Monday, December 4, 2017

MAADHIMISHO YA WIKI YA MSAADA WA KISHERIA YAZINDULIWA LEO JIJINI DAR ES SALAAM

Mkuu wa wilaya ya Ilala Mh. Sofia Mjema amewataka wanasheria kuacha kukaa ofisini kusubiri kesi na badala yake kuingia mitaani kuwapa msaada wa kisheria wananchi ambao wanaonewa kwa kutofahamu sharia na haki zao.
Mkuu wa wilaya ya Ilala Mh. Sofia Mjema alipokuwa akizindua maadhimisho ya wiki ya msaada wa kisheria kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba John Kabudi mapema leo jijini Dar es salaam
Aliyasema hayo mapema leo jijini Dar es salaam alipokuwa akizindua maadhimisho ya wiki ya msaada wa kisheria ambapo alimuwakilisha Waziri wa Katiba na Sharia Prof. Palamagamba John Kabudi.

Maadhimisho hayo yanafanyika katika kanda zote saba za Tanzania ikiwa Kanda ya kusini, Kanda ya Kaskazini, Kanda ya Nyanda za juu kusini, Kanda ya Ziwa nk. Na kwa kanda ya pwani yamefanyika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mh. Sofia Mjema alipokuwa akitoa hotuba kwa wanasheria na wageni mbalimbali walioudhuria katika maadhimisho ya wiki ya msaada wa kisheria yaliyofanyika mapema leo jijini Dar es alaam.
Akiongea kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sharia Mh. Sofia Mjema alisema kuwa maadhimisho hayo yameaza leo tarehe 4 mpaka nane mwezi huu wa 12 na washiriki wakiwa ni Mahakama kuu, na mashirika binafsi yanayotoa huduma ya msaada wa kisheria kama  LSF, TLS, LHRC, TAMWA, WLAC, TAWLA nk.

Mkuu wa wilaya huyo aliendelea kusema kuwa ni kwa mara ya kwanza maadhimisho hayo yanafanyika chini ya wizara ya katiba na sharia na hapo mwanzo yalikuwa yakiratibiwa na mashirika binafi.

Na kauli mbiu ya mwaka huu ikiwa ni “Msaada wa kisheria kwa maendeleo ya wananchi”
Baadhi ya wageni walioudhuria katika maadhimisho ya Wiki ya msaada wa kisheria yaliyofanyika mapema leo viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam
Lakini pia jitihada za mashirika hayo zimeweza kuzaa matunda kwa kukaa chini kwa pamoja na wizara na kuunda sharia Namba 1 ya mwaka 2017 ambayo inaonyesha kutambulika kwa huduma hii kwa serikali ambapo mwanzo ilikuwa haijatambuliwa rasmi.

Mh. Mjema aliendelea kusema kuwa lengo kuu la maadhimisho hayo ni kujaribu kujenga ukaribu kati ya wanasheria na wanachi pamoja na kuwarudishia elimu hii ikiwa ni kama shukrani kwa wananchi hao kwa kuweza kuwapa msaada huo wa kisheria.
Rais Mstaafu wa TLS Bw. John Seka akiwasilisha salamu za Rais wa sasa Mh. Tundu Lissu ambaye kwa sasa ni mgonjwa na  yupo kwa matibabu nchini kenya katika maadhimisho ya wiki ya msaada wa kisheria nchini yaliyofanyika mapema leo jijini Dar es salaam.
Na “Pia inaeleweka kuwa wananchi wengi hawana elimu ya kutosha kuhusu sharia lakini pia hawana hata uwezo wa kulipia mawakili wa kuwasimamia katika kesi zao hivyo husababisha kukosa haki zao au kuonewa, na kutokana na hili wanahitaji msaada wa kisheria ambao utakuwa ni mkombozi wao”. Alisema Mjema

                       

No comments: