Friday, December 11, 2015

MADIWANI TEMEKE WAASWA KUWATUMIKIA WANANCHI KAMA WALIVYOAHIDI WAKATI WA KAMPENI

Meya mpya  manispaa ya Temeke Mh ABDALAH UREMBO akizngumza na wanahabari nje ya Mkutano huo
 Katibu Tarafa wilaya ya Temeke Mh LAWRENCE MALANGWA amewataka madiwani wa manispaa hiyo kuwa wabunifu katika kupanua vyanzo vya mapato mbalimbali katika manispaa hiyo.
Akizungumzia hilo leo jijini Dar es salaam wakati nwa uapishaji wa madiwani wa manispaa hiyo ya temeke LAWRENCE MALANGWA amesema kuwa ni vyema madiwani hao wakatumia fursa na ubunifu walionao katika kupanua vyanzo mbalimbali vya mapato ya manispaa hiyo na kuacha kuonea wafanya biashara wadogo wadogo katika ukusanyaji wa kodi  huku akisema kuwa wananchi wanategemea kufanya shughuli zao bila ya kusumbuliwa katika biashara zao ili waweze kujikimu katika maisha yao ya kila siku.
Baadhi ya madiwani wa Temeke wakila kiapo
Aidha meya mya  manispaa hiyo Mh ABDALAH UREMBO amewataka madiwani kutekeleza sera walizotoa kwa wananchi wakati wa kampeni na pia kuwa na hofu ya mungu  katika kuwatumikia wananchi kwani wananchi wa leo sio wa jana wa sasa ni wafwatiliaji na wana maamuzi ya hapo kwa hapo pale wanapoona unawatendea kinyume na matakwa yao,pia amewataka madiwani wote kumpa ushirikiano bila kujali itikadi za kisiasa ili kupeleka Gurudumu la maendeleo mbele

Madiwani wakisikiliza kwa makini

No comments: