Sunday, July 7, 2013
MAAJABU..MWARABU ASHIKWA AKIMBAKA TAHIRA HUKO RUVUMA
Chiposi alisema kuwa wazazi wa msichana huyo baada ya kubaini mtoto wao ni mjamzito walimuhoji ili kujuwa ni nani aliyemfanyia unyama huo ambapo licha ya kuwa msichana huyo ni tahira alieleza kwa shida kuwa alikamatwa kwa nguvu na kulazimishwa kutoa nguo yake ya ndani na Nassoro ambaye alimtaka ampelekee maji ya kuoga chumbani kwake.
Alieleza zaidi kuwa mtuhumiwa Nassoro kwa hivi sasa anashikiliwa na polisi lakini yupo hospitali ya serikali ya Mkoa Songea(HOMSO) ambako amelazwa akidai kuwa anasumbuliwa na BP ya kushuka na kwamba Jumatatu ijayo anatarajiwa kufikishwa mahakamani na hata kama atakuwa hajaruhusiwa atasomewa mashtaka yake yanayomakabili akiwa amelala kitandani kwenye hospitali hiyo kwani upelelezi wa tukio hilo umeshakamilika.
Kwa upande wake mganga mfawidhi wa hospitali ya Mkoa Songea (HOMSO) Dkt. Benedkto Ngaiza amethibitisha kumpokea mfanyabiashara huyo Jamali Nassoro ambaye alipelekwa hopitalini hapo akiwa chini ya ulinzi mkali na amelazwa wodi ya wanaume namba saba akiwa anaendelea kupata matibabu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment