Thursday, September 7, 2017

TANZANIA IMESHAURIWA ILI KUFIKIA UCHUMI WA KATI KUTOWAACHA NYUMA WANAWAKE

ILI kufikia uchumi wa kati na wa viwanda Serikali imeshauriwa kutowaacha wanawake nyuma ambao ndio kundi kubwa la Watazania wote kwa asilimia zaidi ya 51 kwa mujibu wa sense ya mwaka 2012.
Mratibu wa programu ya Ardhi kutoka Shirika la Kimataifa la Care, Mary Ndaro, Akichangia mada katika mjadala wa wazi kwenye Tamasha la Jinsia Tanzania la mwaka 2017 ambalo ni mara ya 14 linafanyika tangu lianzishwe.
Wito huo umetolewa na Mratibu wa programu ya Ardhi kutoka Shirika la Kimataifa la Care, Mary Ndaro, katika mjadala wa wazi kwenye Tamasha la Jinsia Tanzania la mwaka 2017 ambalo ni mara ya 14 linafanyika tangu lianzishwe.
Alisema ili nchi yoyote iweze kuendelea kiuchumi, kiutamaduni na kijamii inatakiwa iende na wananchi wake wote na sio idadi fulani ya watu hivyo kwa Tanzania ambayo ina wanawake zaidi ya asilimia 51 ili iweze kuendelea lazima isiwaache nyuma wanawake hao ambao ndio wengi zaidi ukilinganisha na wanaume.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake wenyeulemavu ya Shirikisho la Vyama vya Watu wenyeulemavu Tanzania (SHIVYAWATA), Doris Kulanga akizungumza kwenye mjadala wa wazi katika Tamasha la Jinsia Tanzania 2017.
Alisema hali hiyo haimaanishi kwamba wanaume waachwe nyuma lakini ni muhimu kama inataka kuendelea lazima isiwaache wanawake kwa kuhakikisha ardhi inaongelea masuala ya wanawake ambayo kwa sasa inampa fursa ya kutumia tu bali imwezeshe kumiliki, kutumia na kufanya maamuzi kwenye vyote vitokana navyo na ardhi.
“Hapo tu ndipo tutapata nafasi ya kuongelea maendeleo, Tanzania ya viwanda na uchumi wa kati lakini tukiacha hawa wananchi ambao ni wengi tutakuwa tunapiga makitamu,” alisema Mary.
Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao, Lilian Liundi akizungumza leo kwenye mjadala wa wazi katika Tamasha la Jinsia Tanzania 2017.
Alisema kwa upande wa sera ya ardhi wanapokuwa wanazungumzia masuala mtambuka hakuna sehemu yoyote inayoonesha neno jinsia, pia inaongelea wanawake kutumia na sio kumiliki.
“Kwahiyo tuna jukumu la kuhakikisha sera na sheria zetu hazimfanyi mwanamke kuwa ili aweze kumiliki fursa za kiuchumi lazima aungane na mwanaume kwasababu si wanawake wote wenye wanaume pembeni wa kuwashikiria.
Mwanaharakati Mkongwe nchini, Dk Getrude Mongela akisisitiza jambo  kwenye mjadala wa wazi katika Tamasha la Jinsia Tanzania 2017.
“Kupitia sualala ardhi tunaona ni muhimu kuhakikisha sera inaenda mbele zaidi ya fursa wanawake kutumia kwasababu tumepewa hizo fursa miaka mingi iliyopita ukilinganisha tangu Tanzania ipate uhuru yapata miaka 56.
“Imetosha kusema kuwa kidogo kidogo wanawake watasogea wakati wa kusogea ni sasa kwani karibu asilimia 70 ya wanawake Tanzania ardhi inawahusu haijalishi wa kijiji au mjini na kama tunaongelea ukombozi wa kiuchumi lazima tuongeleea ardhi kwa mlengo wa kijinsia,” amesema Mary.

Mwanachama wa Mtandao wa Kijinsia Tanzania (TGNP), Profesa Marjorie Mbilinyi,akiuliza swali kwa watoa mada kwenye mjadala wa wazi katika Tamasha la Jinsia Tanzania 2017.




Baadhi ya ya washiriki kwenye mjadala wa wazi katika Tamasha la Jinsia Tanzania 2017.









No comments: