Jiji la Dar
es salaam laingia katika mashindano ya miji inayokuwa kwa kasi zaidi duniani
likishindanishwa na miji mikubwa kama New York, Cap Town, St. poul, Nairobi nk.
![Tokeo la picha la dar es salaam](https://s-ec.bstatic.com/images/hotel/max1024x768/751/75159764.jpg)
Hayo
yamesemwa mapema jana na Mstahiki Meya wa jiji la Dar es salaam Mh. Isaya Mwita alipokuwa akijiandaa
na safari ya kuelekea katika jimbo la Chicago nchini marekani katika mkutano wa
mameya zaidi ya 84 duniani kote.
Mkutano huo
wenye lengo la kuwakutanisha mameya toka pande zote za dunia ili kuwajengea uwezo wa jinsi ya kuziongoza
Serikali za Mitaa(Local government) na namna ya kuongeza mapato katika Halmashauri
zao.
Hata hivyo
Meya Mwita alisema kuwa jiji la Dar es salaam ambalo linawakazi zaidi ya
milioni sita na ni jiji la tatu barani afrika kwa kukua kwa kasi katika
maendeleo, na hii ikiwa ni kutokana na kuwepo kwa huduma muhimu za kijamii kama
afya, maji pamoja na miundo mbinu mizuri.
Meya huyo
aliendelea kusema kuwa katika mashindano hayo yanayohusisha miundo mbinu jiji
la Dar es salaam limeingiza mradi wa UDART ambao maarufu kama mwendo kasi ili
kuweza kupambana na miji hiyo mikubwa duniani.
Katika
safari hiyo Mh. Mwita aliwataka watanzania kuwa wamoja na kumuombea ili
awakilishe vema jiji letu na hatimaye tuweze kuibuka washindi, Meya ameondoka
jana tarehe 2 na ataweza kurudi nchini tarehe 7 ya mwezi novemba 2017.
No comments:
Post a Comment