Wednesday, July 8, 2015

BARAZA LA MADIWANI TEMEKE NALO LAVUNJWA RASMI,WAPONGEZWA KWA KAZI NZURI

Mkuu wilaya ya Temeke Sophia Mjema amewapongeza madiwani wa manispaa ya temeke kwa kutekeleza ahadi zao kwa wananchi kwa zaidi ya asilimia 90.

Akizungumza na waandishi wa habari hii leo wakati wa shughuli ya kufunga rasmi baraza la madiwani Temeke amesema kuwa asilimia kubwa ya miradi mbalimbali katika manispaa hiyo imekamilika kwa asilimia kubwa kutokana na ushirikiano mzuri wa viongozi na madiwani hao,ikiwemo shule,maabara,hospitali,huku akisema kuwa angependa kuwaona madiwani hao wakirejea katika nyazifa hizo hata baada ya uchaguzi mkuu na kuendelea kuifanya manispaa hiyo kuwa bora katika manispaa zote nchini.

Aidha akizngumza katika mkutano huo meya wa Temeke MAABAD HOJA amesema kuwa katika kipindi cha miaka mitano wamefanikiwa kukusanya mapato kwa zaidi ya asilima 90,na kufanikiwa kupata hati safi kutokana na kuwa na viongozi bora na wenye kufwata maadili.
Aidha meya  huyo amelivunja rasmi baraza hilo la madiwani huku akiowataka kuendelea kufanya kazi za kuwasaidia wananchi wakati wakiendelea kuomba ridhaa ya wananchi ili waweze kurejea tena katika nafasi zao.
PICHA CHINI NI MATUKIO MBALIMBALI KATIKA MKUTANO HUO




No comments: