Showing posts with label HABARI ZA KIJAMII. Show all posts
Showing posts with label HABARI ZA KIJAMII. Show all posts

Wednesday, October 12, 2022

RAIS SAMIA MGENI RASMI KATIKA MJADALA WA KITAIFA WA NISHATI UTAKAOFANYIKA NOVEMBA 1-2, 2022 DAR ES SALAAM

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa Mgeni rasmi katika mjadala wa kitaifa wa utaokuja na suluhu ya namna watanzania watakavyohamasika na matumizi ya Nishati mbadala na kuachana na nishati isiyofaa. 

Mkutano huo utakaofanyika Novemba 1-2, 2022  katika Kituo cha cha Kimataifa cha Mikutano cha Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam utaratibiwa na Wizara ya Nishati.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Oktoba 12, 2022. Waziri wa Nishati Januari Makamba amesema kuwa mkutano huo utawakutanisha wadau mbalimbali kutoka sekta za Afya, Nishati, Mazingira, Jinsia, Usawa watunga sera pamoja na sheria mbalimbali ili kuweza kujadiliana namna gani wanaweza kupunguza au kuondoa kabisa matumizi ya nishati ya isiyo safi na salama. 

Amesema Sera ya Nishati ya 2015 inayosimamiwa na wizara ya nishati inaelekeza Wizara ya Nishati kuchukua hatua za kuwawezesha watanzania kupata nishati safi na salama na kwa gharama wanayoimudu ili kuboresha ustawi wa watanzania kwa kiasi kikubwa. 

Waziri makamba amesema kuwa Mjadala huo utaratibiwa na wizara ya Nishati ili kupata majibu ya kudumu ya kuondokana na matumizi ya nishati ya kupikia ya Mkaa na kuni nchini pamoja na kupata uelewa wa pamoja juu ya suala nishati ya kupika hapa nchini.

Amesema kuwa katika mkutano huo watangazi katika mlengo wa kiuchumi, Kijinsia afya Usawa na mazingira kwa namna ambavyo tunapika hapa nchini kwa kutumia Nishati safi na Salama. 

Waziri Makamba amesema mjadala huo utapelekea kutambua Changamoto za kutumia kuni na Mkaa, athari zilizipo na kuangalia matokeo yake ni nini. 

Amesema Mifumo ya Kisera Sheria, Kikodi, Kifedha na Utawala itawekwa kwaajili ya kupambana na hali ya namna tunavyopika na kuwaondoa watanzania kutumia nishati inaathiri Afya na Maisha. 

Akizungunzia kuhusiana na madhara yanayojitokeza katika jamii juu ya matumizi ya kuni, Mkaa na nishati nyingine zisizo safi na salama Waziri Makamba amesema Vituo vya afya Nchini vimeelemewa na mzigo Mkubwa wa utoaji huduma za afya za mfumo wa upumuaji zinazotokana na namna tunavyopika.

Amesema Watanzania zaidi ya elfu 33 wanafariki dunia kwa mwaka kutokana na kuvuta moshi wa namna tunavyopika chakula hivyo hii inaendelea kuathiri akina mama na watoto wa kike kwa  kupoteza muda mwingi kwenye kutafuta nishati ya kupikia ya kuni na Mkaa. 

Asilimia 70 ni magonjwa yasiyoambukiza ikiwemwo magonjwa ya mfumo wa upumuaji.

"Wanapokuwa wanatafuta nishati hiyo wanapunguza muda wa kutafuta elimu au kufanya shughuli nyingine za uzalishaji mali huko polini wanakutana na dhahama na matukio ya unyanyasaji wa kijisia.

Pia Nishati  isiyo safi na salama inaleta utofauti au kutokuwa na usawa kati ya wanawake na wanaume, watu wa mjini na vijijini wenye kipato na wasio na kipato." Amesema  Waziri Makamba

Kwa Upande wake Daktari Bingwa wa Magonjwa ya mfumo wa Upumuaji, kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili, Pauline Chale ameeleza kuwa Matumizi ya Nishati isiyo safi na salama  inasababisha changamoto nyingi hasa katika Afya na matibabu yake ni gharama kubwa 

Dkt. Pauline ameeleza kuwa mgonjwa wa Mfumo wa Upumuaji yanaondoa watu. Pia amesema matumi ya kuni, Mkaa na Mavi ya wanyama yanasumu zaidi ya 200 ndio maana watu wengi wanakuwa na macho mekundu kutokana na sumu hizinazopatikana kwenye moshi.

Friday, September 9, 2022

TALGWU yaiomba Serikali kufanya Mabadiliko Tozo Miamala ya Kibenki

Na Isaac Thadeo

CHAMA cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa Tanzania (TALGWU) kimeiomba Serikali kufanya mabadiliko katika sheria ya tozo za miamala ya kibenki ili kuepuka malipo ya mara mbili kwenye mshahara wa mtumishi wa umma. 
Mkuu wa Idara ya Habari na Uhusiano wa Kimataifa wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa Tanzania (TALGWU) Shani Kibwasali akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam.
Ombi hilo limetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Idara ya Habari na Uhusiano wa Kimataifa-TALGWU Shani Kibwasali akizungumza na waandishi wa habari kuhusu taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Chama kwa kipindi cha Januari hadi Juni 2022.

Shani amesema tozo hizo zinazidi kumbebesha mzigo na kumkandamiza mfanyakazi huku ikizingatiwa mishahara wanayopata haikidhi mahitaji ya kila Siku na familia zao. 

“Pia naomba nizungumzie suala la tozo za kibenki lililoanza kutekelezwa hivi karibuni. Tozo hizi zinawaathiri sana wanachama Wetu. Ikumbukwe kwamba watumishi wa umma kila mwezi wanalipa Kodi kwa kukatwa katika mishahara yao,” amesema Kibwasali na kuongeza kwamba,

“Lakini sasa kuanza kuanza kutekelezwa kwa tozo ya Serikali kwa miamala ya kutoa na kuhamisha fedha katika benki inamfanya mtumishi wa umma kutozwa zaidi ya mara mbili katika Pato moja kwa mwezi,”.

Kuhusu suala la nyongeza ya mishahara, amesema ni ukweli usiofichika kwamba wanachama wao ambao ni wahanga wakubwa kwani bado wanamanung’uniko na TALGWU kama msemaji wao hawajaridhika kabisa kwa jinsi nyongeza ya mshahara ilivyofanyika.

“Ila naomba niwatoe hofu wanachama wetu kwamba suala hili linashughulikiwa na Chama kwa kushirikiana na shirikisho la vyama huru vya Wafanyakazi nchini (TUCTA),” ameeleza Kibwasali.

Akizungumzia kuhusu mafanikio ya TALGWU kwa kipindi cha Januari hadi Juni mwaka huu, amesema kwamba hadi kufikia Juni 2022 walikuwa na jumla ya kesi 140 ambapo mawakili wa Chama wanasimamia kesi 100, mawakili wa nje wanasimamia kesi 13, na rufaa zilizopo Tume ya Utumishi wa Umma ni 27.

Kwamba Chama kiliandaa utetezi kwa watumishi 12 waliokuwa wamepewa mashataka na waajiri. Hivyo amesema kati ya kesi 140 walizonazo zilizoisha zilikuwa ni 39 na chama kimeshinda jumla ya kesi 35 na kushindwa kesi nne huku kesi nyingine zikiendelea Mahakamani.

Kibwasali amebainisha kuwa katika kipindi hicho pia TALGWU ilikuwa na jukumu jingine kubwa la kushughulikia haki na stahiki za wanachama ambazo kimsingi zipo kwa mujibu wa sheria ya Utumishi wa Umma na kanuni zake.

Hivyo amesema TALGWU inajivunia kuona Serikali imetekeleza maombi yao katika maeneo ya upandiahaji vyeo na mishahara, malipo ya malimbikizo ya mishahara na utawala Bora.

Thursday, August 18, 2022

Wiki ya AZAKI Kuzinduliwa leo Agost 18, 2022 jijini Dar es salaam

Na vicent Macha Dar es salaam.

Sekta binafsi zimetakiwa kushirikiana na Asasi za Kiraia (AZAKI,) Ili kusaidia kutatua changamoto zinazoikabili Jamii kwa kuwafikia wananchi kufahamu mahitaji yao na kuyapatia ufumbuzina kuleta maendeleo ya ya Taifa kwa ujumla.

Zoezi la Uzinduzi wa wiki ya Azaki likiendelea mapema leo jijini Dar es salaam.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Abdulmajid Nsekela wakati akifungua wiki ya AZAKI inayotarajiwa kufanyika kuanzia tarehe 24 hadi 28 Oktoba mwaka huu.

Aliyaongea hayo leo Agosti 18 jijini Dar es Salaam ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni “Maendeleo ya Watu, Habari Fanikiwa za Watu” na Maadhimisho ya mwaka huu yatafanyika jijini Arusha.

Aidha Nsekela amesema kuwa matokeo chanya yatapatikana kupitia wiki ya AZAKI na inaonekana dhahiri tangu kuanzishwa kwake mwaka 2018 licha ya changamoto lakini kumekua na kuongezeka kwa umoja na mshikamano miongoni mwa wadau.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Abdulmajid Nsekela.

‘’Suluhisho ya changamoto zinazoikumba jamii yetu inahitaji ushirikiano baina ya wadau ikiwemo mashirika, taasisi, sekta binafsi, Asasi za kiraia na Serikali kwa ujumla, ushirikiano na AZAKI na sekta binafsi ni hafifu tukishirikiana tutafika mbali zaidi katika kujenga uchumi wa jamii na Taifa kwa ujumla.’’ Amesema. Nsekela

Sanjari na hayo Mkurugenzi amesema, Ushirikiano baina ya AZAKI na sekta binafsi utasaidia kutatua changamoto kwa kiasi kikubwa kuwafikia wananchi wengi zaidi mjini na vijijini.

Nsekela amewasisitiza washiriki hao kuainisha njia mbalimbali mpya za kuwafikia wananchi na maendeleo kwa kuzingatia ushirikiano baina ya AZAKI hizo na sekta binafsi hasa katika uwekezaji utakayosaidia kuzalosha ajira

‘’Tujadili uwekezaji wa manufaa ya kiuchumi na kuwapa watanzania utulivu wa kiuchumi kwa kutoa wigo kwa ushirikiano baina ya sekta binafsi na AZAKI katika sekta mbalimbali ikiwemo elimu, afya na sekta nyingine za uwekezaji.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Foundation for Civil Society (FCS,) Bw. Francis Kiwanga amesema katika wiki hiyo ya AZAKI wanataraji matokeo chanya hasa katika kuimarisha ushirikiano baina ya Serikali, sekta binafsi na Asasi za kiraia katika ujenzi wa Taifa na ushiriki wa wananchi katika kuleta maendeleo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kituo cha Haki za Binadamu (LHRC,) Anna Henga amesema kusanyiko hilo la wana AZAKI tangu kuanza kwakwe 2018 limekuwa na malengo ya kufikia maendeleo endelevu pamoja na kubadili mtazamo wa wananchi na kutambua mchango wa Asasi za kiraia.

Hata hivyo amesema ni muhimu sekta binafsi kushiriki kikamilifu katika wiki hiyo muhimu hasa katika kupanua wigo wa kuwafikia wananchi, kutambua changamto za na kuzipatia suluhu na kuishukuru Benki ya CRDB kwa kuonesha ushirikiano tangu kuanzishwa kwa kusanyiko la Asasi za kiraia mwaka 2018.

Amesema, wiki ya AZAKI kwa mwaka 2022 itakuwa tofauti na licha ya kueleza mafanikio na maendeleo yaliyofikiwa wana AZAKI watatawanyika katika maeneo mbalimbali, kukutana na wananchi na kueleza huduma ambazo AZAKI zinatoa kwa wananchi.

Saturday, July 23, 2022

Waziri Ndalichako Atoa Maagizo kwa Mifuko ikiwemo NSSF na PSSSF Kuwalipa wastaafu mafao yao.

Na Muandishi wetu.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Ajira ,Vijana na Watu wenye Ulemavu Profesa Joyce Ndalichako ameagiza Mifuko ya mafao kwa wastaafu ikiwemo NSSF na PSSSF kuhakikisha wanawalipa Wastaafu wote wanaodaia  ikiwemo wanaodai kiinua mgongo,fidia,na Waliopunjwa.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Ajira ,Vijana na Watu wenye Ulemavu Profesa Joyce Ndalichako akizungumza na wazee waliyofika katika ukumbi wa NSSF Ilalal Boma jijini Dar es salaam.

Agizo hilo amelitoa leo Dar es salaam katika Mkutano aliouandaa Kwa ajili yakukutana na wastaafu wa Mkoa wa Dar es salaam kwa lengo ni kusikiliza malalamiko yao ,ambapo amedai kuwa tangu ameingia kwenye Wizara hiyo takribani miezi sita  amebaini wastaafu wengi wamestaafu  lakini bado hawajalipwa stahiki zao na wanaishi maisha magumu hivyo waje na vielelezo ili wafanyiwe mchakato wa kulipwa.

"Wastaafu hawa wanaodai madai yao wapo katika makundi tofautitofauti ikiwemo mapunjo ambapo mafao ya mtu yamekokotolewa kwa kutumia mshahara ambao ni mdogo kuliko mshahara halisi wa mfanyakazi alipostaafu na kusababisha mafao ya mkupuo anayopewa ni kidogo kuliko ilivyotakiwa"amesema Profesa Ndalichako.

Hata hivyo Waziri Ndalichako amesema kwamba amefuatilia na kubaini kuwepo kwa kesi za wastaafu ambazo  ziko wazi nakwamba suala lililopo  nikwenda tu kurekebishiwa mapunjo yao na kulipwa kwa kuzingatia mshahara wake wa mwisho ,nakusisitiza wastaafu  hao warudishiwe stahiki zao zote walizokuwa wanapunjwa.

Aidha amesema kwamba kuna baadhi ya Wastaafu vikokotoo vyao viko sawa lakini walikuwa hawana Elimu juu ya Vikokotoo hivyo,ambapo wamepatiwa Elimu na kujiridhisha kwamba hawajapunjwa mafao yao.
Zoezi la kuwasikiliza wazee likiendelea.

Kadhalika  Waziri Ndalichako amesema kumekuwa na makosa ya kiutendaji kutoka kwa baadhi ya watendaji wa mifuko ya pensheni kutokusikiliza malalamiko ya wastaafu wanaokuja kudai stahiki zao hivyo ameagiza watendaji hao kuacha tabia hiyo kwani wao ni watishi wa Umma.
 
Kwa upande wake Kassim Mafanya Mkazi wa Dar es salaam ambaye alikuwa Mtumishi  Chuo cha askari  Magereza Ukonga  amesema anashukuru kupata nafasi kusikilizwa kwani wastaafu wengi wamekuwa wanaishi kwa msongo wa mawazo na maisha yao hayaeleweki hawajui kesho yao  wamekuwa wakiahidiwa kupata nyongeza lakini hakuna kinachoendelea wengine wanafariki bila hata ya kufaidi chochote kutokana na jasho lao.

Naye Mtumishi Mstaafu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na watoto Chuki Kashaija mwenye ulemavu wa miguu  amesema alianza kazi tangu mwaka 1973 nakustaafu mwaka 2014,ambapo  amesema mpaka sasa hajapata mafao yake takribani miaka 8 sasa.

Wizara hiyo imepanga kufanya zoezi la kusikiliza malalamiko ya Wastaafu nchi nzima ikiwa ni Utekelezaji wa  agizo la rais Samia Suluhu Hassan aliloliagiza siku ya wafanyakazi Duniani( Mei mosi) iliyofanyika mwaka huu Jijini Dodoma.

Tuesday, July 12, 2022

MAGEUZI MAKUBWA YA KILIMO NDIO YATAKAYOWAINUA WANANCHI WA KIBAKWE

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu (Mb) Mhe. George Simbachawene akizungumza katika mkutano wa Hadhara katika Kijiji cha Kirusi jimbo la Kibakwe Halmashauri ya wilaya ya Mpwapwa.

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu (Mb) Mhe. George Simbachawene akikagua maendeleo ya ujenzi katika kituo cha afya Ipera kilichotengewa na serikali million 500 katilka jimbo la Kibakwe Halmashauri ya Mpwapwa.

Wananchi wakimsikilza Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu (Mb) Mhe. George Simbachawene katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Kikuyu kata ya Ipera jimbo la Kibakwe Halmashauri ya wilaya ya Mpwapwa.

…………………………….

Na mwandishi wetu.

Waziri wa Nchi Ofisi ya waziri mkuu, Sera Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene amehimiza watendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mpwapwa kufanya mageuzi makubwa ya kilimo kwa kuwekeza katika miradi ya kimkakati iltakayoongeza uzalishaji katika sekta ya kilimo.

“Lazima tuwekeze fedha kwenye miundo mbinu ya uzalishaji wa kilimo, wataalam wa kilimo wanaojengewa uwezo na wizara ya kilimo, wafanye kilimo shambani nawatumie maarifa waliyopata kwa kushirikisha wakulima”

Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu (Mb) Mhe. George simbachawene wakati alipofanya mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Kinusi Jimbo la Kibakwe katika Halmashauri ya wilaya ya Mpwapwa.

“Kata ya Malolo na kata Ipera ni eneo ambalo limejikita katika kilimo cha umwagiliaji, Halmashauri itizame namna ya kuimarisha miundo mbinu ya maji ili maji yasipote alisema Waziri”

Serikali ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan, katika bajeti yake ya 2022-2023 imejikita katika maeneo ya uzalishaji, bajeti ya kilimo imeongezwa kutoka billion 200 mpaka billion 900, hivyo fedha nyingi zitaletwa kijijini katika miradi ya kimkakati ya kilimo.

“Amefafanua serikali imeleta pembejeo za ruzuku, baadhi ya gharama zitalipwa na serikali ili mwananchi wapate pembejeo kwa bei nafuu ni lazima maafisa kilimo wajue hiyo mifumo ili waweze kuwasaidia wakulima”

Awali diwani wa kata ya Ipera Mhe. Festo Myuguye ameomba serikali kupimia wananchi maeneo yao na viwanja vyao, ili wananchi waweze kupata fursa ya kutumia hati za viwanja vyao kupata mikopo.

“ tunaomba pia serikali itusaidie kujenga miundo mbinu ya maji katika maeneo ambayo hayajafikiwa na huduma hiyo ili kuwafikia watu wengi, miundo mbinu iliyopo ilijengwa kabla ya Kijiji kuwa kikubwa”

RC SINGIDA APIGA MARUFUKU WANANCHI KUCHOMA MKAA NDANI YA MSITU WA MGORI

 

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dk. Binilith Mahenge akizungumza na Wananchi wa Kijiji cha Mughanga kilichopo Tarafa ya Mgori Wilaya ya Singida, kuhusu uharibifu unaofanyika katika Hifadhi ya Msitu wa Mgori waakati wa ziarayake ya siku moja ya kutembelea msitu huo ambapo aliambatana na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa na wilaya hiyo.
Dk. Mahenge akiangalia uharibifu wa msitu huo uliofanywa na wavamizi kwa kukata miti.
Mkuu wa Wilaya ya Singida, Paskas Mulagiri akizungumza wakati wa ziara hiyo.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Eliya Digha akizungumza katika ziara hiyo.
Muhifadhi wa Misitu wa Wilaya ya Singida, Uswege Mwasumbi akitoa taarifa ya operesheni mbalimbali zilizofanyika za kuwaondoa wavamizi wa msitu huo.
Pikipiki yenye namba za usajili  T 869 CZR ikiwa na magunia ya mkaa baada ya mwendeshaji wake kukamatwa katika hifadhi hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk.Binilith Mahenge na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wakijadiliana wakati wa ziara ya kukagua msitu huo.
Ziara hiyo ikifanyika.
Mifugo ikiwa ndani ya hifadhi hiyo.
Dk. Mahenge akiangalia wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama walivyokuwa wakibomoa moja ya nyumba isiyo rasmi iliyojengwa ndani ya hifadhi hiyo.
Ukaguzi wa msitu huo ukiendelea.
Wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wakiingia ndani ya nyumba isiyo rasmi iliyojengwa ndani ya hifadhi hiyo kabla ya kuibomoa.
Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wakiondoa gogo lililowekwa na wavamizi wa msitu huo kuzuia magari yasipite ili wasiweze kukamatwa.
Msafara wa magari ya wajumbe hao wakati wa ziarahiyo.
Baadhi ya wananchi wakiwa chini ya ulinzi wa polisi baada ya kukutwa ndani ya msibu huo.
Diwani wa Kata ya Mughanga, Nassoro Hassan akizungumzia msitu huo mbele ya mkuu wa mkoa.
Mmoja wa wananchi wa kijiji hicho akielezea msitu huo na jinsi walivyo ondolewa kwenye hifadhi hiyo baada ya kulipishwa fedha ambapo alidai hawana sehemu ya kulima wala kujenga.

Ukaguzi wa msitu huo ukiendelea.

Na Dotto Mwaibale, Singida

MKUU wa Mkoa wa Singida, Dk. Binilith Mahenge amepiga marufuku wananchi kuingia ndani ya Hifadhi ya Msitu wa Mgori  kufanya shughuli za kilimo, kuchoma mkaa na kuchunga mifugo bila kibali kutoka kwa mamlaka zinazohusika na uhifadhi wa msitu huo uliopo Wilaya ya Singida.

Ametoa onyo hilo leo Julai 13, 2022 wakati akizungumza na wananchi wa Kijiji cha  Mughanga baada ya Kamati ya Ulinzi na Usama ya Mkoa ilipotembelea msitu huo kujionea uharibifu uliofanywa na wavamizi huku wengine wakijenga nyumba za kuishi ndani ya hifadhi hiyo.

“Kwa sababu elimu tulikwishatoa na DC (Mkuu wa Wilaya) alipita vijiji vyote kutoa elimu ni marufuku kuingia ndani ya msitu huo na waambie yule mzee mwenye muvi (Dk.Mahenge) amekuja hana mzaha katika hili,” alisema.

Dk.Mahenge alisema mtu yeyote atakayekutwa ndani ya msitu huo atakamatwa na kama ana mifugo nayo itakamatwa kutaifishwa na kuuzwa.

Alisema kuendelea kuharibu misitu ya hifadhi ni laana kubwa ambayo wajukuu zetu wataweza kuja kutuchapa tukiwa ahela.

“DC alipita Novemba 2021 na akatoa elimu watu wasiingie kwenye msitu,wasilime wala kufugia mifugo lakini cha kushangaza leo watu wameuvamia na wanagawana kama mashamba na wamejiwekea mipaka baada ya kugawana ekari zaidi ya 200 hadi 300 kwenye msitu huo wenye miti aina ya Mininga,” alisema.

Mkuu wa Mkoa aliongeza kuwa baadhi ya maeneo wananchi wanahama na kwenda kuishi eneo jingine ili kupisha uhifadhi ili wanyama waendelee kuwepo na hivyo kuingizia serikali mapato ya fedha za kigeni kutokana na kutembelea hifadhi.

” Leo tunapata fedha kwasababu wazungu wanatoka kwao kuja kuangalia wanyama ambao kwao hawapo na sisi babu zetu waliwatunza wanyama ndio maana tumewakuta,” alisema.

Dk.Mahenge aliwaomba wananchi kutoa ushirikiano kwa kuwafichua watu wanaohujumu msitu wa hifadhi wa Mgori ili hatua kali ziweze kuchukuliwa dhidi yao.

Awali Muhifadhi wa Misitu Wilaya ya Singida, Uswege Mwasumbi, alimweleza Mkuu wa Mkoa wa Singida kuwa nyumba  704 za wananchi waliovamia msitu huo ambao upo mpakani mwa Wilaya ya Singida Vijijini na Mkoa wa Manyara zimebomolewa wakati wa operesheni iliyofanywa na askari wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS).

Mwasumbi alisema kati nyumba hizo zilizobomolewa 557 ni za ukanda wa eneo la kitongoji cha Kazamoyo ambalo ndilo lililoathirika zaidi na uharibifu wa ukataji miti ovyo kutokana na kuendesha shughuli za kilimo, ufugaji wa mifugo na uchomaji mkaa.

Alisema nyumba hizo zilibomolewa katika operesheni iliyofanyika mwezi Disemba mwaka jana ambapo eneo lililolengwa ilikuwa ni kitongoji cha Kazamoyo ambacho sio rasmi na hakitambuliwi na Serikali.

“Mifugo imebaki kuwa changamoto ndani msitu wa hifadhi Mgori na jeuri ya wafugaji ni kwamba wao wana nguvu ya pesa wanaweza kuwalaghai viongozi wa vijiji ili waendelee kuwepo ndani ya hifadhi hiyo,” alisema.

Mkuu wa Wilaya ya Singida, Paskas Mulagiri, alisema kaya zaidi ya 200 ziliondolewa ndani ya hifadhi hiyo baada ya wananchi kuuziwa na viongozi wa Serikali za vijiji wasio waaminifu kwa kuwatoza fedha na kuwapa stakabadhi ambazo serikali ilikuja kubaini zilikuwa ni feki.

Mulagiri alisema baada ya kubaini hilo, serikali iliwachukulia hatua za kisheria viongozi wa Serikali za vijiji ambao walihusika na udanganyifu huo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Eliya Digha, alisema wavamizi wa msitu huo wengi wao sio wenyeji wa vijiji vinavyouzunguka bali wanatoka mikoa jirani.

BEI YA UMEME KUTOKA MIRADI MIDOGO YA UMEME SASA NI SHILINGI 1600

 

Waziri wa Nishati, January Makamba akizungumza na Bw.Muhonja Antony ambaye anafanya kazi za uchomeleaji katika kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe. Waziri wa Nishati alifika kisiwani humo ili kukagua hali ya upatikanaji umeme unaozalishwa kwa kutumia mitambo ya umeme Jua.

Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba akitazama nguzo za umeme zilizobeba nyaya ambazo zimesimikwa chini ya ziwa Victoria ili kupeleka umeme kwenye kisiwa cha Ukerewe kutokea Bunda –Mara.

Nguzo za umeme zilizobeba nyaya ambazo zimesimikwa chini ya ziwa Victoria ili kupeleka umeme wa kiasi cha megawati 10 kwenye kisiwa cha Ukerewe kutokea Bunda –Mara.

Waziri wa Nishati, Mhe.January Makamba (kulia) akizungumza na mwananchi katika Kijiji cha Kibara wilayani Bunda baada ya kuona jinsi vituo vidogo vya mafuta vijijini vinavyofanya kazi na kuwaeleza wananchi kuhusu fedha zilizotengwa na Serikali takriban shilingi Bilioni 10 ili kuwakopesha wananchi wanaotaka kuwekeza kwenye vituo vidogo vya mafuta vijijini.

Waziri wa Nishati, Mhe.January Makamba akizungumza na wanachi katika Kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe wakati alipofika kisiwani humo kutatua changamoto ya upatikanaji wa umeme pamoja na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.

…………………

Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba, amesema kuwa, shilingi 1600 itakuwa bei mpya ya umeme kwa unit katika miradi midogo ya umeme iliyo nje ya Gridi ambayo itaanza kutumika tarehe 1 Agosti, 2022 ili kufanya wananchi kupata umeme wa uhakika na wawekezaji binafsi kuweza kujiendesha na kuwekeza zaidi.

Makamba amesema hayo tarehe 12 Julai 2022 akiwa katika kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe mkoani Mwanza wakati alipofika kisiwani humo kutatua changamoto ya muda mrefu ya upatikanaji umeme wa uhakika.

Maamuzi hayo ya Serikali yamekuja baada ya wawekezaji binafsi wa miradi midogo ya umeme kutakiwa kuuza bei ya umeme kwa Shilingi 100 kwa unit gharama ambayo iliwapa changamoto za kiuendeshaji na hivyo kushindwa kuwapa wananchi huduma ya umeme ya uhakika.

Akiwa kisiwani Ukara, Makamba alielezwa na wananchi wa kisiwa hicho kuwa, awali walikuwa wakilipa Shilingi 3500 kwa unit na walikuwa wakipata umeme kwa masaa 24 kwa siku lakini baada ya kutangazwa kwa bei ya umeme ya shilingi 100, kampuni ya JUMEME inayotoa huduma ya umeme kisiwani humo ilianza kuwapa umeme kwa masaa Sita tu kwa siku na pia kutakiwa kununua umeme kwa tokeni.

Akitoa ufafanuzi kwa wananchi kuhusu upangaji wa bei za nishati, alieleza kuwa unapaswa kuhusisha pande zote mbili ambazo ni Mwekezaji na Serikali hivyo, zoezi la upatikanaji wa bei mpya ya umeme limekuwa la uwazi na kwamba gharama mpya iliyotajwa haipo juu kama awali ili kutowaumiza wananchi na pia haitakuwa Shilingi 100 ili kampuni binafsi nazo ziwe na uwezo kufanya shughuli zake kwa ufanisi na kutoa huduma bora kwa wananchi.

Ameeleza kuwa Sera ya Nishati imetamka wazi kuhusu bei ya nishati inayopangwa na Serikali ikiwemo umeme, gesi na mafuta, kuwa lazima iendane na gharama za kuzalisha nishati husika.

Pamoja na kutangaza bei hiyo mpya, Waziri wa Nishati amezitaka kampuni husika kuhakikisha kuwa wanatoa umeme wa uhakika, wawasilishe mpango wa Biashara serikalini pamoja na kuwa na mkataba wa huduma kwa mteja.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kampuni ya JUMEME, Bi. Aida Kiangi aliahidi mbele ya wananchi wa UKARA kuwa kuanzia tarehe 1 Agosti, 2022 umeme kisiwani humo utatolewa kwa masaa 24.

Katika hatua nyingine, Waziri Makamba ameendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa kugawa mitungi ya gesi 167 ambayo itasambazwa kwa Shule za Serikali za Msingi na Sekondari kisiwani Ukara pamoja na walimu wa shule hizo ili wawahamasishe wananchi wengine kutumia nishati safi.

Awali, Waziri wa Nishati alikagua vituo vidogo vya mafuta wilayani Bunda, Mkoa wa Mara katika Kijiji cha Guta B na Kibara ikiwa ni mkakati wake wa kupeleka vituo vya mafuta hadi vijijini ili wananchi wapate Nishati safi na katika mazingira salama ambapo katika Mwaka wa Fedha 2022/2023 Serikali imetenga Shilingi Bilioni 2 ili kutoa mikopo kwa wananchi wanaotaka kuwekeza katika ujenzi wa vituo hivyo vijijini.

Akiwa safarini kuelekea wilayani Ukerewe Waziri Makamba alikagua nyaya za umeme zinazopita chini ya Ziwa Victoria ambazo zinapeleka umeme wa kiasi cha megawati 10 wilayani humo zikitokea Kisorya wilayani Bunda.

Sunday, July 3, 2022

IGP Siro apongezwa kwa kuleta maendeleo katika Kanisa

 Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro (kushoto) akipokea Baraka kutoka kwa Mhashamu Baba askofu Simon Masondole, askofu wa Jimbo Katoliki la Bunda mkoani Mara wakati wa ibada  ya ufunguzi wa kanisa katoliki Kigango cha Muliaza Parokia ya Butiama leo 03/07/2022. Picha na Demetrius Njimbwi – Jeshi la Polisi

Mhashamu Baba askofu Simon Masondole askofu wa jimbo katoliki la Bunda amepongeza kitendo cha kizalendo cha Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro, kwa kuwa mzalendo na kuchangia maendeleo kwa kujenga kanisa kitendo ambacho kitakuwa daraja litakalowezesha kuvusha wengine katika kuufikia wokovu.

Askofu Masondole amesema hayo Musoma Mkoani Mara wakati akiongoza ibada ya Misa takatifu iliyoambatana na ufunguzi wa kanisa kigango cha Muliaza parokia ya Butiama, kanisa ambalo limejengwa kupitia uwezeshaji wa IGP Sirro, wadau pamoja na watu wengine waliofanikisha ujenzi wa kanisa hilo.

Naye Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro amewapongeza wadau mbalimbali walioshirikiana nae hadi kukamilisha ujenzi wa kanisa hilo ambapo pia amewataka watu wengine kuendelea kukumbuka mazingira ya nyumbani kwao wanakotoka kwa kusaidia jitihada mbalimbali za kuleta maendeleo.

Ujenzi wa Daraja la Wami kukamilika Agost 31 mwaka huu

 Na Victor Masangu,Chalinze

UJENZI wa mradi wa Daraja jipya la Wami lililopo katika Halmashauri ya Chalinze wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani  linatarajiwa kukamilika Agosti 31 mwaka huu ambapo kutakuwa ni mkombozi mkubwa katika kupunguza wimbi la ajali za eneo hilo ambazo zimekuwa zikijitokeza mara kwa mara.
Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhandisi Godfrey Kasekenya alipotembelea kukagua ujenzi wa Daraja hilo ambapo limefikia asilimia 93 mradi huo unajengwa na kampuni ya Power Construction Corporation of China Ltd ikisimamiwa na kampuni ya Ilshin Engineers and Advance Solutions Ltd ya Tanzania na limegharimu kiasi cha shilingi bilioni 75.1

Kasekenya alisema kuwa daraja hilo limeghatimu nchi fedha nyingi kwani limejengwa kwa  kutumia teknolojia ya kisasa ambalo lina urefu wa mita 510 likiwa na barabara unganishi kutoka kila upande zenye urefu wa kilometa 3.8 zikiwa zimefikia asilimia 73.

“Ujenzi tumeambiwa unakamilika mwishoni mwa mwezi huu Agosti 31 na tunatarajia magari yaanze kupita Septemba Mosi Mwaka huu na litasaidia kupunguza ajali zilizokuwa zikitokea kwenye daraja la zamani ambalo lilijengwa mwaka 1959,”alisema Kasekenya.

Alisema kuwa ujenzi wa miundombinu unaendelea ambapo serikali ya awamu ya sita inaendelea kusimamia na kutoa fedha kwa ajili hiyo lengo likiwa ni kuifanya nchi kuwa na miundombinu mizuri.

“Kupitia ujenzi wa Daraja hili wataalamu wa hapa nchini wamejifunza teknolojia mpya ambapo asilimia 91 ni wataalamu wa ndani na asilimia tisa ni kutoka nje ya nchi mbali ya kupata utaalamu pia wamejiongezea kipato kupitia mradi huo,”alisema Kasekenya.

Aidha alisema kuwa malengo ya ujenzi wa Daraja hilo ni kukabiliana na changamoto ya ajali, kutumia muda mwingi, uharibu wa mali kutokana na daraja hilo kuwa jembamba na kona kali.

“Hichi ni kielelezo cha Rais bora wa kusimamia miundombinu na haya yalimfanya ateuliwe na bado anaendelea kutuonyesha ujenzi wa miundombinu bora,”alisema Kasekenya.

Naye Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) mkoa wa Pwani Baraka Mwambage alisema kuwa lengo la kujenga daraja hilo ni kutatua changamoto zitokanazo na daraja la zamani ambalo halikidhi mahitaji kwani ni jembamba lenye njia moja.

Mwambage alisema kuwa ujenzi huo umetumia Teknolojia ya madaraja marefu na litakuwa na taa za mionzi ya jua zenye kamera 78 ambapo fidia za mali zilizotolewa ni milioni 194.7. Mradi huo ulianza mwaka 2016.