Thursday, September 7, 2017

TGNP MTANDAO YAHITAJI BAJETI YENYE MLENGO WA KIJINSIA (TAMASHA LA JINSIA 2017)

Serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania kupitia chombo chake muhimu cha kutunga sharia kinachofahamika kama bunge, linapotengeneza bujeti yake limeshauriwa kuwa bajeti hiyo iwe na mlengo wa kijinsia
Muwezeshaji wa TGNP Mtandao mama Gemma Akilimali akitoa ufafanuzi wa jambo fulani katika Tamasha 14 la Jinsia lililoandaliwa na Mtandao wa jisia TGNP 

Hayo yamesemwa mapema leo na mwanachama wa TGNP Mtandao Mama Gemma. S. Akilimali alipokuwa akiwasilisha mada hiyo katika Tamasha la 14 la Jinsia linaloendelea kufanyika makao makuu ya mtandao huo.

“Tunapozungumzia bajeti ya kijinsia ni ile bajeti isiyo na upendeleo kwa upande wowote bali iangalia na itoe nafasi kwa watu wenye mahitaji maalum kama walemavu na kuwapa fursa sawa wanawake kwa wanaume, lakini pia kutoa upendeleo kwa kundi linaloathirika zaidi kwenye vipaumbele kama elimu, maji, afya nk”. alisema Gemma

Lakini pia Mama Gemma alisema kuwa TGNP Mtandao ndilo shirika la kwanza kwa afrika kuanza kupigia kelele bajeti yenye mlengo wa kijinsia, na ndilo shirika lililofundisha mashirika mengi katika bara la afrika na mashirika hayo kwa sasa yameweza kufanikiwa kuwa na bajeti hiyo lakini kwa Tanzania bado hatujaweza kufikia kuwa na bajeti ya aina hiyo na baadhi ya nchi hizo ni kama Nigeria, Uganda nk.
Baadhi ya wawasilishaji mada wakiwa makini kufuatilia mjadala unaoendeshwa na Mama Gemma Akilimali  katika Tamasha la 14 la Jinsia 
Aliendelea kusema kipindi wao wanaanza kudai bajeti yenye mlengo wa kijinsia, serikali ilikuwa ikitengeneza bajeti kwa siri sana kiasi kwamba wananchi hawajui kiwango gani kimewekwa kwenye elimu au afya na jambo lingine kwamba ile pesa ikitoka wizara ya fedha kwanda wizara ya afya au elimu kunawatu waliopo kati hapo wanaipunguza na kutoka wizara husika mpaka kwenye mradi inaibiwa tena kiasi kwamba inayofika kwenye mradi inakuwa ni kidogo sana na inashindwa kumudu mahitaji husika.

Na pia katika utengenezaji wa bajeti haukuwa na uwiano sawa, ilikuwa wanapanga wanaume peke yake na kutowapa fursa wanawake ya kushiriki katika majadiliano wala maamuzi na wizara ilipoulizwa katika hali ilisema kazi hii huwa inafanywa mpaka usiku hivyo sio vyema kwa wanawake kuwepo mpaka muda huo. Wakati kwenye upangaji huo kunakuwa na posho hivyo inamfanya mwanamke kukosa fedha hiyo ambayo ingemsaidia na yeye kupunguza majukumu yake.

Kutokana na hili wao wakiwa kama watetezi wa bajeti yenye mlengo wa kijinsia waliomba wizara ya fedha kufanya utafiti mdogo ambao nao pia uliibua changamoto kama zifuatazo, viwandani wanawake wanapewa nafasi zile ndogo ndogo kama kupanga nguo, kufagia na nafasi za juu kama wakurugenzi na nyinginezo wanapewa wanaume.
Baadhi ya wageni waalikwa waliofika leo ikiwa ni siku ya tatu ya Tamasha la jinsia lililoandaliwa na Mtandao wa Jinsia TGNP
Na eneo la pili lilikuwa ni kilimo ambapo kulikuwa na shida kwa kuwa mwanamke mazao yake anayovuna yanatumika kwenye chakula nyumbani, lakini mwanaume yeye akivuna anaenda kuuza na kuingiza pesa hali ambayo inamyonya huyu mwanamke na kumfanya asiendelee mbele.

Lakini swala lingine pia ni mapato na matumizi ya serikali na hii inasimamiwa na ulipaji wa kodi lakini cha ajabu kwenye kulipa kodi anaumizwa mwananchi wa chini ambae hana chochote analazimishwa kilipa kodi na wakati makampuni makubwa ya migodi inapewa miaka 5 ifanye kazi bila kulipa chochote,


 lakini pia misamaha inayotolewa kwa makampuni na hoteli kwa mfano muwekezaji wa hoteli akija nchini anapewa miaka mitano ya kufanya kazi bila kulipa kodi na akiona miaka hiyo inakaribia kuisha anabadilisha jina ili kukwepa kodi mfano. Kilimanjaro Kempinsky iliyobadilishwa na kuitwa HYTTE Regency au Sheratoni ambayo sasa ni Dar es salaam Serena.

No comments: