Thursday, January 25, 2018

MBUNGE WA ZANZIBAR MOHAMED RAZAR AMKABIDHI MISAADA WAZIRI MKUU KWA AJIRI YA WATU WASIOJIWEZA

MBUNGE wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mohammed Razar, amemkabidhi msaada wa chakula kwa Waziri, Kassim Majaliwa kwa ajili ya kuwasaidia wananchi wenye uhaba wa chakula.
Akikabidhi misaada hiyo mapema leo katika ofisi ya waziri mkuu jijini Dar es salaam Bw. Razar alisema kuwa anatekeleza ilani ya chama cha mapinduzi kwani ndio chama tawala na ndio chenye dhamana ya kuhakikisha wananchi wake wanakuwa katika hali ya usalama.

Mbali na hilo, Razar amempa nafasi Majaliwa amchagulie mikoa mitano ambayo itafanyiwa mashindano na kila mkoa utatoa timu ya taifa ya michezo ya watoto wa shule, ambapo mashindano hayo atayagharamia yeye mwenyewe kuanzia jezi, mazoezi na vitu vingine.

Aidha, Razar ameelezea dhamira yake ya kutaka mashindano hayo yaanzishwe ni kutokana na timu za mpira Tanzania, kuwa na idadi kubwa ya wachezaji kutoka nchi jirani kuliko wale wanaotoka nyumbani, hivyo anachokitaka ni kuzalisha vipaji na kuvikuza vije kuchezea timbu zao hapo baadae.
Lakini pia mbunge Razar alipenda kuwapongeza Marais wote wawili akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Dr. Magufuri na Dr, Sheni kwa kazi nzuri wanazozifanya za kutetea maslahi ya watanzania na kuwakomesha mafisadi.

No comments: