Sunday, September 10, 2017

WAKULIMA WAMEPEWA ELIMU YA KUFAHAMU FAIDA ZA MBOLEA ASILI YA SAMADI

Wakulima kote nchini wametakiwa kutumia mbolea asili za samadi na kuepukana na matumizi ya mbolea za viwandani kwani sio nzuri kwa afya ya watumiaji japokuwa tunziona nzuri kwa kuwa mazao yanakuwa kwa muda mfupi.
Wakulima wa mazao mbalimbali wakisikiliza kwa umakini maelezo toka kwa Muadhiri wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine Bw. Boniphace Cija akielezea namna ya kuboresha kilimo na namna ya kutumia mbolea safi ya samadi kwa kilimo cha mazao ya chakula .
Akiongea na wakulima kutoka mikoa mbalimbali ya hapa Tanzania katika warsha iliyoandaliwa na Mtandao wa Jinsia TGNP muadhiri wa chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine Bw. Boniphace Cija alisema inabidi kuachana nayo ikiwezekana kupunguza matumizi yake.

Bw. Boniphace ameshauri kwa wale wenye mashamba makubwa vyema kutumia kilimo Mseto(mixed farming) ambacho kinahusisha mifugo na mimea kuwa kwa pamoja, hii itasaidia kupata samadi kwa urahisi na kuachana na mbolea za viwandani.

Na tena itasaidia kutokana kwamba mabaki ya mimea yatatumika kama chakula kwa mifugo na samadi ya mifugo itatumika kwa ustawi wa mimea hivyo kuepuka tatizo hilo la kula mboga ama matunda yasiyo na virutubisho asili.
Muadhiri wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine Bw. Boniphace Cija akitoa ufafanuzi wa jambo fulani katika warsha ya kilimo iliyoandaliwa na TGNP Mtandao mapema leo jijini Dar es salaam.
Lakini pia swala lingine ni kutumia dawa za kuulia wadudu wanaokula mazao ya mimea pia ni tatizo kwani sio wadudu wote ni wabaya hivyo kuna baadhi ya wadudu wanahitajika kwa ajili ya virutubisho kwenye udongo.

Endapo kutatokea tatizo la ugonjwa kwa mimea suluhu sio kupiga dawa unaweza kutumia kilimo cha Mzunguko wa Mazao kwani kinasaidia kuondoa magugu kwenye shamba lakini pia kuondoa magonjwa ya mimea na kuboresha viumbe hai muhimu katika udongo.

Na kilimo hiki ufanyika kwa mazao tofauti kulimwa katika shamba moja katika msimu tofauti ama vipande tofauti. Mfano mimea inayopunguza virutubisho kama nitrogen(jamii ya nafaka) itanguliwe na ile inayoongeza nitrogen katika udongo( jamii ya mikunde).

Lakini pia kilimo hiki upunguza athari ya mmomonyoko wa ardhi na kuboresha rutuba ya udongo na kusaidia kuongezeka kwa uzalishaji wa mazao.
Na kitu kingine magugu au wadudu wanapokuwepo shambani kwako sio vyema kupiga dawa au kuchoma moto kwani kufanya hivyo ni kuharibu ardhi kwa kuondoa rutuba na kuunguza wadudu wanaorutubisha udongo, unachotakiwa kukifanya ni kumwaga samadi nyingi ili kuua vimelea wabaya na magugu.

Kwani kwa kuchoma sio tu kuharibu ardhi lakini pia unasababisha madhara hata kwa viumbe wengine kutoweka kwenye ardhi ambao wapo kwa ajili ya kurutubisha udongo, hivyo unashauriwa kutumia njia nyingine mbadala kama kufuga mifugo kama kondoo au bata wanasaidia kula magugu tu hivyo wanazuia magonjwa ya mimea.


No comments: