Friday, December 29, 2017

ARUSHA WAIOMBA KAMPUNI YA ABACUS PHARMA (A) LTD KUWAPELEKEA BIDHAA ZA SUGAR FREE

Muonekano wa jiji la Arusha katika picha

Na Dotto Mwaibale

WANANCHI wa jijini Arusha wameiomba Kampuni ya Abacus Pharma (A) LTD kuwapelekea bidhaa za Sugar Free ambazo zinasaidia kupunguza  matumizi makubwa ya sukari.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi aliyekuwepo mkoani humo kusherehekea Sikukuu ya Krisimasi walisema bidhaa hizo ni mkombozi kwao.

"Binafsi napenda kusema bidhaa hizi za Sugar Free kwa hapa Arusha zitapata soko kubwa kutokana na watu wengi kuathiriwa na ugonjwa wa kisukari" alisema Mzee Mollel mkazi wa Njiro.

Mollel alisema watu wengi jijini humo wananchi kwa masharti ya ulaji na unywaji wa vitu visivyo na sukari jambo ambalo limekuwa ni changamoto kubwa karibu familia nyingi.

Alisema wakazi wa jiji hilo wamezipokea kwa mikono miwili bidhaa hizo ambapo wameiomba kampuni hizo kufungua tawi mjini humo ili bidhaa hizo ziweze kupatika wakati wote.

"Tunaomba bidhaa hizi ziuzwe na maofisa mauzo wa kampuni hiyo wasiwape wenye maduka itakuwa changamoto kupata maelezo ya kina ya matumizi yake na tunahofu wakiachiwa wafanyabiashara wengine wanaweza kutupandishia bei" alisema mkazi mwingine wa jiji hilo aliyejitambulisha kwa jina la Laizer.

Laizer alisema humo kumekuwa na unywaji na ulaji wa vyakula vyenye sukari lakini kuingia kwa bidhaa hizo zitasaidia sana wananchi hasa baada ya kupata maelekezo ya utumiaji wake.

Akizungumza bidhaa hizo, Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Abacus Pharma (A) LTD, Ramesh Babu alisema bidhaa hizo zimesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza matumizi makubwa ya sukari katika vyakula. 

Alisema bidhaa hizo zimetengenezwa mahususi ili kukabiliana na ongezeko la sukari mwilini na hivi sasa zinapatikana kwa bei ya chini katika soko la nchi za Tanzania, Uganda, Kenya, Rwanda na Burundi na kuwa bei hizo zipo kuanzia shilingi,4200, 4,500, 5,700, 8,850 na za bei ya juu ni shilingi 13,000 na kuwa zinategemea bidhaa husika.

"Bidhaa hizi zipo za aina mbili za sugar free gold  ambazo hutumika katika chai, uji, na vinywaji baridi tu  na sugar free natura hutumika katika baking, kupikia vyakula vinavyohitaji sukari katika upishi na pia hutumika katika chai, uji na vinywaji baridi na matumizi yake ni rahisi sana," alisema Babu.

Alisema kwa Tanzania bidhaa hizo zimeanza kuchukua soko kubwa baada ya wananchi kuona umuhimu wake na hivyo wanategemea muitikio utaendelea kuwa mkubwa.

Aliongeza kuwa, lengo kubwa la kampuni hiyo kusambaza bidhaa hizo ni kusaidia jamii kuelewa matumizi ya bidhaa hizo ambazo hazina sukari ingawa zina ladha ya sukari kama ile ya kawaida  na kwamba bidhaa hizo zimethibitishwa na Shirika la Afya Duniani (WHO).

Akizungumza katika uzinduzi wa bidhaa hizo, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya homoni na Kisukari kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Faraja Chiwanga alisema ugonjwa wa kisukari ni changamoto kubwa kwani Tanzania ni nchi ya tano Barani Afrika kwa kuwa na wagonjwa wengi.

Alisema hali hiyo inatokana na watu wengi hasa vijijini kutojijua mapema kama wameathiriwa na ugonjwa huo ambapo baadhi yao huanza kugundua baada ya kupata upofu, kukatwa miguu na kadhalika. 

Aliongeza kuwa, matibabu ya mgonjwa mmoja wa kisukari yanafikia asilimia 25 ya pato la familia fedha ambazo ni nyingi jambo linalowafanya wauguzaji kukata tamaa ya kumtibu mgonjwa na kuamua fedha hizo kuzielekeza katika matumizi mengine.

Dk.Chiwanga alitoa mwito kwa kusema ni vizuri kuzuia kupata kisukari kuliko kutibu.

Akizungumzia bidhaa za sugar free alisema hazitibu ugonjwa wa kisukari isipo kuwa zinamsaidia mgonjwa au mtu mwenye kisukari anapokula vyakula vingine visivyo na sukari kupata radha ile ile.

Alisema mtu mwenye ugonjwa wa kisukari hatakiwi kabisa kuvuta sigara ingawa vitu vingine kama vinywaji na pombe anatakiwa kutumia kwa uangalifu.

Sunday, December 24, 2017

JUMUIYA YA WAZAZI TANZANIA MKOA WA DAR ES SALAAM, WAMPOKEA KWA KISHINDO MWENYEKITI WA TAIFA WA JUMUIYA HIYO DK. EDMUND MNDOLWA

JUMUIYA YA WAZAZI TANZANIA MKOA WA DAR ES SALAAM, WAMPOKEA KWA KISHINDO MWENYEKITI WA TAIFA WA JUMUIYA HIYO DK. EDMUND MNDOLWA
 Mwenyekiti wa Taifa wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania Dk. Edmund Mndolwa akisalimia baadhi wa wana CCM waliofurika katika ukumbi wa Tawi la CCM Mwinjuma, Mwananyamala jijini Dar es Salaam, ambao walifika kumlaki katika mapokezi yaliyoandaliwa na Jumuiya hiyo mkoa wa Dar es Salaam, jana.
 Gari la Dk. Mndolwa likiwasili lango Kuu la Ofisi ya CCM mkoa wa Dar es Salaam wakati wa mapokezi hayo
 Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania-Zanzibar  Abdallah Haj Haidar akimpokea Dk Mndolwa kwenye Ofisi ya CCM mkoa wa Dar es Salaam
 Mwenyekiti wa Taifa wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania Dk Edmund Mndolwa, akisalimiana na  Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam Kate Sylivia Magdalena Kamba alipowasili Ofisi ya CCM mkoa huo
 Mwenyekiti wa Taifa wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania Dk Edmund Mndolwa, akisalimiana na  Katibu wa CCM mkoa wa Dar es Salaam Saad Kusilawe, alipowasili Ofisi ya CCM mkoa huo
 Mwenyekiti wa Taifa wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania Dk Edmund Mndolwa, akisalimiana na  Katibu wa Jumuiya hiyo mkoa wa Dar es Salaam Lugano Mwafongo, alipowasili Ofisi ya CCM mkoa huo
 Mwenyekiti wa Taifa wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania Dk Edmund Mndolwa, akisilindikizwa na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam Kate Sylivia Magdalena Kamba kwenda kusaini vitabu wa wageni na kuzungumza na uongozi, alipowasili Ofisi ya CCM mkoa huo
 Dk. Mndolwa akisaini kitabu wa wageni katika Ofisi ya Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam alipowasili. Kulia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi mkoa huo, Frank Kalokola Kamngisha
 Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania-Zanzibar Abdallah Haj Haidar akisaini kitabu cha wageni, huku Dk. Mndolwa akiendelea kufanya hivyo pia.
 Abdallah Haj Haidar akisalimia
 Mama Patricia Rukia Mndolwa akisalimia
 Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania-Bara Burhan Rutta akisalimia
 Katibu wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, Ndugu Kusilawe akisalimia
 Kalokola akimkaribisha Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, amkaribishe Dk. Mndolwa kuzungumza na Uongozi
 Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam Kate Sylivia Magdalena Kamba alizungumza kabla ya kumkaribisha Dk Mndolwa kuzungumza
 Kate Kamba akimkaribisha Dk Mndolwa kuzungumza na uongozi
 Dk. Mndolwa akizungumza na Uongozi
 Mwafongo na Katibu wa CCM Kata ya Ilala Habib Nasser ambaye pia ni Mjumbe wa Baraza Kuu Jumuiya ya Wazazi mkoa wa Dar es Salaam, wakitoka nje kumsubiri Dk Mndolwa kutoka nje tayari kwa safari ya kwenye kwenye eneo kuu la mapokezi ukumbi wa CCM Mwinjuma Mwananyamala
 Gari lilobeba Dk Mndolwa likiwasili kwenye Viwanja vya Ofisi ya Tawi la CCM Mwinjuma 
 Kijana wa CCM akimvisha Skafu Dk. Mndolwa baada ya kuwasili CCM Mwinjuma
 Dk. Mndolwa akipokea kwa ukakamavu saluti ya kijana wa CCM baada ya kuvishwa skafu
 Dk Mndolwa akiongozana na baadhi ya viongozi kwenda eneo la tukio
 Dk Mndolwa akisalimia baadhi ya wana CCM wakati akienda ukumbini
 Dk Mndolwa akisalimia baadhi ya viongozi wakati akienda ukumbini  
 TOT wakitumbuiza kumlaki ukumbini Dk. Mndolwa
 Dk. Mndolwa akienda meza kuu
 Dk. Mndolwa na Makamu wake- zanzibar wakiwa tayari meza kuu
 Viongozi wa meza kuu wakiungana na Dk Mndolwa kushangilia baada ya kuwasili eneo hilo
 Mmoja wa viongozi katika Baraza la Wazee wa jumuiya ya Wazazi Mzee Mkali akisalimia
 Katibu wa Jumuiya ya Wazazi mkoa wa Dar es Salaam, Ndugu Mwafongo akifanya utambulisho wa viongozi ndazi ya mkoa
 Viongozi ndazi ya mkoa wakisalimia baada ya kutambulishwa 
 Baadhi ya viongozi waliohudhuria mapokezi hayo wakiwa ukumbini
 Naibu Katibu Mkuu wa Jumuia ya wazazi Tanzania Ndugu Rutta akitambulisha viongozi ngazi ya taifa  
 Katibu Mkuu wa Jumuia ya Wazazi tanzania Seif Shaban Mohammed akifafanua maana na umuhimu wa neno 'Mapinduzi'  baada ya kutambulishwa  
 Ndugu Mwafongo akiendeleza ratiba
 Mwenyekiti wa CCM Temeke ndugu Almish akizungumza baada ya kutambulishwa 
 Ndugu Kalokola akizungumza kumtambulisha Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania-Zanzibar Ndugu Haj
 Kakamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania-Zanzibar Ndugu Hajj akizungumza
 Shabiki wa CCM akimuombea maisha marefu na uongozi bora Dk. Mndolwa tukio ambalo lilikuwa la ghafla
 Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam Kate Sylivia Magdalena Kamba akizungumza kabla ya kumkaribisha Dk. Mndolwa kuzungumza na hadhara 
 Omar Kimbau aliyewahi kuhamia CUF akitangaza kurudi CCM mbele ya Dk. Mndolwa
 Dk. Mndolwa akimpongeza Kimbau kwa kuzinduka na kurejea CCM
 Dk. Mndolwa akihutubia kweye mapokezi hayo


