Friday, September 29, 2017

Kituo cha Mabasi Ubungo kuzalisha ajira 20,000


NA CHRISTINA MWAGALA, OFISI YA MEYA WA JIJI

MSTAHIKI Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita amekutana na ugeni kutoka Jiji la Shanghai nchini China na kujadili mambo mbalimbali yamaendeleo jijini hapa ikiwemo suala la uboreshaji wa kituo cha Mabasi Ubungo.

Ugeni huo uliambatana na Meneja Mkuu wa Kampuni ya Linghang Cathy Wang ambayo ndiyo imeingia mkataba na Halmashauri ya jiji kwa ujenzi wa kituo hicho.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa mara baada ya kumalizika kwa mazungumzo hayo, Meya Mwita alisema kuwa ugeni huo umeridhia kuwekeza katika nyanja mbalimbali ikiwemo kituo cha mabasi ubungo.

Alifafanua kuwa jiji la Dar es Salaam linakaribia kunza kwa ujenzi wa mradi mkubwa wa kubadilisha kituo cha mabasi ubungo na kwamba hatua mbalimbli zimeshakamilika ili kupisha mradai huo.

Alisema kuwa mara baada ya kukamilika kwa mradi huo jumla ya watanzania 20,000 watapata ajira jambo ambalo litawezesha kuongeza kipato kwa wananchi na hivyo pia kuwezesha vijana kuondokana kwenye makundi ambayo sio salama.

Alisema kufanikisha kwa mradi huo, utasaidia pia kuongeza mzunguko wa fedha jijini hapa kutokana na kuwepo kwa fursa nyingi za kibiashara.

“ Leo nimekutana na ugeni ambapo kwa kiasi kikubwa mnafahamu ndugu zetu hawa wamekuwa na urafiki mkubwa katika nchini yetu, tumejadiliana mambo mengi ambayo yote ni yakuleta maendeleo katika jiji letu.

“ Lakini kubwa zaidi ni kuhusu ujenzi wa kituo cha mabasi Ubungo, ambapo hivi karibuni tunatarajia kuanza kwa mradi huo, na wananchi pia watajulisha, nitumie fursa hii kuwaeleza wananchi kuwa jiji linafuata utaratibu katika kutekeleza mradi huo” alisema Meya Mwita.

“ Fursa hii ni kubwa ambayo tumeipata, watanzania watapata ajira, mzunguko wa fedha kwenye jiji letu utaongezeka, kama Meya wa jiji hili nimewakaribisha tufanye kazi pamoja, lengo likiwa nikuweka jiji kwenye muonekano mzuri” aliongeza.

Kwaupande wake Meneja Mkuu wa Kampuni ya Linghang Cathy Wang alimpongeza Meya Mwita kutokana na aina ya utendaji wake wa kazi nakuahidi kuonyesha ushirikiano katika utekelezaji wa mradi huo.
Alisema kuwa Meya Mwita ni kiongozi anayefanya kazi kwa bidii na umakini na kwamba kutokana na jitihada hizo za kulijenga jiji , kampuni yao itafanya  kazi na kumuhakikisha kufanya kazi kwa ushirikiano mkubwa.


WATANZANIA WANG'ARA SHINDANO LA MWANDISHI BORA WA SAYANSI NA KILIMO AFRIKA


 Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti ya Uganda na Mjumbe wa Bodi ya ASARECA, Dr. Ambrose Agona (kushoto), akimkabidhi cheti Mwandishi wa Star Tv Dino Mgunda kuwa mshindi wa pili kwa waandishi wa Televisheni kwenye shindano hilo lililofanyika jana nchini Uganda.

 Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti ya Uganda na Mjumbe wa Bodi ya ASARECA, Dr. Ambrose Agona, akimkabidhi cheti Mwandishi wa Tanzania Koleta Makulwa kutoka Radio Free Afrika ambaye alipata tuzo na kuwashinda wenzake ambao walikuwa wanashindana katika eneo la Radio.
 Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti ya Uganda na Mjumbe wa Bodi ya ASARECA, Dr. Ambrose Agona, akimkabidhi cheti Mwandishi wa Tanzania wa gazeti la Guardian, Gerald Kitabu ambae alishinda tuzo ya umahiri wa habari za sayansi katika eneo la magazeti huku akiwaashinda waandishi wengine kutoka nchi zingine saba za Afrika.  
Keki ikikatwa katika hafla hiyo

Na Mwandishi Wetu

Mwandishi wa gazeti la Guardian, Gerald Kitabu ameshinda tuzo ya umahiri wa habari za sayansi katika eneo la magazeti huku akiwaashinda waandishi wengine kutoka nchi zingine saba za Afrika.

Kitabu alikuwa anachuana na waandishi kutoka nchi za Nigeria, Burkina Faso, Ghana, Ethiopia, Kenya, Tanzania na Uganda. Shindano hilo lilifanyika jana katika Hoteli ya Speke Resort Munyonyo iliyoko nje kidogo ya jiji la Kampala.

Kwa ushindi huo, Kitabu ambaye ni mshindi wa jumla wa shindano la Tanzania, alijinyakulia kitita cha dola za marekani 1,500 pamoja na simu aina ya iPhone 7+ yenye thamani za dola za Marekani 1,200. 

Mwandishi mwingine wa Tanzania aliyepata tuzo ni Koleta Makulwa kutoka Radio Free Afrika ambaye aliwashinda waandishi wengine ambao walikuwa wanashindana katika eneo la Radio. ambapo Tanzania ilizidi kung'ara baada ya Mwandishi wa Star Tv Dino Mgunda kuwa mshindi wa pili katika waandishi wa televisheni. 

Koleta aliondoka na kitita cha dola za Marekani  1,500, simu aina ya iPhone 7+ ya thamani ya dola za marekani  1,200 wakati  Dino Mgunda alipata zawadi ya dola za marekani  1,000 na simu ya iPhone7+  ya thamani ya dola za marekani 1,000.

Katika shindano hilo jumla ya waandishi 20 waliwakilisha nchi hizo. waandishi hao ni wale ambao walikuwa washindi katika shindano la nchi mahalia, shindano ambalo lilifanyika mwanzoni mwa wiki hii katika nchi hizo ikiwemo tanzania. 

Shindano hilo liliandaliwa na Jukwaa la wazi la Bioteknolojia za Kilimo (OFAB) ambalo linahamasisha matumizi ya bioteknolojia katika kilimo ili kuwezesha nchi za Afrika ziweze kujitosheleza kwa chakula.

Mshindi wa jumla katika shindano hilo la jana ni  mtangazaji wa kituo cha  TVC, Omolara Afolayan kutoka Nigeria. Washindi waliteuliwa na jopo la majai watano.

MAMIA WAFUNGULIWA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA INJILI JIJINI MWANZA

 Na George Binagi-GB Pazzo
Wakazi wa Jiji la Mwanza wakiwemo waumini wa dini mbalimbali wameendelea kujitokeza kwa wingi kwenye mkutano mkubwa wa injili ulioandaliwa na kanisa la kanisa EAGT Lumala Mpya chini ya Mchungaji Dkt.Daniel Moses Kukola.

Jana mamia ya wananchi walijitokeza kwenye mkutano huo unaofanyika kwenye uwanja wa Sabasaba Ilemela Jijini Mwanza na kukutana na mlipuko mkubwa wa injili kutoka kwa watumishi wa Mungu akiwemo mwinjilisti Rojas Matias kutoka Marekani chini ya huduma ya MORE International Ministry.

Aidha waimbaji Ambwene Mwasongwe, Mbilikimo Watatu, Samwel Lusekelo, Joseph Rwiza, Sam D, Havillah Gospel Singers na wengine wengi wameendelea kukonga nyoyo za wahudhuriaji kwenye mkutano huo.

“Maandalizi ya mkutano huu ni ya kuvutia, tuna majukwaa matatu makubwa, vyombo vya muziki wa injili vizuri na pia tunatoa zawadi mbalimbali ikiwemo vyakula na nguo kwa wanaohudhuria mkutano huu”. Alisema Mchungaji Dkt.Kulola na kuwahimiza watu wote kufika kwenye mkutano huo ili wakutane na nguvu ya Mungu na kufunguliwa.


Mkutano huo ulianza juzi jumatano Septemba 27 na utafikia tamati jumapili Oktoba Mosi, 2017 katika Uwanja wa Sabasaba Ilemela Jijini Mwanza ambapo mamia ya wananchi waliokuwa wakiteswa na majini pamoja na magonjwa mbalimbali wanazidi kufunguliwa, na leo huduma ya maombezi inaanza mapema majira ya saa nne asubuhi na mkutano utaanza saa tisa alasiri hadi saa 12 jioni.
Mwinjilisti Rojas Matias kutoka Marekani akihubiri kwenye mkutano huo
Watumishi mbalimbali wakiendelea kutoa huduma ya maombezi jana ambapo zaidi ya 20 walifunguliwa mapepo huku wengine wengi wakiponywa magonjwa mbalimbali
Mwimbaji wa muziki wa injili Ambwene Mwasongwe kutoka Dar es salaam akihudumu kwenye mkutano ho
Baada ya ibada, kanisa la EAGT Lumala Mpya kwa kushirikiana na wachungaji kutoka Marekani lilitoa zawadi kwa wananchi
Tazama picha zaidi HAPA

KIITEC LAUNCHED SOLAR POWER PLANT AND SOLAR LABORATORY

Excellency Malika Berak, Ambassador of France in Tanzania (C) cuts a ribbon to officiate the launch of Solar Power plant and laboratory at KIITEC in Arusha, others in photo are senior officials from the partners institutions supporting the Institute.
FTE President Fransis Bronchon,(R) briefing invited guests on Solar Project at KITEEK during the launch event at Arusha.
Excellency Malika Berak, Ambassador of France in Tanzania(C) got briefing on project from, Albert Mtana, (R)-Teacher of Electrical and Solar Photovoltaic System (L) is Michel Ramser-VP Strategic Marketing and Sponsorship (ADEI).
Solar panel installed at the centre. The Kilimanjaro International Institute for Telecommunications, Electronics and Computers (KIITEC) has launched 30KW solar power plant and solar laboratory at its training centre in Arusha recently. The Guest of Honour at launch event was Her Excellency Malika Berak, Ambassador of France in Tanzania, also the event brought together the partners that have supported KIITEC for many years. These are: Schneider Electric East Africa, the Schneider Electric Foundation, ADEI, EDF Help and the Foundation for Technical Education (FTE). Speaking during the event, KIITEC Director of studies, Mr. Daniel Mtana, said the opening of this solar power plant speaks to the accomplishment of institute’s vision to become the centre of training excellence for renewable energy, particularly solar photovoltaic systems in East Africa. “Committed to true hands-on experience, KIITEC has now invested heavily in photovoltaic solutions and strives to be recognized as the premier provider of quality technical education in a student-centered community.” General manager at Schneider Electric East Africa, Mr. Mr. Edouard Heripret, said in most sub-Saharan countries, the rate of enrolment in formal secondary technical and vocational training and education (TVET) does not exceed 5%. “Vocational training has always been at the heart of Schneider Electric’s DNA. In East Africa, we have been committed to support technical training since 2009. Kiitec was one of our first training partners and I am pleased today to participate in the inauguration of the solar plant and laboratory, as these new components will allow students to have a full set of competencies to enter the labour market and will support access to energy for everyone.” Mr. Heripret added “At Schneider Electric, we are building sustainable communities through energy knowledge and leadership, thanks to the Schneider Electric Foundation. Its aim is to contribute to the development of people and societies through education, innovation, awareness-raising and vocational training related to energy. It acts, anywhere in the world where the company is present, through its three programmes. KIITEC is an international technical institution, was founded in 2004 by French engineers and has produced some of the most competent technicians in the country. Two NGOs, the Foundation for Technical Education (FTE-Swiss) and Action Development Education International (ADEI-French), support the institution. Schneider Electric assists ADEI in its support of KIITEC. The institute is a pilot centre, with the goal of transposing and exporting its model from Tanzania, to Kenya. It provides its students with the basic skills in telecommunications, electronics, information science, networks and industrial automation systems. The training lasts over two years. It comprises lectures complemented by practical training, project design, and a three-month outplacement in a company. As of today, 350 young people, comprising 90% of the students, have obtained their diploma, the ‘National Technical Award’, which is recognized by the local government, and have all found jobs, mainly in the industrial maintenance sector.

VIDEO: MWINJILISTI KUTOKA MAREKANI AWASHA MOTO JIJINI MWANZA

Mamia ya wananchi wanazidi kujitokeza kwa wingi kwenye mkutano mkubwa wa injili ulioandaliwa na kanisa la kimataifa la EAGT Lumala Mpya kwenye uwanja wa Sabasaba Ilemela Jijini Mwanza. Mhubiri ni  mwinjilist Rojas Matias kutoka Marekani huku mchungaji mwenyeji akiwa ni Dkt.Daniel Moses Kulola.

KIONGOZI MWINGINE WA CUF AFARIKI DUNIA


Kiongozi wa CUF Mheshimiwa Ali Juma Suleiman ambaye alikuwa Kaimu Mwenyekiti wa (CUF) Jimbo la Mto Pepo na Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa (CUF) Wilaya ya Magharibi A. Zanzibar amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya Mnazi Mmoja.
Baadhi ya viongozi wa (CUF) na wanachama pamoja na wananchi wakiwa katika hospitali ya Mnazi Mmoja kufuatilia mwili wa Marehemu Ali Juma Suleyman.

Naibu Katibu Mkuu (CUF) Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrui amethibitisha kutokea kwa kifo hicho na kusema kuwa Mheshimiwa Ali Juma alikuwa amelazwa hospitali ya Mnazi Mmoja kufuatia kuvamiwa nyumbani kwake na kupigwa kisha baadaye kutupwa katika maeneo ya Masingini na makundi ya watu yanayoendesha vurugu Zanzibar.
"Nasikitika kutangaza kifo cha Mheshimiwa Ali Juma Suleiman, Kaimu Mwenyekiti wa CUF Jimbo la Mto Pepo na Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CUF Wilaya ya Magharibi A. Amefariki dunia majira ya saa 4 usiku hapa jana hapa Mnazi Mmoja Hospital baada ya kupigwa vibaya na Mazombi juzi usiku" alisema Naibu Katibu Mkuu CUF Nassor Mazrui

Viongozi wa CUF wamesema kuwa mwili wa marehemu umeshafanyiwa uchunguzi tayari na sasa wamekabidhiwa kwa ajili ya kufanya mazishi ambayo yatafanyika leo katika makaburi ya Mwanakwereke, nje kidogo ya mji wa Unguja.  
Inna Lilahi Wa Inna Ilayhi Rajiuun

SHEIKH JALALA NA ASKOFU BANZA WAMEZINDUA MPANGO WA KUGAWA MAJI NA VIPEPERUSHI BURE

Leo ikiwa ni siku ya tarehe 29 ya mwezi wa 9 sheikh mkuu wa dhehebu la khoja shia Tanzania Hemed Jalala amezindua program ya ugawaji maji na vipeperushi bure iliyofanyika katika msikiti wa kigogo jijini Dar es salaam.
Akiongea na waandishi wa habari mapema leo msikitini hapo Sheikh Jalala amesema kuwa zoezi hili la kugawa maji linaendana sambamba na kumuenzi Imam Hussein ambaye ni mjukuu wa pili wa Mtukufu Mtume Mohamad ambaye alifariki kwa kuwatetea wanadamu bila kuangalia itikadi zao za kidini, kikabila wala maumbile.

Sheikh Jalala aliongezea kwa kusema kuwa imam hussein amekuwa ni alama kwa dunia kwa kukubali yeye kufa ili watu wapate amani pamoja na kutendeana mema ikiwemo kupendana, kuhurumiana kuheshimiana na alithubutu kuyafanya hayo wakati huo ambao mema yalipungua katika dunia na hakukuwepo amani miongoni mwa wanadamu hao na matokeo yake yalikuwa ni ugomvi na chuki ndani ya kizani hicho.
Maulana Sheikh Hemed Jalala akiongea na waandishi wa habari ambao hawapo pichani mara baada ya kuzindua programu ya kugawa maji na vipeperushi bure mapema leo jijini Dar es salaam
Lakini leo hii Imam Hussein anatufundisha watanzania kuwa ni watu wenye huruma, upendo ushirikiano na amani tuliyopewa kama nuru yetu Watanzania, ndiyo maana msikiti huu umeamua kuanzisha program kama hizi ikiwemo kuwatembelea wagonjwa, kujitolea damu kwa hiari, kwenda kuwapa moyo wafungwa pamoja na kuwaona na kuwapa misaada watoto yatima ikiwa ni miongoni mwa njia za kumuenzi Imam huyo aliyejitoa kwa ajiri ya wanadamu.
Askofu Mkuu wa kanisa la Tanzania Outreach Ministries Banza Suleiman akitoa ufafanuzi wa jambo fulani katika uzinduzi wa kugawa maji na vipeperushi bure zoezi lililofanyika mapema leo Masjid Al Ghadiir Kigogo Dar es salaam.
Akiongezea Askofu Mkuu wa kanisa la Tanzania Outreach Ministries Banza Suleiman amesema kuwa kitendo kilichofanywa na msikiti huo ni chema na kinapaswa kuungwa mkono na kila Mtanzania anaependa maendeleo kwani maisha yetu wanadamu yanategemea maji kwa kiasi kikubwa, hivyo ili kumuunga mkono Rais Magufuli kufikia kuwa na uchumi mzuri wa viwanda ni lazima watu wawe na maji ya kutosha ili waweze kufanya kazi ipasavyo.

Askofu huyo aliendelea kwa kusema kuwa mungu anambariki anaetoa hivyo kwa kujitolea huko mungu atawabariki sana na hata serikali itafurahi kwa kuona hata tasisi za kidini zipo kwa dhumuni la kuwajari wananchi wake kwa kuona kitendo kilichofanywa na msikiti huo, lakini pia hata wananchi wataona ni jambo zuri kwani maisha ya mwana damu yanategemea maji hivyo bila maji hakuna maisha.
Mwenyekiti wa Kata ya Kigogo Mbuyuni Bw. Hassan Nguogani akiongea na waandishi wa habari ambao hawapo pichani mapema leo jijini Dar es salaam.
Na mwisho Mwenyekiti wa Mtaa Kigogo Mbuyuni Bw. Hassan Nguogani alimalizia kwa kusema wanaishukuru sana taasisi hiyo ya Shia kwani imechangia maendeleo ya kata hiyo kwa kiasi kikubwa kwani hujitolea mambo mengi sana kama matibabu bure kwa wagonjwa, husaidia watoto yatima katika kata hiyo ujitolea madaftari na vifaa mbalimbali vya shule kwa wanafunzi na huduma nyingine nyingi.

Lakini pia husaidia juhudi za kimaendeleo kama kupanda miti, kufanya usafi maeneo ya kata hiyo na hata kuchangia ujenzi wa vitu mbalimbali katika kata hiyo, hivyo ufanya majukumu mengi ambayo ni ya serikali lakini hujitolea wao na hivyo wakazi wa kigogo hunufaika na nifahari sana kwa uwepo wa msikiti huo mahali hapo.

 

Thursday, September 28, 2017

KUHUSU GARI LA MBOWE,BUNGE LATOA KAULI

PRESS RELEASE GARI LA KUBPRESS RELEASE GARI LA KUB.2

ITEL MOBILE YASHEREHEKEA MAADHIMISHO YA MIAKA 10 KWA KUZINDUA SIMU MPYA ZA KISASA ZAIDI.

IMG_5477Makamu wa Rais wa Itel Mobile Bw.Leslie Ding akizungumza na wadau pamoja na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa kuanzimisha maadhimisho ya Miaka 10 ya Kampuni hiyo.
IMG_5498Balozi wa Itel Mobile,Irene Uwoya akizungumza na wadau pamoja na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa kuanzimisha maadhimisho ya Miaka 10 ya Kampuni hiyo.
………………………………
Kampuni ya Simu ya Itel Mobile imetimiza madhamisho ya miaka 10 tangu kuanzishwa kwake huku ikiendelea kufanya vizuri katika soko la mauzo ya Simu na kuwa kinara kwa ubora wa bidhaa zake barani Afrika na nje ya Afrika.
IMG_5459Miaka 10 iliyopita Itel Mobile ilizindua mpango wa kumwezesha kila mmoja kuwa na simu bora kwa ajili ya mawasiliano ya uhakika,katika kipindi hicho chote tumepitia katika kipindi kigumu katika Nyanja za kiuchumi na kisiasa lakini tumeweza kufanikiwa kutimiza mlongo mmoja kwa uthabiti mkubwa.
Itel Mobile iliingia kwenye soko la Afrika mwaka 2007 na baada ya kuanzishwa kwa timu ya watu wenye ujuzi na moyo wa kufanya kazi na mpaka sasa miaka 10 kampuni hii imekuwa na kuweza kuenea zaidi ya nchi 45 Duniani kote.
IMG_5465
Ndani ya miaka 10 Itel Mobile imekuwa na mabadiliko makubwa chanya ya bidhaa kutokana na kufuatwa matakwa ya wateja wake hivyo imepelekea kupendwa na kuleta mvuto kutokana na kuboreshwa kwa bidhaa hizo kwa ubunifu mkubwa.
”Tumeweza kuongeza idadi ya wateja mara mbili zaidi barani Afrika na pia shukrani zetu za dhati ziende kwa wateja wetu pamoja na mashabiki wote wa Itel na mpaka sasa tumeuza jumla ya simu milioni 100’alisema Makamu Rais
IMG_5480Aidha nguvu kubwa yetu inatokana na bidhaa zetu zilivyo bora pamoja na timu ya wafanyakazi wetu ambao kila mmoja amekuwa akijituma kutokana na nafasi yake na pia ubora na mvuto wa bidhaa unatokana na mapendekezo ya watumiaji wetu na huduma za matengenezo baada ya mauzo na warantii ya miezi 12 kwa bidhaa zetu zote.
IMG_5486Hata hivyo tumekuwa na ushirikiano na mastaa wa nchi za Afrikia kama mabalozi wa kampuni yetu na wamekuwa kiungo muhimu katika kuleta ufahamu na uelewa kuhusu kampuni ya Itel ambapo imekuwa kampuni 3 bora barani Afrika.
Na kwa kuonesha upendo wetu Afrika tumekuwa tukifanya matendo ya ukarimu kwa jamii na kujitolea kutembelea baadhi ya shule na vituo vya watoto yatima kwa ajili ya kusaidia wanafunzi wanaotoka katika mazingira magumu.
Itel Mobile Tanzania kwa kushirikiana na balozi wa kampuni mwaka huu peke mpaka sasa tumewasaidia katika mahitaji muhimu zaidi ya watoto 400 wanaotoka mazingira magumu wakiwemo yatima na tunaendelea kuunga mkono jitahidi za kusaidia jamii.
IMG_5517Tunaposherekea miaka 10 tunatarajia kuleta mabadiliko makubwa zaidi ili kuimarisha bara la Afrika kwa kutoa bidhaa bora za mawasiliano na leo tunazindua simu mpya ambazo ni za kisas zaidi yaani Itel S12 na S32 na zina ubora kutokana na kuwa kila  simu simu ina kamera mbili za mbele pia mwonekano mzuri na kusaidia kuchukua selfie ya kundi ambayo ina uwezo wa kuchukua watu wengi zaidi pia zina Fingerprint ‘alama za vidole’.

MBOWE ANYANG'ANYWA GARI

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema kimesikitishwa na hatua ya uongozi wa Bunge la Tanzania ya kulichukua gari la Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni (KUB), Freeman Mbowe alilokuwa akilitumia kwa shughuli za matibabu ya Tundu Lissu jijini Nairobi.

Chadema imesema Mbowe ambaye ni Mbunge wa Hai, aliamuru gari hilo lipelekwe Nairobi kwa ajili ya kusaidia matibabu ya Lissu ambaye ni mwanasheria mkuu wa chama hicho

Lissu ambaye pia Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), alishambuliwa na kujeruhiwa kwa risasi Septemba 7 akiwa nyumbani kwake Area D mjini Dodoma na yuko Nairobi kwa matibabu.

Mkuu wa Idara ya Uenezi Chadema, Hemed Ali ameeleza hayo leo Alhamisi na kusema kwamba hawana wasiwasi na hatua hiyo kwa kuwa wana marafiki wengi wakiwamo Watanzania waishio nchini humo na Wakenya wenyewe ambao kwa namna moja au nyingine watashirikiana nao.

Akizungumzia suala hilo Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah amedai kuwa hana na taarifa hizo, ndiyo kwanza anazisikia kutoka kwa mwandishi na alimtaka mwandishi amuulize huyo aliyetoa taarifa kama kweli ametumwa na Mbowe.

“Naomba uumulize aliyesema taarifa hizi je ametumwa na Mbowe? Kwa sababu napata shida Mbowe ni kiongozi pale bungeni na ana wasaidizi wake na haya mambo ni ya ndani ndiyo maana nataka kujua huyu aliyetoa taarifa amezungumza kama nani? Alihoji Dk Kashililah.


“Haya mambo yana taratibu zake za kiofisi naomba niishie hapa. Maana tukiendelea nitakuuliza maswali ambayo utashindwa kuyajibu. Pia na utatakakujua mengi ikiwamo hata posho ya dereva wa Mbowe,” amesema.

Mara Paaap! Tigo Fiesta TAMADUNIKA 2017 ndani ya Tabora

Kikundi cha ngoma za utamaduni cha Hekima mkoani Tabora kikionesha umahiri wa kucheza ngoma kwenye maonesho ya kucheza ngoma za utamaduni za Tigo Fiesta Tumekusoma ‘TAMADUNIKA’ kwenye viwanja vya Taasisi(sanamu ya Mwl.Nyerere) Tabora mapema jana.

Kikundi cha ngoma za utamaduni cha Hekima mkoani Tabora kikionesha umahiri wa kucheza ngoma kwenye maonesho ya kucheza ngoma za utamaduni za Tigo Fiesta Tumekusoma ‘TAMADUNIKA’ kwenye viwanja vya Taasisi(sanamu ya Mwl.Nyerere) Tabora mapema jana.

Mshehereshaji  wa Tigo Fiesta ‘TAMADUNIKA’  Mc Kicheko akifanya yake.

Kikundi cha ngoma za utamaduni cha Mapambano mkoani Tabora kikionesha umahiri wa kucheza ngoma kwenye maonesho ya kucheza ngoma za utamaduni za Tigo Fiesta Tumekusoma ‘TAMADUNIKA’ kwenye viwanja vya Taasisi(sanamu ya Mwl.Nyerere) Tabora leo.


Kikundi cha ngoma za utamaduni cha Wayege ya asili ya tambiko la Kimanyema  kikionesha umahiri wa kucheza ngoma kwenye maonesho ya kucheza ngoma za utamaduni za Tigo Fiesta Tumekusoma ‘TAMADUNIKA’ kwenye viwanja vya Taasisi(sanamu ya Mwl.Nyerere) Tabora leo.

Sehemu ya  watazamaji waliojitokeza kwa wingi  kwenye maonesho ya Tigo Fiesta Tamadunika 2017 mkoani Tabora leo.

SEKTA YA MANUNUZI YA MTANDAONI NA CHANGAMOTO ZAKE NCHINI TANZANIA

Na Jumia Travel Tanzania

Miongoni mwa sekta ambazo zimewapatia utajiri mkubwa wafanyabiashara mbalimbali duniani ni pamoja na biashara kwa njia ya mtandao. Leo hii ukiyataja majina ya kampuni kama vile Alibaba au Amazon ni watu wachache wasioyafahamu licha ya kutokuwepo nchini Tanzania. Waasisi wa makampuni hayo wamo kwenye orodha ya watu matajiri duniani, Bw. Jeff Bezos mwasisi wa Amazon ni tajiri nambari 3 huku Jack Ma ambaye ni mwasisi wa Alibaba yeye ni tajiri nambari 23.
Utajiri wa wafanyabiashara hawa sio kama wanamiliki biashara katika nchi mbalimbali bali uwezo wa makampuni yao kuwafikia wateja mahali popote walipo. Kuwafikia wateja hao Jumia Travel ingependa kukufahamisha si kwa njia nyingine bali ni kupitia mtandao wa intaneti. 

WANAHABARI WATEMBELEA MITAMBO YA UZALISHA MAJI YA DAWASCO YA RUVU CHINI NA JUU

Baadhi ya Wanahabari kutoka vyombo mbalimbali wamefanya ziara ya siku moja katika Mitambo ya Uzalishaji Maji ya Ruvu Juu na Ruvu Chini  iliyopo Mlandizi na Bagamoyo mkoani Pwani ,ziara iliyoandaliwa na Shirika la Maji safi na Maji taka Dar es Salamaa (DAWASCO) kwa lengo la kujifunza namna matibabu ya maji yanavyofanyika kuanzia yanapotoka mto Ruvu.
Mbali na kutembelea Mitambo ya uzalishaji maji pia Wanahabari hao wametembelea ofisi za Dawasco mkoa wa Tabata kujionea utendaji kazi kwa watendaji wa Shirika hilo ,kituo cha Tabata. 
Meneja wa Dawasco Tabata, Victoria Masele akiwakaribisha wanahabari ofisi kwake mara baada ya kumtembelea.
Meneja Biashara wa Dawasco Tabata, Jamal Chuma kifafanua jambo kwa wanahabari.
Vifaa vilivyopo katika ofisi za Dawasco Tabata.
Mtambo wa kuzalisha Maji Ruvu Juu.
Maji yakiingia katika mitambo.
Kina cha maji kinavyoonekana.
Meneja 
Meneja wa Mtambo wa Ruvu Juu, Edward Mkilanya akiongea machache na wanahabari.  
Mhandisi wa Mtambo wa Ruvu Chini, Emaculata Msigali akitoa ufafanuzi jinsi unavyofanya kazi.