Friday, February 28, 2014

HABARI ZOOOTEE ZA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI ZIKO HAPA,UDAKU,MICHEZO NA HABARI MAKINI

.
.

TAARIFA MUHIMU KUTOKA AZAM TV JUU YA KUONYESHA MECHI YA YANGA LEO



1377169_224621101037472_893234737_nTumepokea maswali na simu nyingi sana zikiuliza kama Azam TV itaonesha mechi kati ya Yanga na Al Ahal leo, jibu ni kwamba HAPANA...           Ukweli ni kwamba tulipokea maombi toka kwa agent aliyenunua pambano kwa niaba ya Watu wa Misri ambaye aliomba Azam TV impe gharama za kuzalisha ili kuweza kupeleka feed yenye ubora wa kimataifa North Africa & Middle East na ikiwezekana kuonesha nchini Tanzania. Katika vikao vyote na Agent Azam TV iliweka wazi kuwa ipo tayari kuzalisha bure na hata kama ikibidi kuonesha delayed sawa kwa kuwa Yanga walionesha wazi kuzuia Live Coverage nchinikwa kuhofia mapato kupungua.
 
      Bahati mbaya Yanga waliikataa Azam TV na kuamua kutoa pesa waliyolipwa kukilipa kituo kimoja nchini ambacho ndicho kilichopewa kandarasi kwa malipo licha ya kutokidhi vigezo vya watu wa Egypt ambao walitaka angala 8 Camera OB na Azam TV iliwapa 10 Camera OB with HD Feed
 
         Kwa taarifa hii tungependa kuwaarifu wateja wetu kuwa Azam TV ilikuwa tayari kuwapa Yanga na Agent ushirikiano wote ili pesa yote waliyopewa na Watu wa Misri iingie klabuni lakini wao wameamua kuitumia kulipia production iliyo sub-standard ili mradi tuu kuinyima fursa Azam TV
 
       Pamoja na haya yote Azam TV inaitakia kila la kheri klabu ya Yanga kwenye mchezo wake wa leo, na inaamini matatizo hayapo kati ya Azam na Yanga kama taasisi bali mtu mmoja mwenye nguvu ndani ya Yanga

JAMANI JAMANI MTOTO HUYU ANAITAJI MSAADA WENU WATANZANIA,INATISHA SANA,ONYESHA UPENDO KWA KUMSAIDIA.samahani kwa picha ila ndo ukweli

Mtoto Adolotea Njavike (1.4) ambaye kichwa na kiwiliwili vimeungana baada ya kupata ajali ya moto akiwa na mama yake mzazi.

UGONJWA WA MIGOMO WAANZA TENA TANZANIA--WAFANYAKAZI WA TRL LEO WATANGAZA MGOMO USIO NA KIKOMO,SOMA WANACHOKIDAI

WAFANYAKAZI WAKIFUATILIA KWA MAKINI MKUTANO HUO, WOTE KWA UMMOJA WAO WAMEAZIMIA KUTOFANYA  KAZI MPAKA FEDHA YAO YA MWEZI WA KWANZA MPAKA WA TATU ILIPWE TENA KATIKA ONGEZEKO WALILOAHIDIWA KATIKA VIKAO MBALIMBALI.

 WAFANYAKAZI WA SHIRIKA LA RELI HAPA NCHINI MAPEMA HII LEO WAMEWEKA VIFAA VYAO VYA KAZI CHINI NA KUISHINIKIZA UONGOZI WA SHIRIKA HILO KUWALIPA STAHILI ZAO KAMA ILIVYOKUBALIWA NA WAZIRI MKUU,

KAMPENI ZA KALENGA NA MIZENGWE YAKE,DIWANI WA CCM AKUTWA NA BANGO LA CHADEMA

Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Tanangozi, ikiwa ni sehemu ya kampeni za chama hicho za uchaguzi mdogo wa jimbo la Kalenga

Moja ya mabasi yaliyokuwa yakisomba wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi, kutika sehemu mbalimbali likiwa njiani kueleka wafuasi hao katika mkutano wa ufunguzi wa kampeni za chama hicho, katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Kalenga mkoani Iringa uliofanyika jana.

updates----PICHA MBILI ZAIDI ZA AJALI ILIYOTOKEA LEO HUKO MANYONI YA GARI KUGONGA TRENI



SERIKALI YATANGAZA AJIRA ZA WALIMU 36,071



KATIKA kukabiliana na uhaba wa walimu nchini serikali imetangaza kuajiri walimu wapya 36,071 ambapo watapangiwa vituo vya kazi mwezi ujao.
Hatua hiyo ni mikakati ya serikali katika kukabiliana na uhaba wa walimu ambapo sasa watakuwa na upungufu wa walimu 21684 kutoka 57755 iliyokuwepo kabla ya kutanga ajira hizo mpya.
Naibu waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI anayeshughulikia Elimu, Kassim Majaliwa, alisema jana kuwa walimu hao watasambazwa katika shule za msingi na sekondari nchini.
Alisema taratibu zote za ajira kwa walimu hao wapya zimekamilika na kwamba mwezi ujao wote walioajiriwa watakuwa wamepangiwa vituo vyao vya kazi.

HABARI INAYOTIKISA TANZANIA MUDA HUU---BASI LIMEGONGA TRENI.WANNE WAFARIKI

        Habari Mbaya Zilizotufikia Hivi Punde,Basi la Bunda lagonga Treni na Kusababisha Vifo 

YANAYOENDELEA DAR ES SALAAM MUDA HUU

BAADHI  YA WAANDISHI WA HABARI PAMOJA NA WATU MBALIMBALI KUTOKA MASHIRIKA MBALIMBALI WAKIWA KATIKA WARSHA HIYO AMBAYO INAENDELEA HAPA JIJINI DAR ES SALAAM KATIKA OFISI ZA TAMWA ILIYOANDALIWA NA SHIRIKA LA USULUHISHI LILILOPO CHINI YA TAMWA  HUKU MAFDA KUU IKIWA NI MASHARA YA POMBE NA JINSI INAVYOSABABISHA UKATILI WA KIJINSIA KATIKA FAMILIA

Thursday, February 27, 2014

VITA YA KISIASA SASA IPO JIMBO LA KALENGA--CCM YAFANYA KUFURU KWENYE KAMPENI,MWIGURU NCHEMBA ATUA,AZINDUA KAMPENI SASA NI MWENDO WA SEMA NIKUSEME


Mgombea Ubunge wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Godfrey William Mgimwa akibebwa Juu na Wanachama/wapenzi wa CCM mara baada ya Kuwasili Viwanja Vya Stendi-kata ya Ifunda.
Mapokezi Mazito yakiendelea ya Naibu Katibu Mkuu CCM-Bara na Kijana Mgombea Ubunge Jimbo la Kalenga Ndugu Godfrey William Mgimwa kwenye uwanja wa Stedi-Kata ya Ifakara hii leo wakati wa Mkutano wa Ufunguzi wa Kampeni za Ubunge Jimbo la Kalenga. 

LEO MCHANA HAPA KALENGA PALIKUWA HAPATOSHI,CHEKI PICHA ZA KAMPENI ZA CHADEMA HAPA

KAZI NA MUZIKI

TFF, POULSEN WAKUBALIANA KUVUNJA MKATABA


tff

        Uamuzi huo umetangazwa leo (Februari 27 mwaka huu) jijini Dar es Salaam kwa pamoja na Rais wa TFF, Jamal Malinzi na Kocha Poulsen mbele ya waandishi wa habari.

         Rais Malinzi kwa niaba ya TFF ametoa shukrani za dhati kwa Kocha Poulsen kwa ushirikiano na mchango ambao ameutoa kwa Tanzania kuanzia kwenye mpira wa miguu wa vijana.

