Wednesday, February 14, 2018

SHIRIKA LA IYF LA NCHINI KOREA LASAINI MKATABA HUU NA CHUO KIKUU HURIA JIJINI DAR ES SALAAM

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria Prof. Elifasi Bisanda  kulia akisaini mkataba na shirika la Korea la IYF lenye lengo la kuwajengea uwezo vijana kuhusu elimu ya moyo/kujitegemea, na kulia kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa IYF Bw. Song Hun Kim akisaini mkataba wa makubaliano wa shirika hilo na Tanzania.

Makamu Mkuu wa Chuo kikuu Huria cha Dar es salaam Prof. Elifas Bisanda akibadilishana mikataba na Mkurugenzi Mkuu wa shirika la IYF Bw. Seong Hun Kim mapema jana katika Chuo Kikuu Huria jijini Dar es salaam.

Bandi ya IYF ikitoa burudani mbele ya meza kuu mapema jana Chuo Kikuu Huria jijini Dar es alaam

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria Prof. Elifas Basinda akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kusaini mkataba na Shirika la YIF mapema jana jijini Dar es salaam.
Viongozi wa Shirika la IYF wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Chuo Kikuu Huria cha Dar es salaam baada ya kumaliza tafrija fupi ya kusaini mkataba wa makubaliano wa chuo hicho na shirika la nchini Korea la IYF.

NA VICENT MACHA - DAR ES SALAAM

Vijana wametakiwa kuwa na moyo  wa kujituma na kuacha tabia ya kusubiri kuajiliwa na matokeo yake kuweza kujiajiri kwa kazi za mikono na ujasiriamali.

Hayo yamesemwa mapema jana na Makamu Mkuu wa chuo Kikuu Huria cha Dar es salaam Profesa Elifa Bisanda alipokuwa akisaini mkataba kati ya chuo hicho na shirika la Korea kuhusu mafunzo ya elimu ya moyo chuoni hapo.

Akiongea na waandishi wa habari Makamu ya chuo hicho alisema kuwa lengo la shirika hilo la IYF ni kusambaza huduma hii duniani kote ya kuweza kuwa na elimu ya kujitegemea ambayo hapa nchini kwetu iliasisiwa na marehemu Baba wa Taifa.

Aliendelea kusema kuwa faida ya elimu hii kwa vijana ni kuweza kujiongoza wenyewe katika kujitafutia maisha ili wasiwe tegemezi kwa wazazi na kwa kutoa lawama kwa serikali kuwa hakuna ajira.

Aidha prof. basinda alisema kuwa elimu hii imesaidia nchi nyingi kama Korea Kusini yenyewe kwa kuwa na uchumi mzuri bila kutegemea rasirimali zozote za taifa na kumefanya sasa kuwa ni nchi yenye uchumi mkubwa duniani.

“Lakini pia kusaini mkataba huu aimaanishi ni kwa chuo kikuu huria peke yake bali hii nafasi imetolewa kwa wanafunzi wa vyuo vyote hapa nchini lakini kitovu kimekuwa ni hapa chuoni kwetu” alisema Profesa Basinda

“Na pia jambo lingine zuri ni kwamba IYF itakusanya vijana kutoka nchi nyingi duniani kwa kukaa kambi kwa pamoja, na hii itawasaidia vijana wetu kujifunza tamaduni za nchi nyingi duniani”. Alisema Profesa


Na mwisho profesa alipenda kuwashukuru IYF kwa kuleta wawezeshaji chuoni hapo kwani huduma hii itawasaidia walio wengi chuoni hapo wakiwemo walimu wa shule za msingi na sekondari kwa kupeleka elimu hii mashuleni kwao, na kwa wale ambao siyo walimu itawasaidia katika maeneo yao ya kazi. 

No comments: