Friday, March 28, 2014

EXCLUSIVE---JUKWAA LA KATIBA LATANGAZA NIA YAKE YA KWENDA DODOMA KULIFUNGA BUNGE MAALUM LA KATIBA IWAPO TU-----------

Mjumbe wa jukwaa la katiba tanzania bw izrael ilunde akizungumza katika kutano huo na wanahabari juu ya uamuzi wa jukwaa la katiba kuhusu bunge la katiba tanzania


              Jukwaa la katiba Tanzania JUKATA leo limetangaza nia yake ya kutaka kuwashawishi wananchi kuandamana hadi mjini Dodoma kulifunga bunge la katiba endepo kama hawataridhika na bunge hilo na kama watagundua kuwa wabunge hao hawana nia ya dhati ya kuwapatia katiba bora wananchi.
      
         Hayo yamesemwa leo muda huu jijini dar es salaam na kaimu mwenyekiti wa jukwaa hilo bw HEBRON  MWAKAGENDA wakati akizungumza na vyombo mbalombalo vya habari kuhusu mwenendo wa bunge hilo maalum la katiba linaloendelea mjini Dodoma.

Kaimu mwenyekiti wa jukwaa la katiba tanzania bw HEBRON MWAKAGENDA akizungumza na wananchi muda mfupi uliopita kuhusu bunge la katiba


                 MWAKAGENDA anasema kuwa jukwaa la katiba linaendelea kutathmini kile kinachoendelea bungeni na kama wakijiridhisha kuwa kinachoendelea hakielekei kuwapatia watanzania katiba mpya bali ni upotevu wa muda na rasimali za taifa basi JUKATA itatumia ibara ya nane ya katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania kuwaongoza wananchi kulifunga bunge maalum la katiba na kuanza harakati za  kuitafuta katiba mpya kwa utaratibu wenye mantiki na tija kwa taifa.
             
          Aidha jukwaa la katiba Tanzania limeipinga vikali hotuba iliyotolewa na raisi wa Tanzania dk JAKAYA KIKWETE wakati akifungua bunge hilo ambapo wamesema kuwa  hotuba ile ilifaa sana kutolewa na mwenyekiti wa chama cha siasa kwenye mkutano wa chama husika na sio katika bunge kama lile.
               
        Bw MWAKAGENDA anasema kuwa jukwaa la katiba linapenda kuwataarifu watanzania wote kwa ujumla kuwa katiba inayotengenezwa sio ya chama chochote cha siasa bali ni y watanzania wote hivyo ni kosa kwa chama cha siasa kuuteka mchakato huo kama wao ndo wanatengeneza katiba yao ambapo anasema kitendo cha wanasiasa kuwa na sauti kubwa katika bunge la katiba kimeufanya mchakato wote kutekwa na kuonekana kama mchakato wa kisiasa.

          Mchakato wa bunge la katiba unaendelea huku kukiwa na mabishano maengi ambayo watanzania wengi wamekuwa wakishindwa kuelewa ni ya nini hadi kufikia matumizi ya matusi na vijembe kutawala katika bunge hilo

No comments: