Wednesday, March 22, 2017

SOBA HOUSE MPYA YAANZA DAR KWA LENGO LA KUSAIDIA VIJANA WA KITANZANIA

Kituo kipya cha kusaidia vijana walioathirika na madawa ya kulevya kinachofahamika kwa jina la Mamaz and Papaz Abilitation Center au maarufu kama (SOBA HOUSE) chenye makao makuu yake jijini dare es salaam. Na tawi lingine likiwa singida kinapenda kuwafahamisha watanzania kuwa kimeanza kazi hivi karibuni na kina takribani mwezi mmoja na kina jumla ya vijana 7. kituo hicho kinapenda kuwakaribisha vijana wote waliathirika na na dawa za kulevya. Kwani kituo kina wataalamu mbalimbali wakuweza kuwasaidia ikiwa walimu wakutosha na madaktari wakiwa tayari kuwahudumia waathirika wa dawa hizo.

EMMI ALLY GHAHAE MKURUGENZI MTENDAJI WA MAMAZ & PAPAZ AKIONGEA NA VYOMBO VYA HABARI
JANA JIJIN DAR ES SALAAM

Akiongea na waandishi wa habari mkurugenzi wa kituo hicho Bi. Emmi Ally Gahae alisema yeye ameguswa kwa namna moja au nyingine na tatizo hilo na kuamua kufungua kituo hiko kwa kuwa mwanae ni miongoni mwa waathirika wa tatizo hilo. na anapenda kuwahasa wazazi kuleta watoto wao ambao pia ni waathirika ili waweze kushirikiana nao kwa kuweza kuwafanya wakaacha kabisa na dawa za kulevya. Na kufanya shughuli nyingine za kijamii.aliongezea kwa kusema Soba House nyingine ambazo zinawahifadhi baadae wanarudia tena kutumia dawa hizo . lakini hii ni tofauti kabisa na hizo nyingine kwa kuwa huku wanakaa kwa muda wa miezi sita na wakimaliza wanapelekwa kwenye work shop. kuwapa furasa ya kuweza kufanya vitu wanvyoweza kufanya kwani wanawataalamu mbalimbali katika fani tofauti tofauti kwa ajili ya kuwasaidia vijana hao. kuweza kuachana na matumizi ya dawa za kulevya na shughuli zenyewe ni kama kilimo, ufundi mwashi,selemala na umeme kutumia kompyuta na fani nyingi walizo nazo.

PATRICK CHOKALA BALOZ MSTAAFU  (MSHAURI WA TAASISI YA MAMAZ & PAPAZ)
Na kutokana na taasisi hiyo bado changa inauwezo wa kuchukua vijana 40 na laengo ikiwa ni kuchukua watu wengi zaidi hata 100 kulingana na uwezo walio nao. Hivyo basi wanaiomba selikali makampuni na watu binafsi kuweza kuisaidia taasisi hiyo ili iweze kufika mbali zaidi. Na Iweze kuchukua watu wengi zaidi ya hao na pia kukidhi kwa mahitaji muhimu kama chakula mavazi na malazi. Kwani vita ya dawa za kulevya sio vita ya mtu mmoja tua au ni ya selikali peke yake bali ni ya jamii nzima. Na kwa hili taasisi hiyo kupitia walimu wake itaweza  kupitia shule mbalimbali nchi nzima lengo likiwa ni kuwafundisha wanafuzi ngazi ya msingi mpaka sekondari kuweza kupingana na dawa za kulevya kwani zinharibu nguvu kazi ya taifa.
BW. OMARY RAJABU KOMBE MJUMBE WA TAASISI


Na tarehe 26 ya mwezi 6 tunajua ni kilele cha kupambana na dawa za kulevya duniani kote  hivyo basi taasisi hii itafanya tamasha kubwa linao  ambatana na uziduzi wa taasisi hiyo.tamasha hilo litafanyika mkoani singida na mgeni rasmi anatarajiwa kuwa waziri wa  mambo ya ndani na taasisi inatarajia kuwahalika wakurugenzi toka mashirika mbalimbali, mabarozi, viongozi wa selikali na wadau mbalimbali. Pia mchango wako wa hali na mali unahitajika katika kufanikisha hilijambo. Pia wanahalikwa vijana wazee kwa watoto toka maeneo ya karibu kama Dodoma na sehemu nyingi kuja kwa wingi ili kuweza kupata elimu hii. Taasisi hii inapenda kuwashukuru wote waliofanikisha kuweza kusonga mbele kwa harakati hizi na waomba kuungana na selikali katika juhudi hizi.
       (Na muandishi wetu Vicent Macha dar es salaam).

1 comment:

Omy G said...

Thanks for letting us know the presence of this center i hope it will help to reduce the cases of drugs abuse especially to youths. Together we can help them.