         Naye Kim amewashukuru Watanzania kwa ushirikiano waliompatia kwa kipindi cha miaka mitatu alichokaa nchini kuanzia Mei 2011 alipoteuliwa kuwa kocha wa timu za Taifa za vijana, na baadaye Taifa Stars.

         Akizungumzia benchi jipya la ufundi la Taifa Stars, Rais Malinzi amesema linatarajiwa kutangazwa hivi karibuni likiongozwa na kocha kutoka nje ya Tanzania.

BREAKING NEWZZ---- CHEKI DK SLAA NA MGOMBEA WA UBUNGE KALENGA WANAVYOENDELEA KUFUNIKA




MAPIGANO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI KITETO,LHRC YAJA NA TAMKO KALI,SOMA HAPA,BAADHI YA VIONGOZI WAHUSISHWA

WAKILI EMELDA URIO AKIZUNGUMZA NA WANAHABARI MUDA MCHACHE ULIOPITA HAPA JIJINI DAR ES SALAAM

Kituo cha sheria na haki za binadamu nchini tanzania leo kimeitaka serikali kuwachukulia hatua kali za kinidhamu  mkuu wa mkoa wa manyara,mkuu wa wilaya ya kiteto pamoja na mkurugunzi wa wilaya ya kiteto baada ya kugundua kuwa wao ndio chanzo kikubwa cha mgogoro wa wakulima na wafugaji uliotokea mapema mwaka huu na kugharimu maisha ya watu.

      Akizungumza na wanahabari jijini dar es salaam wakati akitoa tamko la kituo hiko kuhusu mgogoro huo wakili EMELDA URIO amesema kuwa kituo hiko kimegundua kuwa viongozi hao ndio chanzo kikubwa cha mgogoro huo baada ya kuruhusu ukusanyaji wa fedha usio wa halali kutoka kwa wafugaji ili kulipia gharama za dalali wa kuwaondoa wakulima katika eneo lenye mgogoro jambo ambalo amesema kuwa lilizua taharuki kubwa na baadae mapigano makubwa sana
         Aidha amezitaja sababu nyingine zilizochangia mgogoro huo kuwa ni mfumo mbovu wa matumizi ya ardhi ya kijiji kwani wale ambao wanaonekana ni wavamizi walipata ardhi maeneo hayo kutoka kwa viongozi wa kijiji kwa kutoa kiasi fulani cha fedha.

       Katika hatua nyingine kituo cha sheria na haki za binadamu kimelitaka jeshi la polisi kuhakikisha kinafwatilia kwa makini mgogoro huo na kuhakikisha kuwa linawachukulia hatua kali za kisheria wale wote wanaotajwa kuhusika katika mgogoro huo.


BAADHI YA MADHARA MAKUBWA YALIYOJITOKEZA KATIKA MGOGORO HUO

Wednesday, February 26, 2014

REPORT MAALUM---INASIKITISHA SANA MAISHA YA BIBI AZIZA WA KIJIJI CHA MIJONGENI TANGU NYUMBA YAKE IZOLEWE NA MAFURIKO SASA AMEHAMIA CHOONI,MAISHA YAKE YOTE NI CHOONI.ENYI WATANZANIA TUNSAIDIENI HUYU


Ijumaa ya February 22 majira ya 7 kasoro dakika kadhaa nawasili kijiji cha Mijongweni wilayani Hai.
Safari yangu hii ni kutizama maenedeleo ya Bib Aziza Mohamed aliyekuwa akiishi chooni baada ya nyumba yake kuezuliwa na mvua yenye upepo mkali ghafla milangoni nakutana na kufuri.
Hata pale nilipomwacha siku ya kwanza kufika ,Chooni ambako bibi huyo alihamishia makazi yake pia kulikuwa na kufuri.

MEYA A DAR ES SALAAM AONYESHA WASIWASI WAKE JUU YA RASIMU YA PILI YA KATIBA

MEYA MASABUR ..

  Mwenyekiti wa jumuia ya serikali za mitaa nchi Didas Masaburi amelalamikia kitendo cha kutojumuishwa kipengele kinacho husiana na serikali za mitaa katika katika rasimu ya katiba mpya inayotarajiwa kujadiliwa hivi karibuni bungeni mjini Dodoma.

TAARIFA MUHIMU KUTOKA TFF KUHUSU MECHI YA TWIGA STARS NA ZAMBIA.SOMA


 tff


         



    Timu ya Taifa ya Zambia (Shepolopolo) inatua nchini kesho mchana (Februari 27 mwaka huu) kwa ajili ya mechi ya marudiano ya michuano ya Afrika kwa Wanawake (AWC) dhidi ya Tanzania (Twiga Stars) itakayochezwa keshokutwa (Februari 28 mwaka huu).

          Shepolopolo yenye msafara wa watu 29 itawasili kwa ndege ya Fastjet ikitokea Lusaka na itafikia kwenye hoteli ya Accomondia kwa ajili ya mechi hiyo itakayochezwa Uwanja wa Azam Complex ulioko Chamazi kuanzia saa 10 kamili jioni.
    
   Waamuzi wa mechi hiyo kutoka Burundi wakiongozwa na Ines Niyosaba wamewasili nchini leo asubuhi wakati Kamishna Fran Hilton-Smith kutoka Afrika Kusini atawasili kesho (Februari 27 mwaka huu) saa 8 kamili mchana kwa ndege ya South African Airways.


BREAKING NEWZ---KINACHOENDELEA MLIMANI CITY MUDA HUU---UZINDUZI WA KAMPENI YA TAIFA YA KUSAMBAZA UELEWA WA RASIMU YA PILI YA KATIBA YA TANZANIA KWA WANANCHI

 
Mgeni Rasmi Bi.Maafudha Hamidu akiwa amewasili katika ukumbi  
 burudani za muziki wa kiafrika maarufu kama makilikili kikiwa jukwaani kwaajiri ya mapokezi ya mgeni rasmi
 Kikundi cha muziki kutoka haki za binadamu kikiwa kinatumbuiza kumpokea mgeni rasmi akiwa anaingia
Baadhi ya Watu wakiwa wanampokea mgen rasmi kwa kupiga makofi

Tuesday, February 25, 2014

MKUU WA WILAYA YA IGUNGA YUPO ZIARANI,LENGO KUHAMASISHA WANACHI KUJIUNGA NA MFUKO WA AFYA (CHF)

            MKUU WA WILAYA YA IGUNGA ELIBARIKI KINGU AKISISITIZA JAMBO KATIKA KIJIJI CHA IBOLE KATA YA IGURUBI  ANAPOENDELEA NA ZIARA    YA KUWAHAMASISHA WANANCHI KUJIUNGA NA MFUKO WA AFYA YA JAMII CHF (picha na abdala khamis)

TANROADS WATANGAZA NAFASI ZA KAZI MPYA.HIZI HAPA


THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
MINISTRY OF WORKS REGIONAL MANAGER’S OFFICE-KILIMANJARO VACANCIES ANNOUNCEMENT
TERMS AND CONDITION OF SERVICE:
Appointment will be contract terms of two years, renewable subject to satisfactory performance. 



1.POSITION TITLE: SHIFT IN CHARGE-(2 POSITIONS)
SCOPE OF POSITION: 

Successful applicant must be read to work on “shift” basis including weekends and public holydays. They should be willing to work for considerable lengths of time away from their permanent stations with minimum supervision. 

PICHA NNE ZA CHADEMA NA KAMPENI ZA KUSAKA UBUNGE HUKO KALENGA,

Mgombea akisalimiana na wananchi wa Magulilwa

Mgombea Grace Tendega akisalimiana na wakazi Kijiji cha Magulilwa baada ya mkutano wa kampeni

Kamanda Mawazo akiwa na makamanda wa Magulilwa wakiimba na kucheza kabla ya mkutano wa kampeni

Katibu Mkuu akifurahia jambo na mtoto mdogo wa Kijiji cha Magulilwa baada ya mkutano wa Magulilwa

HIKI NDICHO KIKOSI KIPYA CHA TAIFA STARS KILICHOTANGAZWA LEO KUIVAA NAMIBIA


        
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetangaza kikosi cha wachezaji 22 kwa ajili ya mechi ya kirafiki ya kalenda ya FIFA dhidi ya Namibia (Brave Warriors) itakayochezwa Machi 5 mwaka huu jijini Windhoek, Namibia.

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE,HUU NDIO UFAFANUZI ULIOTOLEWA LEO NA BARAZA LA MITIHANI.SOMA HAPA



         UFAFANUZI WA MASWALI MBALIMBALI YA WADAU WA ELIMU KUHUSU MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2013
          
     Baraza la Mitihani la Tanzania lilitangaza matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE) 2013 tarehe 21/02/2014. Baada ya kutangazwa kwa matokeo hayo, Baraza limekuwa likipokea maswali mbalimbali yanayoashiria kuwa baadhi ya wadau wa elimu hawakuelewa vizuri kuhusu Viwango vya Ufaulu (grade ranges), alama ya chini ya ufaulu (pass mark) na Ufaulu wa jumla wa mtahiniwa (overall performance). 

Monday, February 24, 2014

STORY YA MTOTO ALIYECHINJWA,NA NYINGINE NYINGI SOMA MAGAZETI YOTE YA LEO JUMANNE HAPA

 .

.

SOMA TAMKO ALILOTOA WAZIRI NYALANDU,AMTIMUA MKURUGENZI WA WANYAMAPORI


     Leo, TAREHE 24 Februari, 2014 Natangaza kuubadili uongozi wa Idara ya Wanyamapori ya Wizara ya maliasili na Utalii kama ifuatavyo: 

samahani kwa picha hizi hali inatisha sana-----PICHA ZA USTADHI ATENGANISHA KICHWA NA MWILI WA MTOTO JAMALI SALUM LIPAKALE HUKO MBAGALA CHARAMBE HIZI HAPA !!

mwili wa marehemu mtoto Jamali aliechinjwa na ustadhi mbagala charambe mianzini

TAARIFA MUHIMU TOKA TFF.SOMA



 


        
        Fomu za wagombea kwa ajili ya uchaguzi wa Kamati mpya ya Utendaji ya Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) utakaofanyika Machi 2, 2014 jijini Dar es Salaam zimeanza kutolewa leo (Februari 24 mwaka huu).
         
        Mwisho wa kuchukua na kurudisha fomu hizo zinazotolewa Idara ya Habari (Maelezo) ni Alhamisi (Februari 27 mwaka huu) saa 9 alasiri.
         
      Ada kwa wagombea wa nafasi za Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu Mkuu, Katibu Msaidizi, Mhazini na Mhazini Msaidizi ni sh. 50,000 kwa fomu. Nafasi za wajumbe wa Kamati ya Utendaji fomu zinapatikana kwa sh. 20,000.
   
        Kwa mujibu wa Ibara ya 21(e)(i), sifa ya elimu kwa wanaowania nafasi za Mwenyekiti hadi Katibu Msaidizi ni diploma au digrii ya uandishi wa habari. Kwa nafasi nyingine kwa mujibu wa Ibara ya 21(e)(ii) ni cheti cha ngazi yoyote katika uandishi wa habari.
     
     Tunawahimiza wanachama wa TASWA kujitokeza kwa wingi kuchukua fomu ili waweze kuwania nafasi hizo.
Boniface Wambura

     MWENYEKITI KAMATI YA UCHAGUZI TASWA