CHAKULA CHA JIONI SERENA HOTEL
 Katibu wa Jumuia ya Wazazi mkoa wa Dar es Salaam, Ndugu Mwafongo akiwakaribisha Dk. Mndolwa na Mkewe walipowasili hoteli ya Serena kwa ajili ya chakula cha jioni
 Mwafongo akiwaongoza kwenda eneo la kuketi 
 Dk. Mndolwa akimsalimia Mwenyekiti  wa Jumuia ya Wazazi mkoa wa Dar es Salaam, Ndugu Kalokola
 Dk Mndolwa akimsalimia  Ndugu Kizigha
 Makamu Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi Tanzania- Zanzibar Ndugu Hajj akimsalimia Mama Mndolwa
 Dk Mndolwa akizungumza jambo wakati wakisubiri muda wa chakula
 Ndugu Mwafongo akiwa amesimama kuwakaribisha rasmi waalikwa wote 
 Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi mkoa wa Dar es Salaam Ndugu Kalokola akizungumza maneno ya ukaribisho kwenye chakula hicho cha jioni
 Dk Mndolwa akiongozana na Ndugu Hajj kuchukua chakula
 Angela Kizigha akimsaidia Dk. Mndolwa kubeba chakula
 Mweneyekiti wa CCM Kinondoni akichukua chakula
 Viongozi mbalimbali wakichukua chakula
 Ndugu Mwafongo akiongoka na chakula chake kwenda sehemu ya kuketi
 Ndugu Hajj akichukua chakula 
 Baadhi ya waandaaji wa nyama choma hotei ya Serena
 Waalikwa wakila chakula 
 Dk Mndolwa na mkewe wakipata chakula na waalikwa wengine  

 Dk Mndolwa akitoa nasaha zake baada ya chakula   
Kisha Dk. Mndolwa akapozi kwa picha ya kumbukumbu na viongozi mbalimbali aliopata nao chakula hicho cha jioni. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO