Sunday, March 8, 2015

MIVUMONI SEMINARY IMETISHA SANA,MATOKEO YAO YA MWAKA JANA YAWAFANYA WAWAPONGEZE WANAFUNZI WAKE

Katibu wa msikiti huo ABDALAH MOHAMED akizungumza na wanahabari leo nje kidogo ya hafla hiyo ya kuwapongeza baadhi ya wanafunzi waliofanya vizuri katika mtihani wa kidato cha nne mwaka jana
 Uongozi wa shule ya seminary ya mivumoni iliyopo jijini Dar es salaam leo umefanya shughuli maalum ya kuwapongeza wanafunzi wake waliohitimu masomo ya kidato cha nne mwaka jana baada kufanya vizuri na kuitangaza vizuri shule yao.
Shule ya mivumoni ambayo ilianza mwaka 2006 ikiwa na wanafunzi 108 hivi sasa ina wanafunzi 460 ambapo katika historia yake shule hiyo haijawahi kutoa mwanafuzni aliyepata daraja sifuri tangu kuanzishwa kwake.
Moja kati ya wanafunzi waliofanya vizuri katika shule hiyo FATMA SALEHE akizgumza na wanahabari ambapo amesema kiuwa siri kubwa ya kufanya vizuri ni pamoja na kuwa na nidhamu katika masomo na kusoma kwa bidii ambapo amesema kuwa pia kumtanguliza mungu katika masomo ndiyo chanzo cha yeye kufanya vizuri katika masomo yake.
Akizungumza na mtandao huu wakati wa hafla hiyo katibu wa shule hiyoABDALAH MOHAMED amesema kuwa shule hiyo inajivunia baada ya kufanikiwa kutoa wanafunzi wawili bora katika kumi bora kitaifa kwa miaka miwili ambapo ilifanya hivyo mwaka 2009 na 2013.
Amesema kuwa kwa mitihani ya kitaifa shule hiyo imekuwa katika kumi bora katika mkoa wa Dar es salaam kwa miaka yote sita na kitaifa imekuwa katika shule hamsini bora na mwaka 2013 shule hiyo imepata cheti cha ubora chini ya B.R.N na mkanda wa kijani wenmye ishara ya kuwa ni shule bora.
Mwanafunzi YASINI RASHID ambaye pia ni mmoja kati ya wanafuynzi waliofanya vizuri katika shule hiyo akielezea siri ya mafaniko yake
Pamoja na shule hiyo kupata matatizo ya kuungua na moto mnamo mwaka 2014 na kupotelewa na majengo pamoja na thamani mbalimbali za kufundishia bado shule hiyo imefanya maajabu katika mitihani ya nkidato cha nne mwaka huo huo baada ya kupata daraja la kwanza na lapili pekee huku kukiwa nhakuna daraja la tatu na kuendelea jambo ambalo uongozi wa shule hiyo umeliita ni jambo la kupongezwa kwani ni juitihada kubwa sana hadi kufikia hapo.







No comments: