Wednesday, March 8, 2017

TIZAMA MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE KUTOKA LHRC HAPA

Mkurugenzi Mtendaji wa kituo cha sheria na Haki za Binadamu Mama Hellen Kijo Bisimba akizungumza na wanawake mbalimbali waliokuwa wanashiriki katika maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani yaliyofanyika Jana ambapo Kituo hicho kilifanya maadhimisho hayo Jijini Dar es salaam na kuwakutanisha wanawake mbalimbali na mashirika Tofauti kuhakikisha kuwa wanajadili kwa Pamoja changamoto zinazowakabili na jinsi gani wanaweza Kuzitatua.


Mwenyekiti wa chama cha ACT WAZALENDO Mama Anna Mgwira akisikiliza kwa makini Hotuba mbalimbali katika maadhimisho hayo ambayo na yeye alishiriki kama mmoja kati ya wanawake waliodhubutu na kuweza kugombea nafasi kubwa ya Urais nchini akiwa ni mwanamke pekee kufanya hivyo katika uchaguzi Uliopita

Naemy Silayo akitoa Tamko la wanawake katika Shughuli hiyo.


Rebecca Jummy moja kati ya wanadada mashughuri wa sheria nchini ambaye amejizolea Umaarifu mkubwa katika kesi aliyoifungua dhidi ya sheria ya ndoa nchini akitoa mada katika Mkutano huo

Rais wa Vikoba,Devotha Likokola ambaye alikuwa Mgeni Rasmi ambapo amesema kuwa Wanawake wanatakiwa kuzitumia fursa zilizopo katika sekta mbalimbali zitakazowasaidia kuondokana na utegemezi ili kuifikia Tanzania ya Viwanda

No comments: