Thursday, April 19, 2018

FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY YABADILI NEMBO YAKE, NA HUU NDIO MUONEKANO WA NEMBO YAO MPYA

Baada ya zaidi ya muongo mmoja na nusu kufikia Azaki nchi nzima, Sasa Foundation for Civil Society (FCS) inajikita katika kuongeza ufanisi na juhudi za kufanya kazi kwa ushirikiano na wadau wote katika kuleta maendeleo.

Baada ya uzinduzi huu ndio muonekano wa Nembo mpya ya Foundation for Civil Society (FCS).

Hayo yameelezwa mapema jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa FCS Bw. Francis Kiwanga wakati wa uzinduzi nembo mpya ya shirika hilo ambayo itaendana na mabadiliko na mfumo wake wa utendaji.

Alisema kuwa hii itahusisha kushirikiana na taasisi zote za Serikali, Bunge, Sekta binafsi, Asasi za kiraia (AZAKI) ili kufikia Maendeleo Endelevu ya Dunia pamoja na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa kuboresha maisha ya watanzania ifikapo 2025.

Aidha aliongeza kuwa kwa sasa FCS itatoa ruzuku kwa wastani wa Asasi 150 kwa pande zote mbili za muungano yaani Tanzania Bara na Visiwani kila mwaka, ambapo hapo awali ilikuwa ikitoa kwa Azaki zaidi ya 5500 zilizokuwa zikihudumia wananchi wa mikoa yote hapa nchini.

Alisisitiza kuwa kiasi cha ruzuku kitaongezeka na kwa sasa taasisi hiyo itatoa ruzuku zenye thamani ya billion 11. kwa mwaka na muda wa mkataba pia utakuwa mrefu hadi kufikia miaka miwili ili kupata matokeo mazuri kwa miradi itakayofadhiliwa na FCS.

Akieleza sababu ya kufanya hivyo alisema kuwa wamejikita katika eneo la utawala bora na maendeleo hivyo siyo rahisi kuboresha maeneo hayo kwa mkataba wa mwaka mmoja au miezi sita tu, Hivyo wameona kuna haja ya kuongeza mkataba na kiwango cha ruzuku katika kufanikisha hili.

Na mwisho kabisa alipenda watu wafahamu kuwa FCS ipo kwa ajili ya watanzania hivyo waondoe mila potofu ya kuwa ni chombo ambacho hakina ubia na serikali na kwa sasa watafanya mambo mengi mazuri kwa kushirikiana na serikali katika kuleta maendeleo kwa wananchi wa Tanzania.


            Mazungumzo ya azaki yanaendelea kupitia hastag hizi.

                                        #AZAKITanzania  / #CivilSocietyTanzania 


Mkurugenzi Mtendaji wa Foundation for Civil Society Bw. Francis kiwanga akitoa maana ya kitu kimoja baaba ya kimoja katika nembo ya kwanza ya shirika hilo kabla ya kuzinduliwa kwa nembo mpya.


Zoezi la uzinduzi wa nembo mpya ya Foundation for Civil                                        Society likifanyika.

Baadhi ya washiriki kutoka AZAKI mbalimbali hapa nchini wakifuatilia matukio yanayoendelea katika Tafrija hiyo ya Uzinduzi wa nembo mpya ya FCS.

Baada ya Uzinduzi wa nembo mpya ya FCS kulifuatiwa na tukio lingine la uzinduzi wa tovuti mpya (Website) mpya ya shirika hilo kama inavyoonekana pichani.

Washiriki wa semina wakiendelea kusherehekea tafrija.

Picha ya pamoja ya wafanyakazi wa shirika la Foundation For Civil Society. 

Wafanyakazi wa Foundation for Civil Society wakiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa Tafrija hiyo, Ambao pia ni wana AZAKI wanaofanyanao kazi kupitia miladi mbalimbali wanayoiendesha.

No comments: