadi saba kwani kufanya hivyo ni kukiuka katiba ya Zanzibar.

Dkt Shein amesisitiza kwamba, aliapa kuilinda katiba ya Zanzibar hivyo hawezi kubadilisha muda wa uongozi na hakuna mtu atakayemfanya abadilishe au amvutie yeye kuendelea kukaa madarakani.
Rais Dkt Shein ameyasema hayo jana katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume visiwani Zanzibar alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mara baaada ya kurejea kutoka kwenye ziara ya wiki moja katika nchi za Falme za Kiarabu (UAE) alipokua ameambatana na mke wake, Mama Mwanamwema Shein.
“Mimi naheshimu katiba ya Zanzibar, na nina heshimu sheria za Zanzibar. Muda wangu ukifika nitaondoka haraka sana. Hakuna atakayenilazimisha mimi nikae, au atakayenivutia mimi nikae”alisema Rais Dkt Shein.
Aidha, Dkt Shein amesema kuwa, alisikia wawakilishi katika Baraza la Wawakilishi wakizungumza hilo, lakini hawazuiwi kujadili kwani wanafanya hivyo kwa mujibu wa sheria, lakini yeye hayuko tayari kuongeza muda.
“Hilo walizungumza wawakilishi barazani, wana haki ya kuzungumza, kwa mujibu wa taratibu zao na sheria zao na yeyote mwingine anaweza kuzungumza. Mimi nilisikia wakati wananzungumza, Mwakilishi mmoja akasema kwamba kuna baadhi ya nchi duniani zina miaka mitano nyingine saba, sasa kwanini na sisi tusiwe na miaka saba!”
Rais Dkt Shein amesema kuwa, suala la miaka saba labda linaweza kuwepo baada ya yeye kutoka lakini hadhani kama kuna jambo kama hilo.
“Mie sijalisema, sitolisema, na hakuna atayanilazimisha niliseme”alihitimisha Rais Dkt Shein, huku akitilia mkazo kwamba, muda wake ukiisha atamchukua mkewe na kumwambia waondoke
Friday, January 26, 2018
ZIMAMOTO NCHINI YAPATA TUZO YA UTENDAJI BORA YA MWAKA 2017
Thursday, November 9, 2017
UMOJA WA VIJANA WALIOSOMA NCHINI CHINA (CAAT) WATEMBELEA HIFADHI YA SELOUS KATIKA KUUTANGAZA UTALII WA NDANI KWA NJIA YA RELI YA TAZARA
Umoja wa Vijana waliosoma nchini China (CAAT) wametembelea katika hifadhi ya ya Taifa ya Selous ili kutangaza utalii wa ndani kwa njia ya treni ya TAZARA.
Akizungumza mwenyekiti wa umoja huo, Dkt. Liggyla Vumilia alisema kuwa wameamua kuandaa kampeni ya kutangaza utalii wa ndani kwa njia ya treni ya TAZARA hasa wa mikoa ya kusini mwa Tanzania ambao umekuwa ukisahaulika. Kampeni hiyo imeandaliwa na Umoja wa Vijana waliosoma nchini China (China Alumni Association of Tanzania -CAAT) kwa kushirikiana na Bodi ya Utalii Tanzania - (TTB) na TAZARA. PICHA ZOTE NA KAJUNASON/MMG - SELOUS-MATAMBWE, MOROGORO.
Mahojiano yakiendelea ndani ya treni.
Moja ya pango ambao treni inapita.
Reli ya TAZARA imenyooka.
Wakipata chakula cha usiku.
Nami mmiliki wa Kajunason Blog, Cathbert Kajuna (kulia) niliweza kuwakilisha vyema na wana-CAAT. Pembeni yangu ni Chris na Yusuph.
Wazee wa kazi Kaijage (mbele) akiwa na Dr. Heri.
Wana-CAAT wakipata kifungua kinywa.
Wana-CAAT wakiwa tayari kuingia mbugani kujionea vivutio mbali mbali.
Wana-CAAT wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuanza safari ya kuingia mbugani.
Moja ya wanyama wanapatikana hifadhi ya Selous.
Eneo la Matambwe gate.
Furaha baada ya kufika eneo la geti kuu.
Mhifadhi wa Wanyama Pori wa Selous kanda ya Matambwe, Gregory Kalokole akitoa maelezo machache juu ya hifadhi ya Selous. PORI la akiba la Selous ni moja kati ya hifadhi zenye utajiri wa vivutio adimu vya utalii na ambavyo vinapaswa kutangazwa zaidi kwa ajili ya watalii wa ndani na wa nje. Selous ni pori la akiba lenye ukubwa wa kilometa za mraba 54,000 likijumuisha maeneo ya ardhi oevu, misitu ya miombo, tambarare, nyasi za kuvutia, maziwa na mito inayotiririka, vyote vikifanya vivutio vya aina yake mbali na wanyama wa aina mbalimbali. Pori hili la akiba la Selous lilianzishwa mwaka 1896 na Wajerumani likiwa ni pori la kwanza kutengwa kwa ajili ya uhifadhi wa wanyamapori katika Bara la Afrika na la pili duniani kwa ukubwa baada ya hifadhi ya pori la Marekani ambalo linaitwa Yellowstone. Poro hili limegawanyika katika kanda 8 kiutawala. Umaarufu wa Selous si katika wanyama pekee ambao ndiyo kivutio kikubwa cha utalii wa uwindaji, utafiti umebaini kuwa katika eneo la Selous kuna utajiri mkubwa wa maliasili ya mimea ambayo ikitambuliwa na kutangazwa inaweza kuwa kivutio adimu na cha kipekee cha kitalii.
Wakisoma ramani mbali mbali inayoonyesha hifadhi hiyo.
Moja ya ramani.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana waliosoma nchini China (CAAT), Dkt. Liggyla Vumilia akizungumza machache na Mhifadhi wa Wanyama Pori wa Selous kanda ya Matambwe, Gregory Kalokole.
Moja ya wanyama wanaopatikana katika hifadhi ya Selous.
Umoja wa Vijana waliosoma nchini China (CAAT) wakifurahia ndani ya treni ya TAZARA wakati wakielekea ndani ya hifadhi ya Selous.

Ilikuwa ni furaha kila kona.
Mahojiano yakiendelea ndani ya treni.
Moja ya pango ambao treni inapita.
Reli ya TAZARA imenyooka.
Umoja wa Vijana waliosoma nchini China (CAAT) wakifurahia ndani ya treni ya TAZARA wakati wakielekea ndani ya hifadhi ya Selous.

Makaribisho ndani ya hoteli iliyopo nje kidogo ya hifadhi ya Selous eneo la Kisaki.
Wakipata chakula cha usiku.
Nami mmiliki wa Kajunason Blog, Cathbert Kajuna (kulia) niliweza kuwakilisha vyema na wana-CAAT. Pembeni yangu ni Chris na Yusuph.
Wazee wa kazi Kaijage (mbele) akiwa na Dr. Heri.
Wana-CAAT wakipata kifungua kinywa.
Wana-CAAT wakiwa tayari kuingia mbugani kujionea vivutio mbali mbali.
Moja ya wanyama wanapatikana hifadhi ya Selous.
Eneo la Matambwe gate.
Furaha baada ya kufika eneo la geti kuu.
Mhifadhi wa Wanyama Pori wa Selous kanda ya Matambwe, Gregory Kalokole akitoa maelezo machache juu ya hifadhi ya Selous. PORI la akiba la Selous ni moja kati ya hifadhi zenye utajiri wa vivutio adimu vya utalii na ambavyo vinapaswa kutangazwa zaidi kwa ajili ya watalii wa ndani na wa nje. Selous ni pori la akiba lenye ukubwa wa kilometa za mraba 54,000 likijumuisha maeneo ya ardhi oevu, misitu ya miombo, tambarare, nyasi za kuvutia, maziwa na mito inayotiririka, vyote vikifanya vivutio vya aina yake mbali na wanyama wa aina mbalimbali. Pori hili la akiba la Selous lilianzishwa mwaka 1896 na Wajerumani likiwa ni pori la kwanza kutengwa kwa ajili ya uhifadhi wa wanyamapori katika Bara la Afrika na la pili duniani kwa ukubwa baada ya hifadhi ya pori la Marekani ambalo linaitwa Yellowstone. Poro hili limegawanyika katika kanda 8 kiutawala. Umaarufu wa Selous si katika wanyama pekee ambao ndiyo kivutio kikubwa cha utalii wa uwindaji, utafiti umebaini kuwa katika eneo la Selous kuna utajiri mkubwa wa maliasili ya mimea ambayo ikitambuliwa na kutangazwa inaweza kuwa kivutio adimu na cha kipekee cha kitalii.
Wakisoma ramani mbali mbali inayoonyesha hifadhi hiyo.
Moja ya ramani.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana waliosoma nchini China (CAAT), Dkt. Liggyla Vumilia akizungumza machache na Mhifadhi wa Wanyama Pori wa Selous kanda ya Matambwe, Gregory Kalokole.
Moja ya wanyama wanaopatikana katika hifadhi ya Selous.
Subscribe to:
Posts (Atom)



