Showing posts with label BIASHARA. Show all posts
Showing posts with label BIASHARA. Show all posts

Friday, August 19, 2022

NSSF yajipanga kukusanya Trioni 7.3 katika Mwaka wa fedha 2022/2023

Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umepanga kukusanya kiasi Cha shilingi trioni 7.3 katika Mwaka wa fedha 2022 / 2023 Kutoka katika vyanzo vyake mbalimbali.

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Bw. Masha Mshomba akiongea na Waandishi wa habari mapema leo jijini Dar es salaam.

Kauli hiyo imetolewa leo Agosti, 19 jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa huo Bw. Masha Mshomba, alipokua akizungumza na waandishi wa habari, akitoa Taarifa ya Utendaji wa Mfuko pamoja na Vipaumbele vya Mfuko kwa mwaka wa Fedha  2022/23.

Amesema kuwa, ukuaji huo ni mkubwa tofauti na miaka miwili ya nyuma iliyopita ambapo thamani ya Mfuko ilikuwa ni Shilingi Trilioni 4.3 na kuwa ukuaji huo umechangiwa na ongezeko la makusanyo ya michango.

"Tumepata mafanikio makubwa katika suala zima la ukuaji wa Mfuko na hii imesababishwa na sababu kadhaa ikiwemo kuweka misingi imara na madhubuti ya ukusanyaji wa mapato" amesema Mshomba.

Ameongeza kuwa, katika mwaka wa fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2022, Mfuko ulikusanya zaidi ya Shilingi Trilioni 1.42 kwamba makusanyo hayo ni zaidi ya hata bajeti ambayo walijipangia iliyokuwa Shilingi Trilioni 1.38, ambapo pia Mfuko umeboreshaji sana udhibiti wa matumizi jambo ambalo limechangia ukuaji wa NSSF.

Amesema kuwa, mafanikio mengine yaliyopatikana, ni pamoja na uboreshaji wa huduma hasa kwa kutumia mifumo mbalimai ya TEHAMA ambapo sasa mwanachama na wadau wanaweza kupata huduma popote walipo bila ya kufika katika ofisi za NSSF kwa kutumia mifumo ya waajiri na wanachama yaani Employer Potal na Member Potal.

Mshomba alisema Mfuko pia unapata matokeo mazuri sana katika Uwekezaji hasa ukizingatia kuwa wanawekeza katika maeneo salama ambapo katika kipindi cha miaka miwili uwekezaji umeleta mapato makubwa.

"Ilikuwa haijafikiwa NSSF kuweza kupata mapato ya mwaka zaidi ya Shilingi bilioni 500 lakini katika mwaka huu wa fedha umepata zaidi ya Shilingi bilioni 600,matokeo haya ya uwekezaji yametokana na Mfuko kujikita zaidi katika uwekezaji kwenye maeneo ambayo yanaleta faida kwa Mfuko na kuhakikisha wanaudhibiti wa fedha"amesema Mshomba.

Hata hivyo, amesema chachu kubwa ya mafanikio ya NSSF imechagizwa na kasi ya utendaji wa Rais Samia Suluhu Hassan kwa sababu amekuwa chachu ya ongezeko kubwa la wawekezaji hapa nchini hususan katika sekta binafsi kutokana na kufungua fursa za uwekezaji.

Kuhusu waajiri kutowasilisha michango alisema wameweka mikakati mbalimbali kwa kushirikiana na taasisi nyingine za Serikali ili kupata orodha kamili ya waajiri ambao watawafikia na kufuatilia michango ya wanachama.

Mshomba aliwahamasisha Watanzania wote kushiriki katika zoezi zima la Sensa ya Watu na Makazi ifikapo tarehe 23 Agosti, 2022 ili waweze kuhesabiwa.

Wednesday, August 17, 2022

Watanzania wahamasishwa kuchangamkia fursa ya Uwekezaji na

Na Vicent Macha, Dar es salaam

Kituo Cha Uwekezaji Tanzania ( TIC) imewaomba Watanzania ambao wana nia ya kufanya Uwekezaji katika sekta mbalimbali, wachangamkie  fursa hizo nasio kuwachia wawekezaji kutoka mataifa mengine  kuja kuwekeza hapa nchini.
Kaimu Mkurugenzi wa Kituo Cha Uwekezaji Tanzania ( TIC) Jonh Mnali.

Rai hiyo imetolewe na Kaimu Mkurugenzi wa Kituo hicho Jonh Mnali wakati akizungumza na  Waandishi wa habari Kuhusu Mafanikio ya TIC katika kipindi Cha Mwaka 2021/ 2022,ambapo amebainisha kuwa watananzani bado hawajitokezi kuwekeza katika fursa  mbalimbali za Uwekezaji zilizopo.

" Naomba kutoa wito kwa watanzania wajitokeze kuchangamkia fursa za Uwekezaji katika maeneo yao,waondokane na dhana ya kufikiria kwamba Uwekezaji unawahusu watu kutoka nje ya nchi pekee,bali watambue uwekezaji unawahusu wawekezaji wa ndani na nje ya nchi" amesisitiza Mnali

Amendelea kusema kuwa TIC imefanikisha Uwekezaji kwa kufanya maboresho ya kituo Cha utoaji wa huduma za mahali pamoja " One Stop Facilitation Centre ya TIC" nakwamba taasisi zipatazo 12 za  serikali kwa sasa zinatoa huduma katika kituo cha mahali pamoja ambapo taasisi hizo ni Wizara ya Kazi,Wizara ya Ardhi,Uhamiaji,NIDA,NEMC,TRA,BRELA,TBS,TMDA,OSHA, TANESCO pamoja na TIC wenyewe.

Amesema kuwa TIC inaendelea kuhamasisha uwekezaji wa ndani na nje kwa kushirikiana na ofisi za kibalozi na ofisi za wakuu wa Mikoa, ambapo TIC inaendelea kupokea wawekezaji wenye nia ya kuwekeza nchini,hatua hiyo ni kutokana na serikali  kuendelea kuboresha mazingira ya Uwekezaji na Ujenzi wa Miundombinu wezeshi kama vile barabara,reli,bandari,viwanja vya ndege na umeme.

" Katika kipindi cha kuanzia Juni 2021 hadi 2022 uhamasishaji uwekezaji wa nje umeendelea kufanyika kupitia makongamano ya uwekezaji yaliyofanyika Qatar,Doha na ushiriki wa TIC kwenye kongamano na maonesho haya yameleta matokeo chanya ambapo wawekezaji mbalimbali walifika nchini kukutana na wataalamu wa sekta ambazo wanahitaji zaidi kuwekeza" amesema Mnali.

Kaimu  Mkurugenzi Mtendaji huyo wa TIC ameongeza kuwa wawekezaji wa ndani wameendelea kutembelea kituo cha Uwekezaji kutafuta fursa ,huku TIC pia imeendelea kusaidia wawekezaji hao kuratibu uwasilishwaji wa miradi ya watanzania katika majukwa mbalimbali yanayohusu uwekezaj.

Hata hivyo amefafanua kwamba Serikali imechukua hatua mbalimbali kuhakikisha inarahisisha utoaji huduma kwa kuondoa urasmu ,kutumia teknolojia ya mawasiliano ,na kuweka vigezo vinavyotumika kutoa huduma Kama vile cheti cha uwekezaji ambacho kimefanya uboreshaji ya utendaji kazi wa ndani,mtirirko was nyaraka na mafaili,utoaji maamuzi wenye tija,pamoja na kuweka vigezo na viwango vya utoaji huduma kwa wawekezaji.
 
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TIC Jonh Mnali, amesema kipindi cha mwezi Juni 2021 hadi 2022 jumla ya miradi 274 imesajiliwa ikilinganishwa na miradi 234 iliyosajiliwa katika kipindi hicho Mwaka 2020/ 2021 ambayo ni sawa na ongezeko la asilimia 14.6 ,miradi iliyosajiliwa katika kipindi hicho inatarajiwa kuzalisha ajira 43,925 ukilinganisha na ajira 36,470 zilizoripotiwa kipindi hicho mwaka 2020/ 2021.

Tuesday, August 16, 2022

TRA Kukusanya Shilingi Trilioni 23.65, Mwaka wa fedha 2022/2023

 

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Richard Kayombo akizungumza na waandishi wa habari Leo kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo jijini Dar es Salaam kuhusu mkakati wa makusanyo ya Kodi mwaka 2022/23.

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Richard Kayombo, amesema mamlaka hiyo kwa Mwaka wa Fedha wa 2022/2023, inatarajia kukusanya Shilingi Trilioni 23.65, ikiwa ni sehemu ya bajeti kuu ya Serikali ya Shilingi Trilioni 41.48, ambapo kwa mwaka wa fedha uliopita wa 2021/2022, walikusanya kiasi cha shilingi Trilioni 22.99.

Bw. Kayombo amesema kufuatia ongezeko la makadirio ya makusanyo hayo, TRA inaendelea kutoa elimu ya ulipaji kodi kwa wafanyakazi na wafanyabiashara, ya kuhusu sheria mbalimbali za kodi, tozo na ada zilizofanyiwa marekebisho ili kuhakikisha wanakuwa na uelewa sawa na kurahisisha ukusanyaji na ulipaji kodi kwa hiari na kutimiza majukumu na malengo yaliyowekwa katika utekelezaji wa bajeti ya mwaka huu wa fedha.

Ameyasema hayo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam, kuhusu utekelezaji wa Bajeti ya Serikali ya mwaka wa fedha 2022/2023 ambapo amewataka watanzania kulipa kodi inavyostahili ili kujenga uchumi wa nchi.

*“Katika mwaka wa Fedha 2022/2023 tumeanza kwa kasi ya kuelimisha watumishi wetu na wafanyabiashara kote nchini juu ya mabadiliko mbalimbali ya sheria mbalimbali za kodi, tozo na ada zinazosimamiwa na TRA pamoja na taratibu za ukusanyaji na usimamiaji wa mapato ya Serikali.”* Amesema Bw. Kayombo.

Aidha amebainisha kuwa, marekebisho na mabadiliko ya sheria za kodi yamefanyika kwa lengo la kuongeza kasi ya kufufua uchumi na kuimarisha sekta za uzalishaji kwa ajili ya kuboresha maisha ya wananchi, ambapo miongoni mwa mabadiliko ni pamoja na sheria ya usimamizi wa kodi ambayo inamtaka kila mwananchi mwenye Namba ya Kitambulisho cha Taifa (NIDA) kupata Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN).

“Katika mabadiliko ya sheria ya usimamizi wa kodi, Sheria ya sasa inamtaka kila Mwananchi mwenye Namba ya Kitambulisho cha Taifa (NIDA) kusajiliwa na kupata Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN) ili kumwezesha katika shughuli zake za kila siku”.* Amesema Bw. Kayombo.

Amesema katika mwaka wa fedha uliopita wa 2021/2022, Mamlaka hiyo ilifanikiwa kutatua changamoto za walipakodi, kuweka mazingira mazuri ya kulipa kodi, kuongeza kasi ya kusajili walipakodi wapya, kuwekeza kwenye TEHAMA na kutoa elimu na kuhamasisha

Ripoti ya ya wafanyabishara wa Mipakani yazinduliwa leo jijini Dar es salaam.

Liberty sparks ni Shirika lisilo la Kiserikali, lilojikita katika elimu na tafiti, linalotekeleza mradi wa urahisi wa kufanya biashara nchini Tanzania ambao unafadhiliwa na taasisi ya Atlas Network”.

Mradi huu unategemea kuleta maboresho katika mazingira ya biashara kwa kutazama uboreshaji viashiria vya kiuchumi vinavyo tolewa na riport mbalimbali ikiwemo Ripoti ya Benki kuu ya dunia mwaka 2020. 

Mradi huu chini ya kampeni ya Ujirani mwema ,ambapo hapa tuna angaliautaratibu, muda na gharama katika utumaji na uingizaji wa bidhaa mipakani kwa kuzingatia muda,taratibu na gharama zilizowekwa kisheria.

Kama think tank, tumegundua sehemu ya biashara za mipakani kwa sasa Tanzania imekuwa haifanyi vizuri sana ukilinganisha na nchi nyingine zilizopo chini ya Jangwa la Sahara kama Mauritius, Rwanda, Kenya, Botswana, Burundi na nchi nyinginezo katika urahisi wa kufanya biashara.

Ingawa Tanzania ilipanda kwa ngazi tatu kwenye ripoti ya benki kuu ya dunia mwaka 2019 -2020 bado kuna huitaji mkubwa wa kuhakikisha tunafanya vizuri zaidi, hili litatusaidia kutangaza na kuvutia wawekezaji nchini na kuwezesha vijana wetu kujiajiri wanapomaliza vyuo vikuu.

Naibu waziri wa Uwekezaji, Biashara na Viwanda Exaud Kigahe akizungumza wakati wa uzinduzi wa ripoti ya Wafanyabisahara wa Mipakani Mapema leo jijini Dar es salaam.

Liberty sparks inatambua mchango mkubwa wa serikali wa kuboresha mazingira rahisi na rafiki ya ufanyaji biashara pamoja na kutambua mchango mkubwa wa wadau katika kuchochea maendeleo ya nchi,na kutoa nafasi ya kufanya tathmini ya vipaumbele vya sera kwa kulinganisha na nchi na chumi zilizofanikiwa duniani kwa kuwa na mazingira bora ya ufanyaji biashara za mipakani na ukuaji wa uchumi katika kupambana na umaskini.

Katika kampeni hii tumefanikiwa kufanya tafiti ilayofanywa na Daktari Sauti Magai kutoka (College of Business) chuo kikuu cha Dar es Salaam. Tafiti hii inalenga kuboresha biashara za mipaka kama nilivyosema awali kwa kuzingatia taratibu,muda na gharama.

Sasa ili kufikia malengo hayo, tumeita wadau kutoka sekta binafsi pamoja na serikali na kuunda kikosi kazi kilichotoa mapendekezo ya pamoja kwa kuzingatia utendaji na uwakilishwaji wa moja kwa moja. 

Ni mategemeo yetu kupitia ripoti hii iliyotolewa leo na mgeni rasmi kuwa Mh Exaud Kigahe yataumika katika kufanya maboresho ya kisera na kuweka mazingira bora na rafiki yaufanyaji biashara Tanzania.

Tunaamini kwamba kila mtanzania akipata nafasi na kuweza kufanya biashara kwa urahisi, tutaweza kabisa kupunguza tatizo la umasikini na ajira kwenye kaya zetu kwa sehemu kubwa.

Hili litasaidia kuchochea maendeleo ya jumla na kuondokana na utegemezi. Hatua hii ya kuwaleta serikali na sekta binafsi kwa pamoja itasaidia kutoa mapendekezo yenye mchango chanya kwenye mpango wa muda mrefu wa Tanzania (TDV 2025), Mpango wa maendeleo wa miaka mitano (2021/2022 - 2025/2026) na maendeleo endelevu ya Dunia 2030.

Wadau walioshiriki leo ni kutoka serikalini na sekta binafsi ni kama wafuatao; 

Ni matengemeo yetu Taasisi za kiserikali , waandishi wa habari, wabunge, wanazuoni na wadau wengieneo wa maendeleo watatuunga mkono katika kampeni hii ya kuboresha mazingira ya biashara Tanzania.

Matokeo ya mda mrefu na mfupi ya mradi huu ni kuona mazingira ya biashara yakichochea maendeleo ya nchi na watu kwa pamoja.

Baadhi ya Wajumbe wakufuatilia matukio yanayoendelea katika Uzinduzi wa ripoti ya Wafanyabiashara wa Mipakani.

Tuesday, July 12, 2022

TIC YATOA TATHIMINI YA MAONESHO YA SABASABA 2022, YATANGAZA MAFANIKIO YA MFUMO MPYA WA ‘ELECTONICS INVESTIMENT WINDOW’

Na: Hughes Dugilo, DAR ES SALAAM.
Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) John Mnali ametoa rai kwa wawekezeji wote wa ndani na nje ya nchi kutumia fursa ya Mfumo mpya wa Kielectonic kupata huduma mbalimbali ikiwemo kuomba Vibali na Leseni za Biashara ikiwemo ya uwekezaji na kwamba mfumo huo umelenga kuwawezesha wawekejazi kupata huduma zote kwa wakati mmoja.
 
Mnali ameyasema hayo Julai 12,2022 alipokuwa akitoa tathimini ya maonesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba yanayotarajiwa kufungwa rasmi Julai 13,2022 katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam ambao amesema kuwa Mfumo huo ujulikanao kama ‘TANZANIA ELECTONICS INVESTIMENT WINDOW’ umewezesha kuunganisha taasisi 6 kwa awamu ya kwanza na kwamba baadae wanatarajia kuongeza taasisi nyingine 11 zitakazofanya kazi kwa pamoja.
 
Ameeleza kuwa katika mfumo huo mwekezaji anaweza kuleta maombi yake kwa njia ya mtandao au kutoa taarifa ya kuhama kutoka eneo moja kwenda eneo jingine, au kurekebisha cheti chake na kwamba kwa kupitia mfumo kunamfanya  mwekezaji kuondokana na usumbufu wa kutembea katika kila ofisi kufuata huduma.
 
“Huduma ziko kwa wawekezaji wote wa ndani na wa nje hivyo itakuwa vizuri kutumia fursa hii kuweza kuandikisha miradi yao, na kufanya maombi yao katika maeneo mambalimbali yanayohitaji huduma katika taasisi husika” 
 
“Kituo cha Uwekezaji tunafahamu kuna miradi mingi sana ambayo inafanyika na wawekezaji wa ndani ambayo haina cheti cha uwekezaji ukizingatia hali ya miradi yao jinsi ilivyo na ukubwa wake inastahili kupata cheti cha uwekezaji.
 
“Elimu hii tuliyoitoa hapa kwa siku zote hizi za maonesho ni vizuri sasa wananchi wanaotaka kuleta maombi mbalimbali watumie mfumo huu kuleta maombi yao, hii itawarahisishia sana kupata huduma kwa haraka” amesema 
Ameongeza kuwa ushiriki wao katika maonesho ya mwaka huu umekuwa wa mafanikio makubwa kutokana na kuwa na maeneo matatu waliyoshiriki ikiwemo Kliniki ya Biashara, uwepo wa eneo maalum la kuonesha utendaji kazi wa mfumo mpya wa ‘ELECTONICS INVESTIMENT WINDOW’, pamoja na ushiriki wao wa jumla ndani ya Banda la Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara lililojumuisha taasisi zote zinazofanyakazi chini ya Wizara hiyo.
Amewataka wananchi wote kutembelea katika ofisi zao za Kanda zilizowekwa kwaajili  ya kutatua changamoto mbalimbali za wawekekezaji waliopo nje ya Jiji la Dar es Salaam, ambapo amezitaja Ofisi hizo kuwa ni pamoja na Kanda ya  Kaskazini,  Nyanda za juu Kusini, Kanda ya Kati na Kanda ya Ziwa.

MTENDAJI MKUU BRELA AKABIDHI VYETI VYA USAJILI KWA WAFANYABIASHARA SABASABA

 

Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Usajili wa Majina ya Biashara na Leseni (BRELA) Bw.Godfrey Nyaisa kulia na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) Bi. Latifa Khamis wakimkabidhi Cheti cha Usajili wa Jina la Biashara Bw.Hussein Mustaali Lukmanjee jana kwenye maonesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa kwenye viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.

Afisa MtendajiMkuu wa Mamlaka ya Usajili wa Majina ya Biashara na Leseni (BRELA) Bw.Godfrey Nyaisa akimkabidhi Cheti cha Usajili wa Jina la Biashara Bi. Mariam Kihelelo jana kwenye maonesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa kwenye viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Usajili wa Majina ya Biashara na Leseni (BRELA) Bw.Godfrey Nyaisa akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa taasisi hiyo kwenye maonesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa kwenye viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Usajili wa Majina ya Biashara na Leseni (BRELA) Bw.Godfrey Nyaisa akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa taasisi hiyo kwenye maonesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa kwenye viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.

Wednesday, June 29, 2022

Shirika la Posta Tanzania limesaini Mkataba wa kusafirisha Sampuli za Kibailojia na kampuni ya TUTUME.

Na. Vicent Macha Dsm

Shirika la posta nchini pamoja na Kampuni ya kusafirisha mizigo ya TUTUME wamepongezwa kwa ubunifu wa kushirikiana kuhakikisha watanzania hawakosi huduma muhimu za afya.

Pongezi hizo zimatolewa na Waziri wa Habari, Mawasialiano na Teknolojia ya Habari Mh. Nape Moses Nauye alipoalikwa kushuhudia utiaji saini wa mkataba wa usafirishaji wa sampuli za kibaiolojia baina ya shirika hilo pamoja na kampuni hiyo.

Aidha amesema kuwa kama lilivyo lengo la serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan la kusogeza huduma mbalimbali karibu na wananchi hivyo mikataba hiyo itasaidia sana kupanua huduma hizo hasa katika upende wa Afya.

Ameongeza kuwa licha ya kuwa mkataba huo unalenga sekta lakini angalieni pia katika maeneo mengine ambayo mnaweza kushirikiana na mkiangalia wote mnafanya kazi ya aina moja hivyo mkiongeza mashirikiano katika vitu vingi mtaweza kuwasaidia watanzania kwa sehemu kubwa sana.

Amemalizia kwa kuwataka TUTUME, Shirika la Posta pamoja na wote wanaotoa huduma za kusafirisha bidhaa kuweza kuutumia vizuri mfumo wa anuwani za makazi ili kurahisisha ufanyaji wao wa kazi, na pia amewaomba Wizara ya Afya ikiwezekana kuwafuata watu majumbani kuchukua sampuli na kutuma kwa mashirika haya na baadae kuwarudishia pia majibu kupitia wasafirishaji hao hao.

kwa upande wake Posta Masta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania (TPC) Macrice Mbodo amesema kuwa mkataba huo waliyosaini na Kampuni ya TUTUME ni wa kiuwakala wa kusambaza Sampuli mbalimbali za Mahabara

Ameongeza kuwa majukumu ya TUTUME, itakuwa ni kuchukua Sampuli kutoka katika ngazi ya kwanza ya Mahabara na kupeleka ngazi ya pili ya Mahabara na wao Shirika la Posta kazi yao itakuwa ni kutoa ngazi ya pili na kupeleka katika Mahabara za uchunguzi na baadae muhusika kupelekewa majibu yake.

Ameendelea kusisitiza kuwa Shirika la Posta limekuwa likitoa huduma za kusafirisha mizigo kwa njia mbili yaani njia ya haraka pamoja na kawaida, Na kuongeza kuwa mpaka sasa shirika hilo limetoa ajira ya uwakala kwa vijana wa boda boda zaidi ya 450.

Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya Tutume, Misana Manyama amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuweka mazingira wezeshi kwa sekta binafsi zinapohitaji kushirikiana na idara za Serikali ili kuweza kuleta maendeleo katika nchi yetu. 

Ameongeza kwa kusema kuwa waoa kama TUTUME, wataifanya kazi hiyo kwa uadilifu na weledi mkubwa sana, na kutii masharti yale yote yaliyopo kwenye mkataba huo na kwamba wao wanauzoefu wa kutosha katika kazi hiyo kwani walikwisha ifanya hapo nyuma na wanaendelea kuifanya na kuongeza kuwa mpaka sasa wanavijana wa boda boda zaidi ya 1450 nchi nzima.

HABARI PICHA.
Waziri wa Habari, Mawasialiano na Teknolojia ya Habari Mh. Nape Moses Nauye katika zoezi la kusaini mkataba kati ya shirika la Posta na Kampuni ya TUTUME.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Jim Yonaz akitoa neno katika zoezi la uwekaji saini mkataba wa kusafirisha Sampuli za kibaiolojia.
Posta Masta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania (TPC) Macrice Mbodo akiongea katika zoezi la kusaini mkataba kati ya shirika la Posta na Kampuni ya TUTUME.
Mkurugenzi wa Kampuni ya TUTUME, Misana Manyama akiongea namna watakavyoshirikiana na Shirika la Posta nchini kuweza kusafirisha sampuli za kibaiolojia.
Zoezi la utiaji wa saini likiendelea kati ya Shirika la Posta nchini na Kampuni ya TUTUME, zoezi lililofanyika mapema jana Mkoani Dar es salaam.






Tuesday, April 24, 2018

Zantel yazindua Ofa babu kubwa ya mfungo wa Ramadhan

Meneja Uhusiano wa Zantel Rukia Mtingwa akizungumza wakati wa uzinduzi wa Ofa maalum ya mfungo wa Ramadhani jijini Dar es salaam, Ofa hiyo mpya itawapa wateja uhuru zaidi wa kuwasiliana pamoja na kuwapa taarifa muhimu kipindi cha mfungo kama nukuu za Quran pamoja na jumbe za kuwakumbusha muda wa swala kufuturu na mwisho wa kula daku.

Kampuni ya Mawasiliano ya Zantel April 23, 2020 imezindua ofa maalumu ya mwezi mtukufu wa Ramadhan kwa wateja wake ili kuwawezesha kufanya mawasiliano kwa gharama nafuu pamoja na kupata taarifa mbalimbali zenye kujenga imani zao katika mwezi huu mtukufu.

Ofa hiyo inawapa wateja uhuru wa kuwasiliana zaidi pamoja na kupata taarifa muhimu kama vile nukuu mbalimbali za Koran takatifu pamoja na jumbe za kuwakumbusha muda wa swala na ujumbe wa sauti utakaoingia kwenye simu zao
kama simu nyakati za iftar na nyakati za daku.

Akizindua ofa hiyo mjini Zanzibar, Mkuu wa Zantel Zanzibar Mohammed Mussa alisema ofa hiyo itawasaidia waumini wa dini ya kiislamu kuimarisha zaidi mahusiano baina ya ndugu, jamaa na marafiki katika kipindi hiki cha mfungo.

“Zantel inapenda kuwatakia waislamu wote mfungo mwema wa mwezi mtukufu wa Ramadhan. Tunatambua mwezi huu ni muda muafaka wa kujenga mahusiano mazuri na ndugu, jamaa na marafiki hivyo ofa hii itahakikisha kwamba wateja
wetu wanawasiliana bila mipaka na pia kuwapa taarifa zitakazosaidia kujiimarisha kiimani ili kufanikisha funga zao,” alisema Mussa.

Naye, Meneja bidhaa na huduma wa Zantel, Aneth Muga alisema ofa hiyo itawazawadia wateja watakaojiunga na vifurushi vilivyoboreshwa zaidi vya siku,wiki na mwezi ambapo mbali na muda wa maongezi watajipatia nukuu za Koran takatifu pamoja na jumbe za kuwakumbusha muda wa swala tano.

“Tumeboresha zaidi vifurushi vyetu ili kuwapa wateja sababu zaidi za kuwasiliana msimu huu.Kwa wateja watakaojiunga kifurushi cha siku kwa Shilingi 1,000/- watajipatia dakika 150, SMS 100 pamoja na nukuu moja ya Koran, jumbe tano za kukumbusha muda wa swala,” alisema Muga.

Vilevile, kwa kifurushi cha wiki cha Shilingi 2,000 mteja atapata dakika 250, SMS 200 huku kifurushi cha mwezi cha Shilingi 10,000/- atapata dakika 1,250, SMS 500 pamoja na nukuu mbalimbali za maandiko ya Koran takataifu, jumbe za
kuwakumbusha muda wa kufuturu pamoja za kukumbusha muda wa swala. 

Ili kujiunga na ofa hii mteja wa Zantel apige *149*15# na kuchagua namba 1 ambayo ni Ramadhani ofa na atajiunga na kifurushi anachohitaji.

Kuhusu Zantel
Zantel ni Kampuni inyaoongoza kwa utoaji wa huduma za mawasiliano Visiwani Zanzibar kwa miaka mingi hivi sasa ikiongoza kwa ubora miundombinu ya mawasiliano, huduma pamoja na bidhaa.

Huduma ya kifedha ya Ezypesa ni ya kwanza nchini Tanzania kutoa huduma za kibenki za kawaida pamoja na za kiislamu kwa ushirikiano na benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ).

Aidha, Zantel ni kampuni inayoongoza kwa utoaji wa huduma za intaneti nchini Tanzania kupitia uwekezaji kwenye teknolojia ya fibre optic cable ambayo inaiunganisha Tanzania na nchi nyingine za Afrika Mashariki na duniani
umeiwezesha Kampuni hiyo kuleta mapinduzi ya haraka ya kidigitali hapa nchini.

Aidha,Miundombinu hiyo imeiwezesha Zantel kutoa huduma za kimataifa za sauti na data kwa jumla kwa kampuni nyingine na nchi jirani hivyo kuchagiza ukuaji wa teknolojia ya digitali

Kwa Mawasiliano zaidi kuhusu Zantel tembelea tovuti; www.zantel.co.tz
Rukia Mtingwa – Manager Brand and Communication 
Mobile: +255 774 55 9999





Saturday, April 21, 2018

#IdrisnaUber: Kampuni ya Uber imesaini mkataba na Msanii Idris Sultan kuwa Balozi wake nchini Tanzania mwaka 2018










Dar es Salaam, Tarehe 20 Aprili 2018.... Kampuni ya Uber imemtangaza msanii Idris Sultan kuwa balozi wake mpya nchini Tanzania mwaka 2018. Idris anakuwa msanii wa kwanza nchini Tanzania kuwa balozi wa Uber, programu ya usafiri yenye umaarufu mkubwa, nchini Tanzania.
Msanii huyu wa uchekeshaji, muigizaji wa tamthlia, na mtangazaji wa vipindi vya redio ametangazwa rasmi katika hafla ya kukata na shoka iliyokwenda kwa jina la #IdrisnaUber iliyohudhuriwa na wageni wachache na wanahabari wa humu inchini. Shughuli hiyo imefanyika katika mgahawa wa kifahari wa Akemi jijini Dar es Salaam.
Tangu mwanzoni mwa zoezi hili, tulifanya juhudi kubwa kuhakikisha kwamba tunampata balozi mwenye ufuasi mkubwa na atakayeiletea Uber ufanisi nchini Tanzania,amenukuliwa Bi.Elizabeth Njeri, Meneja wa Masoko wa Uber Kanda ya Afrika Mashariki. Idris Sultan ni mcheshi na ni msanii ambaye hafanyi mambo yake kwa mazoea, pia anaheshimika katika tasnia ya uchekeshaji,tamthlia, na utangazaji wa vipindi vya redio. Tuna imani kwamba Idris atailetea Uber tija kubwa kwa sababu ni mzalendo kweli kweli - yeye ni kielelezo cha Utanzania na anawasiliana na mashabiki wake kupitia mitandao ya jamii kila wakati. Hizi ndizo sifa tunazosistiza tunapotaka kuwa na mkataba na mabalozi wa kampuni yetu kwa sababu zinasaidia sana katika kuonesha kwamba tunajali maslahi ya wasafiri na madereva wanaotumia mfumo wetu nchini Tanzania.
Akizungumza kwenye hafla hiyo Bw Alfred Msemo; Meneja Msimamizi wa Uber nchini Tanzania, alisema; “Kampuni ya Uber inajituma kutumia uwezo wake kupitia oparesheni zake kimataifa ili kuwa karibu na wateja wake humu nchini. Mchango wa Idris Sultan katika muziki wa Tanzania unaendana na dhamira yetu ya kujenga kampuni ya kimataifa inayogusa maisha ya madereva na wasafiri wanaotumia mfumo wetu hapa nchini. Tutaendelea kuwahudumia wasafiri wetu sambamba na kutoa fursa za ajira kwa madereva wanaotumia mfumo wetu.
Idris alifurahi sana alipotangazwa kuwa Balozi wa Uber nchini Tanzania; “Nimefurahi sana na ni heshima kubwa kwangu kupata fursa hii adimu ya kushirikiana na Uber,kwa sababu mimi nishabiki mkubwa wa mapinduzi yaliyoletwa katika sekta ya usafiri kupitia kwa mfumo wake kote duniani. Nimefurahi kuona jinsi Uber imepata umaarufu jijini Dar es Salaam, binafsi mara nyingi mimi hutumia usafiri wa uberX nikiwa na marafiki zangu kwenye mitoko yetu ya jioni na sasa wamaleta huduma nyingine ya bajaji; uberPOA ambayo nina hamu sana kuitumia - utaniona hivi karibuni. Uber inaendelea kubadilisha maisha ya maelfu ya madereva jijini Dar es Salaam sambamba na kuwapa wasafiri uhuru wa kuchagua usafiri wanaotaka. Nimefurahi sana kuwa sehemu ya kampuni ambayo inajituma kuleta mabadiliko chanya katika maisha yetu.
Baadaye kwenye hafla hiyo, Idris alipanda jukwaani na kuwatumbuiza mashabiki, wanahabari,na wafanyakazi wa Uber kwa kionjo cha kazi yake ya uchekeshaji. Msanii huyo na mshindi wa zamani wa shindano la Big Brother Africa alivunja mbavu za umati huo kwa vichekesho vyake.  
Tangazo hili linakuja siku chache tangu Uber ilipo tangaza kushirikiana na Tigo kwenye mpango
ambao wateja wa Tigo wanapata bando za bure wanapotumia programu ya Uber. Ushirikiano
huu wa kipekee nchini Tanzania umekuwa na manufaa makubwa kwa wasafiri na madereva
wanaotumia Uber na umechochea wasafiri na madereva zaidi kujiandikisha kutumia programu
ya Uber nchini Tanzania.

Thursday, April 19, 2018

Uber na Tigo zashirikina kama njia ya kuwafikia wateja wao vizuri

Mkurugenzi Mkuu wa Tigo Tanzania, Simon Karikari akipeana mikono na Meneja Mkuu wa Uber Afrika Mashariki, Loic Amado mara baada ya kuingia makubaliano ya kipekee yatayowafaidisha watumiaji wa Tigo wakaotumia huduma za usafiri za  Uber kwa kutumia Uber App bure. Kulia ni Mkurugenzi Mkaazi wa Uber Tanzania, Alfred Msemo na kushoto ni Afisa Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Fedha wa Tigo, Hussein Sayed kwenye hafla iliyofanyika jijini Dar Es Salaam.
uber
Ufanisi katika jambo lolote lenye tija na manufaa ni kitu muhimu sana na sasa huduma ya usafiri wa kukodi unaotolewa na Uber imefungua ukurasa mpya kwa kuamua kufanya kazi na Tigo Tanzania.
Usafiri wa kukodi, Uber umekuwa na umaarufu wake kwa wakazi wa jiji la Dar Es Salaam na hivyo kuwa na mvuto kwa wengi hasa wale ambao hawapendi kupata shida ya kugombania usafiri au kufika sehemu ambayo mtu anakwenda bila nguo yake kuchafuka kwa vumbi/majasho.
Unaweza ukajiuliza nini ambacho kimewaleta Uber na Tigo katika meza moja na kuamua kufanya kazi kwa pamoja? Jibu ni rahisi sana, teknolojia lakini utauliza tena kivipi? Uber anamiliki programu tumishi na ili uweze kuita huduma ya usafiri wa Uber basi itakubidi uwe na kifurushi cha intaneti (MBs).

Watumiaji wote wa app ya Uber na wanaotumia laini ya Tigo hawatatozwa kiasi chochote cha kifurushi cha intaneti wanapokuwa wanatumia programu tumishi ya Uber.



Uber na Tigo
Uber ni moja ya huduma ya usafiri ambapo iwapo safari ya kwenda mahali imeanza na dereva hakuwasha kiyoyozi una haki ya kulalamika kwanini dereva hajawasha “Kileta upepo” ndani ya gari.


Uwezo wa kutumia app ya Uber bila kifurushi chako cha intaneti kutumika ni kwa wote, dereva pamoja na abiria anayetumia laini ya TIgo.

MAkubaliano baina ya Uber na Tigo Tanzania yanaangaziwa kama hatua mojawapo ya watu kuzidi kutumia programu tumishi ya Uber ili kuweza kupata huduma hiyo bila makato ya MBs (bure).

Ofa nyingine kutoka Tigo na Uber zipo mbioni kuja. Ulishawahi kutumia huduma ya usafiri wa Uber kabla na baada ya ofa hii kuwepo? Unazungumziaje makubaliano ya Tigo Tanzania na Uber?

Wednesday, April 18, 2018

Tigo yamwaga zawadi za simu washindi 84 wa katika promosheni ya Tigo Nyaka Nyaka Bonus jijini Dar es Salaam leo

Meneja Mawasiliano wa Tigo Tanzania, Woinde Shisael (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za Tigo jijini Dar es Salaam leo katika hafla ya kukabidhi simu janja aina ya Tecno R6 kwa washindi 52 kutoka Dar es Salaam wa wiki hii katika promosheni ya Tigo Nyaka Nyaka Bonus. Kulia ni Mtaalam wa Usambaji Bidhaa wa Tigo, Baraka Hamza. 





Meneja Mawasiliano wa Tigo Tanzania, Woinde Shisael (kushoto) akikabidhi zawadi ya simu janja aina ya Tecno R6 kwa  Tatu Shomari Kandi (kati) mjasirialimali n amkaazi wa Tabata jijini Dar es Salaam baada ya kuibuka kama mojawapo ya washindi 84 wa wiki hii katika promosheni ya Tigo Nyaka Nyaka Bonus jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mtaalam wa Usambaji Bidhaa wa Tigo, Baraka Hamza. 


Meneja Mawasiliano wa Tigo Tanzania, Woinde Shisael (kushoto) akikabidhi zawadi ya simu janja aina ya Tecno R6 kwa  Mariam Yatela Omari (kati), mhudumu wa saluni katika eneo la Kisarawe, Dar es Salaam baada ya kuibuka kama mojawapo ya washindi 84 wa wiki hii katika promosheni ya Tigo Nyaka Nyaka Bonus iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mtaalam wa Usambaji Bidhaa wa Tigo, Baraka Hamza.

Meneja Mawasiliano wa Tigo Tanzania, Woinde Shisael (kushoto) akikabidhi zawadi ya simu janja aina ya Tecno R6 kwa  Boni Japhet Sanga (kati) mjasirialimali n amkaazi wa Tabata jijini Dar es Salaam baada ya kuibuka kama mojawapo ya washindi 84 wa wiki hii katika promosheni ya Tigo Nyaka Nyaka Bonus jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mtaalam wa Usambaji Bidhaa wa Tigo, Baraka Hamza.  

Tuesday, April 17, 2018

QNET inaleta bidhaa zake za kuboresha maisha nchini Tanzania



·        Dar es salaam inakuwa mwenyeji wa siku 2 za maonyesho ya Absolute Living (Kuishi kikamilifu) ya bidhaa QNET 
·        Watu wote wanakaribishwa kuhudhuria na kuelewa bidaa za QNET, huduma na mtindo wake wa biashara.
Tarehe 13 Machi 2019, Dar es salaam: Kampuni yenye asili ya Asia ya mauzo ya moja kwa moja QNET itaendesha maonyesho ya bidhaa na huduma zake jijini Dar es salaam siku ya tarehe 16 na 17 Machi 2019 katika ukumbi wa Mlimani City  kuanzia saa 4 asubuhi mpaka saa 1 Jioni. 
Maonyesho yenye jina la Absolute Living, (Kuishi Kikamilifu) sambamba na falsafa ya bidhaa za kampuni ya mauzo ya moja kwa moja, huwa yanafanyika kila mwaka katika nchi mbalimbali duniani kote ikiwa na lengo la kuonyesha bidhaa zake na huduma kwenye masoko mapya.  Onyesho hilo pia linakuwa kama jukwaa kwa wateja na wadau wengine wanaotaka kufahamu kuhusu QNET na mtindo wake wa biashara. 
Nadharia ya Absolute Living (Kuishi Kikamilifu) inaakisi juhudi za QNET za kukuza mwenendo wa kujali afya, mtindo wa maisha wenye uwiano sahihi, ikiwa inatilia mkazo katika Afya, Ustawi na Elimu. 
Akizungumza kwenye mkutano na vyombo vya habari Meneja Mkuu wa Kanda wa QNET kwa Kanda ya Kusini mwa Jangwa la Sahara Afrika, Biram Fall alisema kwamba, "Tunatoa aina mbalimbali za bidhaa za kiwango cha juu na huduma kwa wateja wetu kuwasaidia waweze kuishi maisha yenye uwiano sahihi, na pia kutatua tatizo la msingi kama vile elimu, ufahamu, na maendeleo binafsi kupitia program za mafunzo yetu, ambayo yanawasaidia katika safari yao ya kujiajiri mwenyewe.  Kutoka katika kozi za elimu kwa njia ya mtandao kama vile SELI/qLearn, mpaka katika vifurushi vya sikukuu kama vile Tripsavr, mpaka bidhaa za kuongeza nguvu kama vile Bio Disc3, virutubisho kama EDGE, na saa za mkononi kama Bernhard H. Mayer, QNET ina aina mbalimbali za kukidhi mahitaji mbalimbali ya watu.  Katika kitovu cha yote haya, ni hamu yetu ya kutoa fursa ya Kuishi Kikamilifu "Absolute Living”
Zaidi ya watu elfu mbili wanatarajiwa kuhudhuria maonyesho ya siku 2 ambayo yatakuwa na bidhaa za mfano katika onyesho, na kuonyesha namna ya matumizi ya bidhaa na faida zake kwa wateja na watumizji wa mwisho.  Kwa kuongezea, wataalamu wa bidhaa na biashara watakuwepo kwa ajili ya kujibu swali lolote kutoka kwa wageni ili kuelewa vizuri ulimwengu wa QNET.
QNET inaalika watu wote kuhudhuria onyesho hili jijini Dar es salaam na kujifunza kwanza kuhusu bidhaa, huduma na fursa za biashara.
Maonyesho ya Dar es salaam yanafuata mfululizo wa maonyesho kama hayo yaliyofanikiwa nchini Togo, Guinea, Ivory Coast, Senegali, Burkina Faso na Cameroon mwaka jana.
Msafara wa maonyesho utasisimama katika mji wa Kumasi, Ghana, baada ya Dar es salaam kuanzia tarehe 23 mpaka 24 Machi mwaka 2019.