Showing posts with label BURUDANI. Show all posts
Showing posts with label BURUDANI. Show all posts

Wednesday, October 5, 2022

Kamati ya Kutafuta Mdundo wa Taifa yakamilisha kuchukua maoni Katika Mkoa wa Dar es salaam

Na Moshi Saidi Dsm.

Kamati ya Mdundo wa Kitaifa iliyoundwa hivi karibuni na Waziri Tamaduni Sanaa na Michezo  Mohamedi Mchengrwa imepokea maoni  Kutoka kwa Wadau mbalimbali wa muziki ikiwemo watayarishaji wa muziki,watunzi,watangazaji wa vyombo vya habari pamoja wasanii wa ngoma za asili lengo ni kupata vionjo vitakavyotumika kutengeneza Mdundo wa kitaifa.

Wajumbe wa Kamati ya kutafuta Mdundo wa Kitaifa wakiendelea kukusanya maoni.
Wakitoa maoni katika Mdahalo uliofanyika Jijini Dar es salaam Mkurugenzi kikundi cha muziki (Kay wa Mapacha) Levison Kasuhuwa alisema tangu nchi  imepata  uhuru haijawahi kuwa na mdundo wa kulitambulisha Taifa hivyo wasanii wa muziki wameiga Midundo ya za nje kutengeneza muziki yao hivyo sasa kwakuwa serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassani kupitia kamati iliyochaguliwa lazima ije na mdundo utakaokwenda kubadilisha taswira za watu kuondokana na kutumia Midundo isiyo ya asili yao   

"Tunakubali kuwa ukoloni umetuathiri kwa kipindi kirefu kwa kuacha Tamaduni zetu kuna usemi asiyependa kwao ni mtumwa hivyo tumechoka kuwa watumwa kutumia Midundo ya kigeni Sasa ni wakati wa kuwa na mdundo wetu wa asili ambao utatutambulisha "alisema Levision

Sixmondi Mneka kutoka  chama cha muziki wa Reggae dansi nchini amewasihi na kuwaomba Watanzania kuacha  ushabiki wa makabila na badala  yake kushirikiana Kwa pamoja kuunganisha vionjo vya  makabila mbalimbali ili kutengeneza mdundo wa Taifa utakaotambulisha asili ya mtanzsnia katika mataifa mbalimbali Duniani 

"Watanzania wanatabia ya kuibua jambo lakini hatufiki mwisho hivyo tufanye vitu Kwa Makubaliano ambapo naisihi kamati yenu(kamati ya Mdundo wa Taifa) kuendelea kuifanya kazi hiyo iwe endelevu kulingana na mahitaji ya muziki wetu kwasasa ili kuendelea kuulinda Utamaduni wa kitanzania kupitia Sanaa hiyo ya Burudani."amesema Mneka.
Meneja wa Sisi Tambala Bendi Bw. Kibiriti akitoa maoni yake mbele ya wajumbe wa Kamati ya kutafuta Mdundo wa Kitaifa. 
Nae Meneja wa Sisi Tambala Bendi Bw. Kibiriti Nanjuja ameshauri kuwa ngoma za asili za makabila mbalimbali zenye vionjo vya kuvutia ndizo zitumike katika kutengeneza mdundo wa Kitaifa ,nakwama Jamii isipuuzie ngoma za asili kwani ndio utambulisho halisi wa Utamaduni wa Mtanzania kupitia Sanaa hiyo .

Akizungumza na Waandishi wa habari mara baada ya mdahalo huo Makamu Mwenyekiti kamati ya Mdundo wa asili Tanzania Masoud Masoudi ambaye ni Manju Muziki amesema kwamba zoezi la kutengeneza mdundo wa Kitaifa unatokana na nia ya Rais Samia Suluhu Hassan ambaye amenuia kulinda Mila na Tamaduni za Mtanzania kwani zimekuwa zikisahaulika tangu Tanzania ipate uhuru..

" Tumekubali kwa maoni ya wadau ambao wanaonekana wanakubaliana na dhana nzima ya Mdundo wa Taifa,wamekubali kwamba mdundo wa Taifa ni Muhimu,hivyo kuelewa mdundo wa Taifa ni hatua Moja kubwa sana" Amesema Masoud ambaye pia ni Mtangazaji wa TBC 

Tuesday, July 5, 2022

Luiza Mbutu "Tunaisuka CHAMUDATA Mpya wasanii wa Dansi nchi nzima waje kujiunga".

Na Muandishi wetu.

Chama Cha Muziki wa Dansi Nchini (CHAMUDATA) kimewataka wasanii wote wa Muziki wa Dansi kujitokeza kuhisajili kwenye chama hicho pamoja na Baraza la Sanaa la Taifa( BASATA) ili kuwawezesha kutambulika.
Mwenyekiti wa CHAMUDATA Luizer Nyoni(Luiza Mbutu) akiongea na waandishi wa Habari ambao hawapo pichani mapema leo mkoani Dar es salaam.
Rai hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa chama hicho Luizer Nyoni maarufu Kama mama "Luizer Mbutu"wakati wa Mkutano na Waandishi wa habari kuelezea mwelekeo mpya wa Chama hicho baada ya kupata uongozi mpya 

Amesema kwamba wasanii wengi wa Dansi hawajajisajili kwenye Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) pamoja na CHAMUDATA hivyo kutokana na kupatikana na uongozi mpya wa Chama hicho kinawasihi kuhisajili ili kufikia malengo yao kwani CHAMUDATA ya Sasa imejiwekea malengo makubwa.

"Sisi kama viongozi wapya tuna  vipaumbele kumi tutakavyo vitekeleza ikiwa ni pamoja na kueneza CHAMUDATA nchi nzima, kuandaa semina ya mafunzo ya hakimiliki na hakishiriki na mirahaba ambapo tayari tumezungumza na COSOTA ili watupe mafunzo,pia kukutana na viongozi wa bendi mbalimbali ili kuainisha changamoto zinazowakabili Wanamuziki na Biashara ya Muziki Kwa Ujumla." amesema Luizer

Nakuongeza kuwa vipaumbele vingine ni kushirikiana na vyombo vya habari katika kuutangaza Muziki wa Dansi,kutengeneza tovuti ya CHAMUDATA Ili kusaidia wanachama kuhisajili kidigitali,kusimamia masuala ya Bima ya afya Kwa wanachama,kuiwezesha CHAMUDATA kuwa karibu na serikali ili kutatua changamoto zinazowakabili,kuhakikisha bendi zote zinazofanywa maonyesho zimesajiliwa BASATA pamoja na kuandaa Tamasha kubwa la Muziki wa Dansi.
Katibu Mkuu wa CHAMUDATA Bw. Said Kibiriti akijibu swali la Muandishi wa habari mapema leo Mkoani Dar es salaam.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa CHAMUDATA  Bw.Said Kibiriti amesema kwamba uongozi uliopo Kwa sasa ni uongozi mpya,baada ya kukabidhiwa ofisi na uongozi wa zamani baadhi ya nyaraka za ofisi hazipo nakwamba baada takufatilia wamebaini baadhi ya viongozi hao wameshafariki,hivyo kumekuwepo na madeni huku akaunti za chama  za  NMB na CRDB zikiwa hazina fedha.

" Hatuna Hesabu Sahihi ya madeni kwasasa,lakini bado tunaendelea kuyakusanya na yakiwa tayari tutawafahamisha wanachama,kwasasa tuanaendelea kukiimarisha chama kwani kimeanzishwa tangu mwaka 1986 lakini bado kimekuwa hakifahiki vizuri kwa wanamuziki wa Dansi Nchi nzima" amesema Bw.Kibiriti.
Mkutano ukiendelea.

Monday, July 4, 2022

MHE. MCHENGERWA SERIKALI KUJENGA STUDIO KILA WILAYA NCHINI

Na John Mapepele

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa amesema Serikali inakwenda  kutengeneza studio kila wilaya kwa ajili ya kurekodia kazi za sanaa.
Mhe. Mchengerwa ameyasema haya leo Julai 3, 2022 wakati akifunga tamasha la kwanza la  kitaifa la utamaduni katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Amesema wizara yake inakwenda  kutekeleza maelekezo ya viongozi wetu ya kuthamini, kuandaa  mavazi ya taifa ili kuhakikisha mila na desturi za mtanzania zinaendelezwa.

"Maelekezo ya viongozi wetu ni sheria, amri iwe jua, iwe mvua  sisi Wizara, tutawajibika kutekeleza bila kusita wala kuchelewa" Amesisita Mhe. Mchengerwa

Pia amesema  wizara imejipanga vizuri kuhakikisha Tamasha la kitaifa la pili la Utamaduni litakalofanyika mwakani litakuwa katika kiwango cha kimataifa.

Ameongeza kuwa kumalizika  kwa tamasha hili ni mwanzo wa kuanza maandalizi ya matamasha kwenye mikoa  na wilaya zote nchini ambapo ametaka maafisa utamaduni kulisimamia hili.

"Ni matarajio yangu kuwa mikoa yote itakaoanza sisi kama wizara tutakuja mara moja. Tunahitaji watanzania wakae katika furaha katika maisha yao" amefafanua Mhe. Mchengerwa

Amewapongeza wakuu wa mikoa  kwa kuwezesha  vikundi  vya Utamaduni kuhudhuria kwenye tamasha.

Amesema  bila Utamaduni taifa hili litaendelea kukopa tamaduni za mataifa mengine.

Aidha, amesema  kufanikiwa kwa tamasha hili kuonekana  ni kutokana na maono ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan 

Amesisitiza kuwa tamasha hili litakuwa endelevu na litakuwa  linafanyika kwa mzunguko kila mkoa.

Pia amesema Wizara imefanikiwa kulitangaza tukio hili kwa  kuwa watu zaidi ya milioni  10 wametazama kupitia mitandao ya kijamii na vyombo vya habari.

"Niseme kwa hili tumefanikiwa" amepongeza Mhe. Mchengerwa

Kwa upande mwingine Selikali imeanzisha Mfuko wa Utamaduni kwa lengo la kuwasaidi wasanii nchini ambapo amesema tayari kwa mwaka 2022/2023 umetengewa shilingi bilioni mbili kwa kazi hiyo.

Amewaomba viongozi wa mila  na wananchi kwa ujumla kuendelea kukemea vitendo ambavyo ni kinyume cha maadili ya mtanzania.

Pia amewataka wananchi kushiriki kwenye sensa.

Katika tamasha  hilo amekadhi zawadi kwa washindi wa ngoma na vyakula ambapo washindi wa ngoma za asili ni mkoa wa
Mwanza ambao umekuwa namba moja, Lindi ambao umekuwa namba mbili na mkoa wa
Mjini magharibi umekuwa wa tatu.

Kwa upande wa vyakula vya asili mkoa Kilimanjaro umeongoza ukifuatiwa na mkoa wa Tanga na mkoa wa Kagera umeshika nafasi ya tatu

   Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Mohamed Mchengerwa akikabidhi Zawadi kwa  Vikundi vya Ngoma za Asili vilivyofanya vizuri vikiongozwa na Mkoa wa Mwanza, wakifuatiwa na Lindi na mshindi wa tatu ni Mkoa wa Magharibu kutoka Zanzibar katika  kucheza ngoma za Asili kwenye  Tamasha la kwanza la Kitaifa la Utamaduni lililofanyika Julai 01 hadi 03,Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam.

Sunday, July 3, 2022

MAJALIWA: WATANZANIA TUISHI KWA KUZINGATIA MILA NA DESTURI ZETU

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amefungua Tamasha la Kwanza la Kitaifa la Utamaduni na kuwataka watu wote wanaojihusisha na vitendo viovu vinavyokiuka misingi ya maadili waache mara moja na badala yake waamue kuishi kwa kuzingatia mila na desturi za Kitanzania.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akionyesha nakala za Mwongozo wa Maadili  na Utamaduni wa Mtanzania baada ya kuuzindua  katika Tamasha la Kwanza  la Kitaifa la Utamaduni  lililofanyika kwenye uwanja wa Uhuru, Temeke Mkoani Dar es salam, Julai 2, 2022. Katikati ni Waziri wa  Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mohamed Mchengerwa na kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Tameke, Joketi Mwegelo. (Picha na ofisi ya Waziri Mkuu)

“…kwa kuwa suala zima la maadili linaanzia katika ngazi ya familia na jamii, ninatoa wito kwa wazazi na walezi, taasisi za dini, machifu na wadau wengine, kuendelea kukemea uovu huo na kuwafunza watoto na vijana wetu maadili mema ili kukilinda kizazi chetu cha sasa na kijacho.”

Waziri Mkuu amefungua tamasha hilo leo (Jumamosi, Julai 02, 2022) katika Uwanja wa Uhuru, Temeke mkoani Dar Es Salaam. Amesisitiza kuwa kuwa familia ni kitovu cha makuzi na malezi kwa watoto na vijana. “Familia ni asasi ya msingi na muhimu katika mfumo wa jamii na hivyo inaweza kuendeleza maadili, malezi na urithishaji wa utamaduni wetu wa Kitanzania.”

Waziri Mkuu amesema walezi na wazazi wanatakiwa wajifunze kutilia maanani malezi ya watoto kwa kutenga muda wa kukaa na watoto na vijana na siyo kuziachia shule peke yake. “Tushirikiane na Serikali, taasisi za dini na wadau wengine, kukemea mmomonyoko wa maadili katika Taifa letu.”

 Waziri Mkuu amewataka vijana wote wa Kitanzania waache kuendekeza tabia ya kutumia muda mrefu kwenye mitandao ya kijamii kwa kusoma au kuangalia mambo ambayo hayaongezi thamani ya maisha yao na badala yake watumie muda huo kufanya kazi. “Tutumie mitandao kutafuta maarifa yanayofaa na tujikite zaidi katika shughuli mbalimbali za uzalishaji.”

“Kwa kuwa maadili ni chimbuko la uzalendo na utu wetu, ninaitaka Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kuongeza jitihada katika kuandaa programu za elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa kuheshimu na kuthamini mila na desturi zetu, pamoja na uzalendo, ili tutengeneze kizazi kinachozingatia maadili mema. Tusikubali kamwe kuwa watumwa wa tamaduni za kigeni.”

Amesema jukwaa mojawapo ambalo wizara hiyo inaweza kuanza nalo ni kuandaa mdahalo wa kitaifa kuhusu mmomonyoko wa maadili, ambapo wanaweza kupata picha halisi ya hali ya maadili ilivyo nchini kwa sababu watakutanisha makundi mbalimbali.

“Programu nyingine ni kuunda kablu za maadili katika shule za msingi na sekondari. Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) wana klabu ambazo zinawaelimisha wanafunzi kuhusu mapambano dhidi ya rushwa. Kwa hiyo na nyinyi Wizara kwa Kushirikiana na TAMISEMI igeni mfano huo mzuri.”

“Nyote mtakubaliana nami kwamba hali ya mmomonyoko wa maadili katika Taifa letu ni mbaya sana kwa rika zote. Mlezi wetu namba moja Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamuhuri ya  Muungano wa Tanzania na mama mlezi wa familia anaguswa sana jambo hili ambapo, katika hotuba zake nyingi haachi kugusia suala la maadili.”

“Vilevile, tumeshuhudia baadhi ya vitendo viovu vingi kama vile kuongezeka kwa vitendo vya watoto kuwauwa wazazi wao; ulawiti; wanawake kuuwawa na waume zao; ubakaji hususani kwa watoto na wanafunzi; watoto na vijana kutowaheshimu watu wazima hususani katika vyombo vya usafiri na kutumia lugha zisizofaa wanapozungumza na watu wazima; uvaaji wa mavazi yasiyo na stara hususani kwa wasichana na wavulana na matumizi ya madawa ya kulevya.”

Akizungumzia kuhusu umuhimu wa tamasha hilo, Waziri Mkuu amesema tamasha hilo limetokana na agizo la Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alilolitoa akiwa mkoani Mwanza tarehe 8 Septemba, 2021 kwenye Tamasha la Utamaduni. “Mheshimiwa Rais alielekeza yafanyike matamasha ya utamaduni ya namna hii nchi nzima.”

“Naiagiza Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, iandae mwongozo wa jinsi gani matamasha haya yataendeshwa. Pia ninaiagiza Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kushirikiana na wadau ambao wanaandaa matamasha ya Utamaduni. “

Pia, Waziri Mkuu amesisitiza kuwa wadau wahakikishe wanaishirikisha Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo wanapoandaa matamasha yao wahakikishe wizara husika inafahamu. “Si vema mdau unaandaa tamasha huku wizara yenye dhamana na utamaduni haifahamu kabisa au inafahamu dakika za mwisho.”

Akizungumzia kuhusu vyombo vya habari, Waziri Mkuu amesema vyombo vya habari vinatakuwa viwe walimu wema wa kuhakikisha maadili yanazingatiwa, visiwe chanzo cha mmomonyoko wa maadili. “Hakikisheni mnakagua kazi zenu kabla hamjazirusha hewani hususani filamu, muziki au programu zinazotoka nje ya nchi.

Kwa upande wake, Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mohamed Mchengerwa  amesema tamasha hilo ambalo linafanyika kwa siku tatu lilianzia jana Julai Mosi, 2022 litamalizika kesho Julai 3, 2022, limeandaliwa mahsusi katika wiki ya kuelekea siku ya Kiswahili Duniani ambayo kilele chake ni Julai 7, 2022.

Amesema Tamasha hilo litachagizwa na shughuli mbalimbali zikiwemo mashindano ya ngoma za kitamaduni na vyakula vya asili pamoja na maonesho ya bidhaa mbalimbali za kitamaduni. Kauli mbiu ya tamasha hilo inasema “Utamaduni wetu; tujiandae kuhesabiwa, kazi iendelee.”

Amesema moja ya matokeo tarajiwa la tamasha hilo ambalo limeshirikisha mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani ni kuwepo kwa hamasa kubwa nchini ya kupenda, kuhifadhi, kulinda, kuendeleza mila na desturi ambazo ndio msingi wa maadili na utambulisho wa Taifa kwa ujumla.

Awali, Mheshimiwa Majaliwa alipokea matembezi ya utamaduni ambayo yalihusisha wananchi kutoka katika mikoa mbalimbali ya Tanzania ambao walipita wakiwa katika magari ya wazi huku kila mkoa ukionesha na kucheza ngoma za utamaduni za mkoa husika.Tamasha hilo limejumuisha matembezi ya kiutamaduni (road carnaval) katika mitaa ya jiji la Dar es Salaam.

Wednesday, June 22, 2022

MAKAMU WA RAIS OTHMAN AZINDUA TAMASHA LA ZIFF2022

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Othman Masoud Othman.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Othman Masoud Othman, amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), itatengeneza na kusimamia Sera ya Filamu itakayohakikisha kukua kwa utamaduni na kusaidia kuweka mazingira bora ya uwekezaji utakoimarisha ushirikiano wa kidiplomasia na mataifa mengine.

Mheshimiwa Othman ameyasema hayo Usiku wa Juni 19, mwaka huu wakati wa Sherehe za Ufunguzi wa Tamasha la 25 la Filamu kwa Nchi za Jahazi (ZIFF) zinazoendelea kwa siku 9 katika viunga vya Ngome-Kongwe, Forodhani, Mjini Unguja.

Mhe.Othman amesema kuwa hiyo ni kutokana na uhalisia kwamba mwendelezo wa harakati za Tamasha la Filamu na Maonyesho ya shughuli mbali mbali za Utamaduni wa Asili wa Mzanzibari na Nchi za Jahazi, zinaitambulisha Zanzibar duniani na kwamba ni miongoni ma fursa muhimu za kuikuza Nchi kiuchumi.

Ambapo amesema matukio ya kitamaduni, kama vile Tamasha la ZIFF linaloendelea sasa nchini hapa, huwezesha ubadilishanaji wa moja kwa moja wa mawazo, mila, silka na maongezi kati ya jamii za watu tofauti, hasa kwa kuzingatia uzuri na upekee wa Visiwa vya Zanzibar tangu asili uliotokana na historia ndefu katika ulimwengu wa ustaarabu.

Mhe.Othman amebainisha kuwa Binaadamu daima hujisikia vyema anapoweza kutambulisha ustaarabu wake na wengine wakasifia na kuweza kujifunza kutoka kwake, ambapo hiyo ni katika siri za Tamasha la Utamauni wa Nchi za Jahazi.

"Katika kujifunza tunapata kubadilishana mawazo, ujuzi, ufahamu na elimu, vitu ambavyo ni muhimu kwa maendeleo ya binadamu na ni sehemu muhimu sana ya kuenzi na kutukuza utu wetu katika njia ya mshikamano na hivyo kuwa kielelezo cha haki, amani na ustawi wa kimataifa", amesisitiza Mheshimiwa Othman.

Aidha amesema kuwa filamu zinazungumza lugha moja; ni muhimu na zina maana sawa  kwa ulimwengu na watu wote, bila kujali asili zao za kitaifa, kitamaduni au kijamii ambapo pia ni njia moja maarufu ya sanaa za kisasa, zinazovunjavunja vizuizi baina ya watu, mataifa na tamaduni, huku zikisisitiza maadili, hisia na utashi ambao mwanadamu daima anapenda kuudhihirisha kupitia kubadilishana mawazo.

Katika nasaha zake Mheshimiwa Othman ametoa wito kwa wageni ambao ni kutoka ndani na nje ya Afrika, wakiwemo washiriki kutoka Oman,Falme za Kiarabu, na Umoja wa Ulaya, kutenga muda na kutembelea vivutio vya Zanzibar kwa ujumla, na kujionea urithi na utajiri wa utamaduni wa visiwa hivi,huku akisisitiza kwa kusema, "haya ni maendeleo ya kipekee ya Tanzania ya leo na ndipo tunapoona umuhimu wa kuwa na Tamasha la Kimataifa".

Aidha, akabainisha:
"Kupitia mahusiano haya wakaambukizana utamaduni na urithi wa dunia; ndiyo maana ni furaha kubwa kuona kwamba kwa kupitia Tamasha hili tunaendeleza nguzo hiyo moja muhimu ya utu na urithi wa binadamu", ameongeza Mheshimiwa Othman.

Kwa upande wake Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo, Bi Tabia Maulid Mwita amesema kuwa daima amekuwa akifahamisha tija ya ziada iliyopo katika ufanikishaji wa Tamasha la Filamu la ZIFF hapa visiwani, ikiwemo upeo mpya wa ubunifu baina ya watengeneza- filamu wa Tanzania, na kwamba ikitokea shaka yoyote dhidi ya mila na silka za asili, ni vyema watu wasisite kuibuka na kushauri ili kunusuru utamaduni uliojaa ustaarabu wa Kizanzibari. 

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya ZIFF, Bw. Hassan Mitawi amesema kuwa filamu ni chombo muhimu cha kuelezea maisha na utamaduni wa watu na jamii yeyote inayohitaji maendeleo katika nyanja zote za maisha zikiwemo za uchumi. 

Akieleza mafanikio ya ZIFF kwa Kpindi cha Miaka 25 tangu kuasisiwa kwake, Mkurugenzi Mtendaji wa Tamasha hilo hapa Visiwani, Profesa Martin Mhando amesema kuwa katika miaka ya hivi karibuni, tasnia ya filamu ya Tanzania na Afrika kwa ujumla imestawi, ambapo filamu bora zaidi za Kiafrika na hata za Kitanzania zinaonekana katika orodha ya Tuzo za Kimataifa. 

Nae Mkurugenzi Mkuu a Tamasha hilo, Prof. Martin Mhando alibainisha kuwa, Watengeneza filamu wa Kitanzania kupitia Tamasha hilo, watapata fursa adhimu ya kutazama filamu kutoka nchi mbalimbali zilizochaguliwa vyema, zenye mandhari na mitindo mbalimbali, ili kujifunza zaidi. 

Aidha, alisema kuwa, Mwaka huu takribani filamu 3450 kutoka Nchi 33 ziliingia katika mchujo na hatimaye 101 zilipata kupita na kuoneshwa kupitia Tamasha hilo. 

Watu Mashuhuri na Viongozi mbali mbali wa Serikali na Asasi za Kiraia wamejumuika katika tukio hilo.

Sunday, June 19, 2022

Efm kuzindua kipindi kipya kiitwacho "Jioni ya Leo"

Vipindi vingi vya redio vinavyoanza majira ya jioni kuanzia saa 10 havifanyi vizuri kama inavyotakiwa na hii nimeiona katika utafiti wangu na kuamua kuja na kipindi kitakachokonga nyoyo za mashabiki wetu hapa nchini Tanzania.

Hayo yameelezwa mapema jana mkoani Dar es salaam na Mkuu wa vipindi kutoka kituo cha Efm Redio Bw. Dickson Ponera wakati wa uzinduzi wa kipindi kipya kiitwacho "Jioni ya Leo" kitakachorushwa na Redio hiyo.

Aidha ameongeza kuwa kipindi hicho kitakuja kuleta mapinduzi makubwa sana kwani kitakuwa kimesheheni mambo mengi mazuri na kuunganisha watangazaji kutoka katika vipindi tofauti vya Efm, akiwemo Dina Marious aliyetoka katika kipindi cha uhondo, Osca Osca sports HQ, Mpoki na Roman Shirika kutoka kipindi cha ubaoni.

Ameendelea kusema kusema kuwa Kipindi hichi cha "Jioni ya Leo" kitakuwa siki za katikati ya wiki na kitaanza saa 10 mpaka saa 1 kamili usiku na kuchukua nafasi ya kipindi cha Ubaoni ambaho ndio kilikuwa kikianza na kumalizika muda huo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Efm Bw. Dennis Busolwa (Sebo) akiongea na waandishi wa habari katika Tafrija fupi ya kutambulisha kipindi kipya cha "Jioni ya leo" kilichozinduliwa makao Makuu ya Media hiyo Mkoani Dar es salaam.

Mkurugenzi wa Vipindi Efm Dickson Ponera (Dizzo ONE) akizungumza katika hafla iliyoandaliwa na kituo cha Radio cha Efm mapema jana mkoani Dar es salaam.
Mtangazaji wa Muda mrefu Dina Marios Akiongea na waandishi wa habari katika hafra fupi ya kutambulisha kipindi kipya cha "Jioni ya leo" kilichozinduliwa jana makao makuu ya Efm Redio Mbezi Beach mkoani Dar es salaam.
Tafrija ikiendelea.
Baadhi ya Viongozi na Watangazaji wa Efm wakishangaa bango la kipindi kipya cha "Jioni ya leo" baada ya uzinduzi mapema jana Mkoani Dar es salaam.




Thursday, April 26, 2018

Uzinduzi wa malori wa kustajaabisha zaidi katika kanda

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya CFAO Motors, Marius Prinsloo (wa pili kulia) akizungumza na waandishi wa habari juzi jijini Dar Es Salaam kwenye hafla ya uzinduzi wa Malori mapya ya kisasa ya Mercedes Benz aina ya Actros na Arocs. Wengine kwenye picha kutoka kulia ni Maneja Mauzo wa MB Trucks Africa, Hansjorg Richter, Mkuu wa Kitengo cha Mauzo na Huduma kwa Wateja Mercedes Benz Trucks Africa, Torsten Bauerheim na mwisho kushoto ni Meneja Chapa wa Mercedes Benz Tanzania, Jerome Sentimea. 
Mkuu wa Kitengo cha Mauzo na Huduma kwa Wateja Mercedes Benz Trucks Africa, Torsten Bauerheim (wa pili kushoto) akizungumza na waandishi wa habari juzi jijini Dar Es Salaam kwenye hafla ya uzinduzi wa Malori mapya ya kisasa ya Mercedes Benz aina ya Actros na Arocs. Wengine kwenye picha kutoka kushoto ni Meneja Chapa wa Mercedes Benz Tanzania, Jerome Sentimea, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya CFAO Motors, Marius Prinsloo na Maneja Mauzo wa MB Trucks Africa, Hansjorg Richter
Meneja Chapa wa Mercedes Benz Tanzania, Jerome Sentimea (wa kwanza kushoto ) akizungumza na waandishi wa habari juzi jijini Dar Es Salaam kwenye hafla ya uzinduzi wa Malori mapya ya kisasa ya Mercedes Benz aina ya Actros na Arocs. Wengine kutoka kulia ni Maneja Mauzo wa MB Trucks Africa, Hansjorg Richter, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya CFAO Motors, Marius Prinsloo na Mkuu wa Kitengo cha Mauzo na Huduma kwa Wateja Mercedes Benz Trucks Africa, Torsten Bauerheim


·  Mercedes-Benz inapeleka mbele historia ya malori yenye nguvu nchini TANZANIA

·       Malori yote mapya aina ya Actros na Arocs yamezinguliwa
Tarehe 8/02/2019 Jijini Dar es salaam. Actros mpya kabisa: Ni malori ya kuaminika na yenye ufanisi kwaajili ya masafa marefu na usamabazaji yamezinduliwa leo katika mji mkuu wa Tanzania.

Akiongea katika hafla hiyo ya kupendeza, Mkurugenzi wa Mauzo na Huduma kwa Wateja wa Malori ya Mercedes Benz Afrika Bwana Mr Torsten Bauerheim akisema, 'Malori yote mapya ya Actros na Acros yanakuja na injini yenye ufanisi yenye silinda 6 katika mstari, vyumba vya dereva vya kisaa vinavyoruhusu hewa kupita na Mercedes PowerShift 3 ya kisasa, injini ya kujiendesha yenyewe zikiwa na miundo mbalimbali tofauti kutegemeana na mazingira ya kanda husika.  Aliongeza kuwa, Malori yote mapya ya Actros ni ya kuaminika na ya uhakika kwaajili ya ujenzi na matumizi katika barabara za vumbi na zote zimepitia majaribio makali ya ubora ya zaidi ya kilomitea milioni 60 kabla ya kufanya uzinduzi wa soko.

Mkurugenzi Mtendaji wa wasambazaji walioithibishwa wa Mercedes-Benz, CFAO Motors Tanzania Ltd, Bwana Marius Prinsloo amesema kwamba 'Maloti mapya ya Actros na Arocs yanatoa kiwango cha ziada cha uimara, ufanisi katika matoleo ya malori ya Mercedes-Benz Yakiwa yametengenezwa katika kiwanda cha malori kikubwa kuliko vyote duniani nchini Ujerumani, Malori haya yanakuja katika aina mbalimbali mahususi kwaajili ya soko letu la Tanzania - yakiwa yamebuniwa na kutengenezwa kuhimili mazingira magumu ya uendeshaji.

Yamejaribiwa kwa kina duniani kote, katika barabara za aina zote na katika mazingira magumu zaidi, magari haya ni mifumo bora zaidi kwaajili ya kazi ngumu. Majaribio yalijumuisha jumla ya zaidi ya kilometa milioni 6 za mbio za ustahimilivu zilizofanywa na kituo cha majaribio ya malori ya Mercedes-Benznchini Abu Dhabi, Umoja wa Falme za Kiarabu.
Aliongeza kuwa 'Chumba kipya cha pekee cha dereva kinajivunia kiwango cha juu cha vifaa na mazingira mazuri ya ndani, wakati uendeshaji ni rahisi na wakustarehesha . Aina zote mbili za malori ya Actros na Arocs zinavutia kwa teknolojia ya kisasa zaidi na mfumo wa kuaminika wa uendeshaji kutokea chanzo kimoja.  Injini zenye ustahimilivu, zenye nguvu na zenye ufanisi zinapatikana katika aina za utoaji moshi wa Euro III, IV na V, ikiwa inatoa aina mbalimbali za nguvu ya msukumo kuanzia 240 kW (326 hp) mpaka 460 kW (625 hp). Ikiwa imeunganishwa na toleo la hivi karibuni la Mercedes PowerShift 3, gia boksi ya kujiendesha yenyewe, malori ya Actros na Arocs yanafikia kiwango cha juu cha ufanisi wa mafuta, ikiwa inachangia kuongeza faida za uendeshaji

Actros mpya zimetengenezwa kwaajili ya usafirishaji wa masafa marefu pamoja na usambazaji wa mizigo mizito. Zinapatikana na mpaka aina 22 tofauti za chumba cha dereva na zinakuja katika matoleo ya chuma au ya kushikiliwa na upepo. Kwaajili ya mazingira magumu ya uendeshaji, Actros zinapatikana katika injini zenye nguvu za 15.61 na kasi ya 16 na gia boksi ya kujiendesha yenyewe ya Mercedes PowerShift 3

'Arocs mpya ya kustaajabisha iko kwaajili yako pale utakapo kuwa unahitaji ustadi wa kipekee - iwe katika shughuli za ujenzi mbali na barabara za lami. Malori ya Arocs yenye ustahimilivu mkubwa yanaweza kufanya kazi katika mazingira magumu zaidi ya barabara za vumbi mbali na bara bara za lami. Arocs zinapatikana kama Chassis-, Mixer-, Tipper- na aina mbalimbali za uendeshaji - kuanzia miundo ya 4x2 mpaka 8x8 na uzito (GCW) wa mpaka kufika tani 250.

Kwa kudokeza, Actros na Arocs yanaweka viwango vipya pale inapokuja kuhusu suala la usalama na mifumo ya usaidizi, inayomsaidia dereva na kuokoa maisha. Bwana Torsten Bauerheim alihitimisha.


Tamasha la Tigo Fiesta Vibe Kama Lote Mjini Iringa


 Mshindi wa Tigo Fiesta Supa Nyota 2018 mkoani Iringa kwa jina la usanii PPT akitoa burudani kwenye jukwaa la Tigo Fiesta
Msanii wa Bongo Fleva Chege akiwa kwenye jukwaa la Tigo Fiesta Vibe Kama Lote usiku wa kuamkia Jumatatu tamasha lililofanyika  kwenye uwanja wa Samora Mjini Iringa

Mkuu wa Wilaya ya Iringa , Richard Kasesela akilishwa keki na msanii Chege ambaye usiku wa Tigo Fiesta mjini Iringa ilikuwa sherehe ya siku yake ya kuzaliwa

Mkuu wa Wilaya ya Iringa , Richard Kasesela (mbele kulia) akicheza pamoja na wasanii waliotoa burudani kwenye Tamasha Kubwa la Tigo Fietsa 2018 Vibe Kama Lote  uwanja wa Samora Mjini Iringa Usiku wa kuamkia jumatatu

Nyota wa Iokote Maua Sama akitoa burudani kwenye Jukwaa la Tigo Fiesta Iringa.



Tamasha la Tigo Fiesta Vibe Kama Lote 2018 limeendelea usiku wa kuamkia jumatatu kwenye uwanja wa Samora mjini Iringa. Hii ni mara ya tatu mfululizo kwa kampuni ya simu za mkononi Tigo kudhamini tamasha hilo.
Akizungumza mbele ya umati wa mashabiki waliohudhuria tamasha hilo Mkuu wa wilaya ya Iringa mjini, Richard Kasesela amepongeza kampuni ya Tigo kwa kuwaletea burudani na fursa mbalimbali kwa wakazi wa Iringa. "  Hii ni fursa ya pekee kwa wakazi wa mji huu ambayo kampuni ya Tigo imetuletea kwa mara nyingine ndani ya mkoa huu" Ukiondoa Burudani, pia wafanyabiashara wamenufaika sana ndani ya wiki nzima alisema Kasesela.
Pia mkuu huyo wa wilaya aliweza kupata nafasi ya kumkabidhi zawadi ya Keki kwa msanii Chege Chigunda kwa kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwake.
Kwa upande wa Burudani wasanii wa kundi la Weusi ndio waliofunika kwenye tamasha hilo ilipopelekea mashabiki kuomba wasitoke kwenye jukwaa na kundi la Weusi walifanya hivyo hadi mwisho wa shoo kwa kuimba nyimbo zao nyingi za kuvutia zikiwemo, Madaraka,Swagire, NiCome na nyingine nyingi.
Mdhamini mkuu wa msimu huu, kampuni ya Tigo imewakumbusha mashabiki wote wa muziki kufurahia promosheni zake tatu murwa katika msimu hii wa vibes. ‘Data Kam Lote inawapa wateja hadi mara mbili ya vifurushi vya intaneti watakavyonunua kupitia menu iliyoboreshwa ya *147*0#. Hii itawawezesha wateja wa Tigo kufurahia msimu huu wa vibes kupitia mtandao wa kasi ya juu zaidi wa Tigo 4G+.

Tigo pia inatoa punguzo kubwa la bei kwa tiketi za tamasha la Tigo Fiesta 2018 zitakazonunuliwa kupitia Tigo Pesa Masterpass QR. Kwa Sumbawanga, tiketi zitakazonunuliwa kwa mfumo wa Tigo Pesa Masterpass QR zitagharimu TSH 5,000 pekee badala ya TSH 7,000 kwa watakaonunua kwa pesa taslim, Wateja wanapaswa kupiga *150*01#  na kuchagua 5 (lipia huduma) kisha kuchagua namba 2 (lipa Masterpass QR) na kutuma kiasi husika kwenda namba ya Tigo Fiesta 78888888.

Wateja wa Tigo pia watapata faida zaidi kupitia shindano la Tigo Fiesta 2018 – Chemsha Bongo Trivia linalotoa zawadi za kila siku za TSH 100,000, zawadi za kila wiki za TSH 1 milioni, simu janja za mkononi zenye thamani ya TSH 500,000 kila moja, pamoja na donge nono la TSH milioni 10 kwa mshindi wa jumla. Kushiriki wateja wanapaswa kutuma neno MUZIKI kwenda 15571 au kutembelea tovuti ya  http://tigofiesta.co.tz na kuchagua Trivia.

Wednesday, April 11, 2018

BONGO MOVIE KUIBUA VIPAJI VIPYA NA KUHUBIRI AMANI, UPENDO NA UZALENDO TANZANIA

Mwenyekiti wa Uzalendo Kwanza ambaye ni Mratibu wa Tamasha la Iringa ya Kwetu, Kijana Amka tufanye kazi, Steve Nyerere akizungumza leo na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuelezea Tamasha la 'Iringa ya Kwetu, Kijana Amka tufanye kazi,' Pembeni (kushoto) ni Msanii Shamsa Ford na kulia ni Msanii Wolper.
 Wasanii waliohudhuria utambulisho wa Tamasha la 'Iringa ya Kwetu, Kijana Amka tufanye kazi.
Msanii wa maigizo na filamu nchini, Single Mtambalike maarufu kwa jina la Richie akifafanua machache. 

 Na Mwandishi Wetu

Kundi la Wasanii wa Muziki, Bongo Fleva, Mziki wa Singeli na Filamu nchini wanataraji kutoa elimu ya kujikwamua kiuchumi vijana wa Iringa katika Viwanja vya Mwembe Togwa mkoani Iringa. 

Akizungumza wakati wa utambulisho wa Mwenyekiti wa Uzalendo Kwanza ambaye ni Mratibu wa Tamasha la Iringa ya Kwetu, Kijana Amka tufanye kazi, Steve Nyerere amesema kuwa Tamasha hilo lenye kauli mbiu ya 'Kijana wa Iringa inuka tukafanye kazi,'. 

 “Tunataka tuwaonyeshe vijana kuwa huyu Wolper, JB au Steve Nyerere awakuwa wasanii maarufu moja kwa moja bali kuna maisha walipitia mpaka kufikia hapo hivyo wanatakiwa kufanya kazi ili waweze kufikia mafanikio kutoka kijiweni na kuwa wajasilimali kama walivyo hawa wasanii wakubwa” amesema Steve. 

Kwa upande wake Msanii mkongwe kwenye tasnia ya filamu nchini, Msanii maarufu wa Bongo Movies Jacob Steven 'JB amesema wanafika Iringa kwa lengo moja tu la kuhakikisha wanaonana na wasanii na vikundi vya Iringa kwa lengo la kutaka kuwainua kitaaluma kwa kuwapa uzoefu ambao wameupata kwa zaidi ya miaka 20. 

Amesema tunajua kuna wasanii wengi sana huku mikoani lakini je ni muda gani wanapata nafasi hivyo wanakwenda Iringa na wataacha mabalozi ambao ndio watakuwa maharufu katika kizazi kijacho cha filamu. 

Kwa upande wake Msanii maharufu wa kike wa filamu nchini, Jackline Wolper amesema umaharufu hauzuii kufanya mambo ya msingi kama ujasiliamali ili aweze kujiongezea kipato. Amesema kuwa licha ya kuwa maarufu bado amekuwa akijihusisha na ufundi cherehani kama sehemu ya kujiongezea kipato katikamaisha yake ya kila siku.
Msanii Jackline Wolper akifafanua machache.
Mwenyekiti Steve akitoa ya Moyoni.

Tuesday, April 10, 2018

UBUNIFU: MAKEKE KUJA NA VAZI LA UNGO LIJULIKANALO KAMA "LUPAHERO".

 Jinsi wazo lilivyopatikana.

Katika maandalizi yaonyesho la kwanza kufanywa chini ya MAKEKE INTERNATIONAL lililofahamika kama I AM MAKEKE ndipo wazo hili la lupahero lilipozaliwa. Kwamujibuwa MAKEKE INTERNATIONAL ilimchukua muda mrefu kupata wazo la kufanya katika onyesho hilo licha ya kua na bidhaa nyingi za kubuni nguo mbalimbali ofisini kwake.

Baada ya kuwaza kwa muda mrefu ndani ya ofisi, alitoka nje na kurudi baada ya kutuliza akilila na wakati akirudi aliuona ungo kupitia dirisha uliokua umetundikwa ukutani kama pambo la ofisia mbapo aliamua kuuchukua na kukaa nao huku kichwa kikiendelea kuwaza na kuwazua ni wazo gani ataonyesha kwenye onesho lililokua mbeleyake.

Baada ya kuwaza kwa masaa kadhaa wazo lilimjia na kutaka kutoboa ungo aliokua nao  kwakiasi cha kuweza kuvaa shingoni ambapo alifanya hivyo na kupata ladha ya mapambo ya shingoni ya kimasaii la katika mwonekano wa ungo na ndipo alipoanza kufikiria mikato mingine ambayo   ungo unaweza kuingia na kudhihirisha ubunifu wa ungo kama vazi.

Baada ya kupata yote hayo Makeke alichukua daftari na kuanza kuchora kila alichokua amekiwaza kwa ufanisi zaidi kufanyia kazi kwa muda aliokua nao hali iliyofanya ubunifu wa ungo kutumika kwamara ya kwanza katikatamasha la I AM MAKEKE mpaka hivisasa.

Mikato ya Lupahero

MAKEKE INTERNATIONAL 
imelenga zaidi kujenga dhana ya ushujaa na asili ya kiafrika ili kujenga mazingira ya kuweza kujiamini na kujua kuwa wewe ni bora zaidi kutoka na jinsi ulivyo kama mwafrika na shujaa akiwa katika kila jambo.
Follow us on Facebook  @makeke international Instagram@makekeinternational  
On Apr 6, 2018 8:11 PM, "Mr. Lulela" wrote:

LUPAHERO
Baadayauzoefumkubwakatikamatumiziyamapishijikoni, ungoumejizoleaumaarufumkubwabaadayakuingizwarasmikatikatasniayasanaahususanikatikaubunifuwamavazinakupewajina la LUPAHERO naJocktanMakeke.

Maanaya LUPAHERO

Ubunifu huu wa mavazi umepewa jina la LUPAHERO ambalo nimchanganyiko wamajina mawili ambayo ni LUPAPIKE, neno la kinyakyusa lenye maana ya ungo na neno la pilini LUHELO, ambalo ni neno la kihehe lenye maana ya ungo.

Muunganikowamaneno haya mawili yamelenga kuletadhana yaushujaa kutokan ana ladha ya mavazi hayo kuwa na dhima hiyo, huku neno Luhelo likitamkwa herufi zamwisho kama Hero, herufi L ikibadilishwa kuwa R ilikupataneno hero la kingereza lenyemaana ya shujaa nakukamilisha maana halisi yaubunifu huo kuwashujaa wa ungo.  

Jinsiwazolilivyopatikana.

Katika maandalizi yaonyesho la kwanza kufanywa chini ya MAKEKE INTERNATIONAL lililofahamika kama I AM MAKEKE ndipo wazo hili la lupahero lilipozaliwa. Kwamujibuwa MAKEKE INTERNATIONAL ilimchukua muda mrefu kupata wazo la kufanya katika onyesho hilo licha ya kua na bidhaa nyingi za kubuni nguo mbalimbali ofisini kwake.

Baada ya kuwaza kwa muda mrefu ndani ya ofisi alitoka nje na kurudi baada ya kutuliza akilila na wakati akirudia aliuona ungo kupitia dirisha uliokua umetundikwa ukutani kamapambo la ofisia mbapo aliamua kuuchukua na kukaa nao huku kichwa kikiendelea kuwaza na kuwazua ni wazo gani ataonyesha kwenye onesho lililokua mbeleyake.

Baada ya kuwaza kwa masaa kadhaa wazo lilimjia na kutaka kutoboa ungo aliokua nao  kwakiasi cha kuweza kuvaa shingoni ambapo alifanya hivyo na kupata ladha ya mapambo ya shingoni ya kimasaii la katika mwonekano wa ungo na ndipo alipoanza kufikiria mikato mingine ambayo   ungo unaweza kuingia na kudhihirisha ubunifu wa ungo kama vazi.

Baada ya kupata yote hayo Makeke alichukua daftari na kuanza kuchora kilaalichokua amekiwaza kwa ufanisi zaidi kufanyia kazi kwa muda aliokua nao hali iliyofanya ubunifu wa ungo kutumika kwamara ya kwanza katikatamasha la I AM MAKEKE mpaka hivisasa.

Mikato ya Lupahero


MAKEKE INTERNATIONAL 
imelenga zaidi kujenga dhana ya ushujaa na asili ya kiafrika ili kujenga mazingira ya kuweza kujiamini na kujua kuwa wewe ni bora zaidi kutoka na jinsi ulivyo kama mwafrika na shuja akiwa katika kila jambo.
Follow us on Facebook  @makeke international Instagram@makekeinternational