Wednesday, September 6, 2017

Makamu wa Rais azindua Kamisheni ya Kiswahili


Zanzibar. Makamu wa Rais, Samia Hassan Suluhu amezindua rasmi leo Jumatano shughuli za Kamisheni ya Kiswahili Afrika Mashariki, lengo  ikiwa ni kuisogeza karibu taasisi hiyo muhimu ya lugha kwa nchi wanachama.


Pia, Mama Samia alizindua mpango mpango mkakati wa Kamisheni ya Kiswahili Afrika Mashariki ukiwa na lengo la kuhimiza matumizi ya lugha hiyo kwa nchi wanachama katika nyanja mbalimbali.
Alisema kamisheni hiyo imekuwa ikifanya kazi zake kwa takribani miezi sita lakini  awali ilikuwa haijazinduliwa jambo ililofanya watu wengi kutofahamu shughuli zake.

Akuzungumza kwenye kongamano hilo la kimataifa la  kwanza linalofanyika Zanzibar kwa siku tatu, Mama Samia alisema ili kushirikiana kwenye nyanja tofauti umoja wa forodha, soko la pamoja, sarafu moja na ushirikiano wa kisiasa lugha ya Kiswahili  inatakiwa kuenziwa kwa sababu ndicho kiunganishi.
Pia aliwaomba nchi wanachama wa kamisheni hiyo kuongeza juhudi kwenye mtumizi ya Kiswahili kwani wasijionye wanyonge kuliko wengine huku akisema serikali za nchi wanachama zitakuwa zikichangia bajeti ya kamisheni hiyo.

Aidha, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Balozi Augustine Mahiga aliwataka wananchi wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kukitumia Kiswahili kutokana na kuwaunganisha watu wote.

Alisema licha ya kuwepo kamisheni lakini imekuwa ni fursa ndani ya jumuiya kutokana na baadhi ya wanachama ambao hawafahamu vyema lugha za Kiswahili kuomba walimu wa Kiswahili kutoka Tanzania.
Kongamano hilo linashirikisha nchi zaidi ya saba ambazo ni Rwanda, Burundi, Kenya, Uganda, Sudan Kusini, DR Congo na wenyeji Tanzania huku wageni wengine wakitoka kwenye mataifa rafiki kama vile Namibia na Msumbiji.



                              

No comments: