Wednesday, September 6, 2017

MAMBO MATANO MUHIMU YA KUWEZESHA MWANAMKE WA KIAFRIKA (TAMASHA LA JINSIA 2017)

Mambo muhimu matano yanayotakiwa katika kumuwezesha mwanamke wa kiafrika ambayo hawayapati mabinti waliopata mimba mashuleni na hii ni ndani ya familia au jamii iliyowazunguka.
Mwanachama wa TGNP Mtandao Bi. Rehema Mateba akiongoza Warsha ya kupinga ukatili dhidi ya wanafunzi waliopata mimba mashuleni katika Tamasha la 14 la Jinsia Mabibo Dar es salaam.

Akiongoza warsha hiyo ya kupinga ukatili dhidi ya watoto waliopata mimba shuleni Bi. Rehema Mwateba alisema kuwa mambo haya ni muhimu sio tu kwa mabinti waliopata mimba mashuleni bali ni kwa kila binadamu, ila kwa watoto hawa imekuwa kama ni desturi kutopewa kwa kuonekana wao ni wakosaji zaidi watu wote.

                                        Miongoni mwa mambo hayo ni yafuatayo.
1.     Ustawi – ni ile hali ya kukua vyema kwa kupata mahitaji yale muhimu ya kibindamu ambayo akiyakosa mtu yoyote basi hakuna maisha, na hii inajumuisha mahitaji yanayopimika na yale yasiyo pimika mfano wa mahitaji yanayopimika ni vitu kama  Chakula, Mavazi, Malazi pamoja na Maji, na mahitaji yasiyopimika kama Upendo, Furaha, Heshima, Kusikilizwa, Kuthaminiwa kupatiwa Ulinzi, kuchangamana na wengine nk. Kwaiyo unakuta hivi vyote wanavikosa wasichana waliopata mimba mashuleni.
Bi. Salma Majaliwa toka Visiwani Pemba akielezea hali ilivyo kwa mabinti waliopata mimba wakiwa shuleni kwa upande wa Tanzania Visiwani, kuwa kwao sheria inawaruhusu kuendelea na masomo kama kawaida baada ya kujifungua.

2.     Ufikiaji rasilimali – hii pia ni changamoto kubwa wanayokutana nayo wasichana wanaopata mimba mashuleni kwani kutokana na kutopewa heshima nyumbani au hata katika jamii hali inayowafanya wawe na msongo wa mwazo na kushindwa hata kuzitumia vizuri rasilimali walizo karibu nazo kama Zahanati inaweza kuwa karibu lakini ikashindwa kumnufaisha binti huyu.

3.     Kupata Muamko – hii ni ile hali ya kushtuka na kuchukua hatua ya haraka endapo umedhamilia kufanya jambo Fulani, lakini kwa wasichana hawa wanashindwa kupata miamko kwa kuwa bado akili hazijapevuka na kujijua kuwa sasa nina mimba inabidi nifanyaje kuhusiana na hili? Na pia wanashindwa kuchukua hatua ya haraka, lakini pia kujua kuwa nahitajika niende kwa wataalamu wa uzazi ili wanisaidie kwa mabinti hawa wanakuwa hawana fikra hizo na mpaka akipata muamko inakuwa ni siku ya kujifungua .
Diwani wa Mwadui Luhombo mkoani Shinyanga Mh. Sarah Masinga akitoa ufafafanuzi wa jambo fulani katika Tamasha la jinsia la 14 lililoandaliwa na mtandao wa jinsia TGNP.
4.     Kushiriki na kushirikishwa – hii ni ile hali ya kuwepo na kupewa nafasi ya kusikiliza na kutoa maoni yako katika kitu chochote cha kifamilia hata cha kijamii pia. Lakini kwa wazazi wengi hawaliangalii hili wakiona binti yao kapata ujauzito hawampi nafasi ya kumsikiliza katika maamuzi ya hali ya afya yake lakini pia hata kumshirikisha katika mambo ya kifamilia kwa kumuona kama ni mkosefu.

5.      Kumiliki mali – hili pia ni tatizo kubwa sana sio tu kwa wahanga wa mimba za mashuleni bali ni kwa wanawake wengi wanakumbana nalo tatizo hili la kutomilikishwa  mali. Na kwa upande wa wahanga wa mimba za mashuleni kwa familia nyingi hawapewi kabisa nafasi hizi kwani wanaonekana kuwa wameshakuwa wakubwa ndio maana wamepata  mimba, hivyo wazazi wengi uamini kuwa binti huyo atamiliki mali ya mumewe ambae ndio aliyempa mimba hiyo.
Muwezeshaji wa TGNP Mtandao Mama Rehema Mateba akiendelea kutoa elimu kwa vijana, wazazi toka mikoa mbalimbali ya Tanzania ili kupinga ukatili unaofanywa kwa mabinti wanaopata mimba shuleni.

Hivyo basi kutokana na hali hii wanageni toka maeneo  mbalimbali ya Tanzania bara na Visiwani walipendekeza mapendekezo yafuatayo .

Kwanza kutoa elimu kwa wazazi ili waachane na mila potofu kwamba binti akipata mimba shuleni basi nafasi yake ya kusoma imeishia hapo, lakini pia watambue kuwa hata kama kapta mimba akiwa shuleni bado ni mtoto wao na anatakiwa kupewa mahitaji kama mtoto mwingine na suruhisho sio kumfukuza au kumpiga.

Lakini pia jambo lingine ni kutumia marafiki wa elimu waliyoenea karibu mikoa yote ya Tanzania bara kwani wao wanatoa misaada ya kimawazo na kujua watakupa mbinu gani ili mtoto aendelee na elimu, lakini pia kumpa darasa litakalomuongoza kufikia malengo yake kwani kupata mimba sio mwisho wa maisha ya shule.

                          


No comments: