Wakati bunge la jamhuri
ya muungano wa Tanzania likigubikwa na sintofahamu baada ya wabunge wanaounda
kambi ua upinzani maarufu kama ukawa kugomea na kufanya vurugu wakati wa
uwasilishwaji wa miswada mitatu ya dharura ya gesi na mafuta, naye Kiongozi
mkuu wa chama kipya cha ACT mh ZITTO KABWE ameibuka na kusema kuwa kitendo cha
kugomea miswada hiyo isiwasilishwe ni kitendo cha kishujaa na kinapaswa
kupongezwa na kila mtanzania mwenye mapenzi mema ya nchi yake.Shughuda wako Exaud mtei msaka
habari anasimulia-------
Pongezi hiyo ameitoa
leo jijini Dar es salaam wakati wa mkutano wa kwanza wa hadhara wa chama hicho
katika jiji la Dar es salaam ambapo amesema kuwa umefika wakati sasa wa
kuwaambia serikali ya CCM kuwa imetosha kuburuzwa na kufanya jambo la kishujaa
kama lililofanywa na viongozi wa upinzani bungeni.
“Huwezi kujadili
maswala makubwa kama ya gesi na mafuta ambayo moja kwa moja yanawagusa
watanzania ukayafanya mambo ya dharura na kutaka kuyapitisha haraka haraka bila
kuwashirikisha watanzania ambao ndio wenye mafuta yao,ni jambo ambalo
haliwezekani na watanzania hawatakubali kuona mafuta na gesi yao inamilikiwa na
watu wachache”amesema mh ZITTO.
Ameongeza kuwa swala la
mikataba ya gesi nchini na mafuta hayapaswi kufanywa kwa siri wala kukimbizwa
na badala yake bunge la sasa liachane na miswada hiyo hadi bunge lijalo chini
ya serikali mpya waanze kujadili upya miswada hiyo.
Katika mkutano huo
uliokusanya maelfu ya wanachama na wakazi wa Dar es salaam mwembe yanga chama
hicho kimeutumia kujitambulisha rasmi kwa wananchi wa Dar es salaam na kueleza
malengo yao kwa siasa za Tanzania na kwanini wamekuja na chama kipya.
Mh ZITTO anasema kuwa
chama cha ACT sio chama ambacho kimepandikizwa kwa ajili ya kuzigawa kura za
watanzania kama ambapo imekuwa ikielezwa kila kona bali ni chama ambacho
kimekuja kubadilisha mwelekeo wa siasa za Tanzania na kufanya siasa za maswala
ya wananchi zaidi zaidi ya kufanya siasa za kuwajadili watu na matusi.
Moja kati ya mambo
ambayo anasema kuwa chama hicho kimeshamiria kuyafanya ni kurudusha misingi na
miiko ambayo iliwekwa na baba wa taifa mwalimu nyerere kwa kulifufua azimio la
arusha ambapo kwa sasa wamelipa jina la azimio la tabora.
Naye mwenyekiti wa
chama hicho Taifa mama Anna Mghwira
amewaeleza wana Dar es salaam kuwa moja kati
ya mipango ya chama hicho ni kuifanya Dar es salaam iwe salama kwa wakazi wake
tofauti na sasa ambapo amesema kuwa Jiji hilo limekuwa sio salama kutokana na
kutokuwa na mpangilio unaoliweka kuwa jiji salama.
Chama cha ACT
kimeendelea na ziara zake katika mikoa mbali mbali kujitambulisha kwa wananchi
kwa lengo la kupata wanachama zaidi kuelekea uchaguzi mkuu mwaka huu
No comments:
Post a Comment