Wednesday, May 28, 2014

LHRC WAZINDUA KITABU CHA URANI NA MAZINGIRA 2014,MADHARA YA MADINI HAYO YAANISHWA

Kituo cha sheria na haki za binadamu nchini Tanzania kwa kushirikiana na ROSA LUXEMBURG FOUNDATION  leo wamezindua kitabu cha urani na mazingira 2014.
Akizindua kitabu hiko leo mgeni rasmi bi MOHFAUDHA HAMID ambaye ni makamu mwenyekiti wa Tume ya haki za binadamuna utawala bora amesema kuwa Tanzania lazima itafakari kwanza maamuzi yake ya kuchimba madini ya urani kwani madini hayo yana madhara kwa binadamu wanaozunguka madini hayo
kitabu hiko kimeainisha mambo yote ambayo ni madhara ya kimazingira na kiuchumi yatokanayo na madini hayo endapo yatachimbwa. 

Bi  HELLEN KIJO BISIMBA ambaye ni Mkurugenzi mtendaji wa LHRC akizungumza katika hafla hiyo ya uzinduzi wa kitabu hicho leo jijini Dar es salaam



Mgeni rasmi ambaye ni makamu mwenyekiti wa Tume ya haki za binadamu na na utawala bora Hon MAHFOUDHA HAMID akikata utepe kuashiria kizindua Kitabu hiko ambacho kimejaa athari na madhara yatakayoletwa kama tutachimba madini ya urani katika nchi ya Tanzania

Tuesday, May 27, 2014

RAIS KIKWETE YUPO NEW YORK.PICHA

 Mhe. Rais akitoka ndani ya uwanja wa ndege wa JFK New York.
Bendera ya Tanzania ndani ya jiji la New York City. 

UCHAGUZI SIMBA SC MAMBO MOTO--WAMBURA OUT

 KAMA ilivyotarajiwa, Michael Richard Wambura ameenguliwa katika kinyang’anyiro cha Uchaguzi mkuu wa Simba SC unaotarajiwa kufanyika mwezi ujao, kwa sababu kubwa mbili.

          Akizungumza katika Mkutano maalum na Waandishi wa Habari mchana huu makao makuu ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), makutano ya mitaa ya Ohio na Libya, Dar es Salaam Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya Simba SC, Wakili Dk Damas Daniel Ndumbaro amesema Wambura ameondolewa kwa sababu kwa sasa si mwanachama halali wa klabu hiyo.

SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI--KITAIFA NI MWANZA,WAZIRI MAHENGE ATOA NENO

Watanzania wametakiwa kuungana kwa pamoja katika kuadhimisha siku ya mazingira duniani ambayo itaadhimishwa tarehe 5 mwezi juni mwaka huu ambapo kidunia siku hiyo itaadhimishwa katika kisiwa cha BARBADOS moja ya visiwa vya karibian na tanzania siku hiyo itaadhimishwa mkoani mwanza.

    Akitangaza maadhimisho hayo leo mbele ya wanahabari jijini dar es salaam waziri wa nchi ofisi ya makamu wa rais mazingira mh BINILIUS MAHENGE  amesema kuwa siku ya mazingira duniani iliamuliwa na azimio la baraza la umoja wa mataifa la mwaka 1972 kama kielelezo cha ufunguzi wa mkutano wa kwanza wa umoja wa mataifa kuhusu mazingira uliofanyika huko stockholm nchini sweden.

Monday, May 26, 2014

PIGO TENA BONGO MOVIES--HUYU NDIYE MSANII MAARUFU WA KIKE ALIYEFARIKI DUNIA MUDA HUU WAKATI AKIJIFUNGUA

HABARI AMBAZO MTANDAO HUU UMEZIPATA MUDA HUU NI KUWA MSANII MAARUFU WA SINEMA ZA TANZANIA RECHO HAULE AMEFARIKI DUNIA ASUBUHI HII.MAREHEMU AMEPOTEZA MAISHA BAADA YA KUJIFUNGUA ASUBUHI HII,MUNGU AILAZE PEPONI ROHO YAKE AMEN.

HABARI KUTOKA KWA RAIS WA BONGO MOVIES STEV NYERERE AMEDHIBITISHA KUTOKEA KWA KIFO HICHO ASUBUHI HII YA JUMANNE NA TAYARI YUPO NJIANI KUELEKEA HOSPITALI YA MUHIMBILI KWA AJILI YA TARATIBU NYINGINE.

WASANII WOTE WA BONGO MOVIES MNAOMBWA MKUTANE VIWANJA WA LEADERS CLUB LEO MCHANA KWA AJILI YA KUPANGA JINSI YA KUMPUMZISHA MWENZENU.

HABARI24 BLOG INATOA POLE SANA KWA FAMILIA YOTE YA HAULE NA WANATASNIA WOTE WA TASNIA YA FILAMU TANZANIA.


BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA,JINA LA BWANA LIHIMIDIWE.

AMENNNNN

BAADHI YA MAGAZETI YA LEO JUMANNE MAY 27 YAKO HAPA


PICHA ZA MGOMO WA MADEREVA NA MAKONDAKTA WA DALADALA LEO ASUBUHI KUGOMA KUPELEKA ABIRIA MWENGE KUTOKA MAKUMBUSHO

 Kamanda wa Polisi Kinondoni akiongea na waandishi wa habari kuelezea ni jinsi gani watashughulikia shida ya barabara hiyo ya kutoka kituoni makumbusho kuelekea mwenge
 Kondakta wa Daladala akiwa ameumia mkono wake wa kulia baada ya kukatwa na side mirror ya basi la UDA alipokuwa akilizuia lisipakie abiria na kuondoka kwenda mwenge
 Hapo ni Madereva na makondakta wakilikimbiza basi la UDA ambalo lilimkata mkono dereva mwenzao wakati wanalizuia lisiweze kutoka ndani ya kituo kuendelea na safari.

BIBI ALIYENASWA NA MADAWA YA KULEVYA AANGUA KILIO MAHAKAMANI

BIBI wa Kinigeria, Olabisi Ibidun Cole (65), leo ameangua kilio katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar ers Salaam wakati akipelekwa kizimbani kwa ajili ya kusomewa kesi yake ya kunaswa na madawa ya kulevya yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 37.
Hakimu aliyepelekewa kesi hiyo, Frank Mushi, aliiahirisha kesi hiyo mpaka kesho ili bibi huyo ambaye hajui Kiswahili wala Kiingereza atafute mkalimani.
Cole alisema lugha anayoweza kuitumia kiufasaha ni Kiyoruba ambacho hutumiwa nchini Nigeria. Katika hali iliyoonesha kukata tamaa, bibi huyo alianza kuangua kilio akiomba Mungu amsaidie.

 
Bibi wa Kinigeria, Olabisi Ibidun Cole akipelekwa mahakamani.


KAMISHNA KOVA AMLILIA MWANDISHI MZEE MAX,ATOA RAMBI RAMBI YAKE,WENGINE TUIGE KWAKE

Na Karoli VInsent

        JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,lamlilia Aliyekuwa Mwandishi na mpiga Picha wa Kituo cha Runinga cha Mlimani Mzee Maxmiliani,ambaye aliyefariki Gafla kwa Presha.

       Kilio hicho, kimetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Kamishna Suleiman Kova,wakati wa Mkutano na Waandishi Habari, Ambapo alisema wao kama Jeshi la Polisi wamesikitishwa na Kifo cha Mwandishi wa huyo Mkongwe wa Habari na Mpiga picha Nchini.

     “Sisi  Jeshi la polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Tumesikitishwa sana na Kifo cha Mzee wetu huyo Bwana Maxmiliani,kwani amekuwa akitoa Mchango mkubwa,kwetu Jeshi la Polisi hususani Kanda hii ya Dar es Salaam kwa kuhakikisha Taarifa zinafika kwa Wananchi kutoka kwetu kwa wakati Muhafaka,”

SALAAM ZA RAMBIRAMBI KIFO CHA MWANDISHI MAXIMILIAN JOHN NGUBE KUTOKA CHADEMA

Kurugenzi ya Mawasiliano na Uhusiano ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), imepokea kwa mshtuko na majonzi makubwa taarifa za kifo cha mmoja wa waandishi wa habari za picha (mpiga picha) mwandamizi nchini, Maximillian John Ngube aliyefariki siku ya Ijumaa baada ya kuugua muda mfupi.

Kwa masikitiko makubwa kurugenzi, kwa niaba ya chama, inatuma salaam za pole kwa familia ya marehemu Maximilian kwa kuondokewa na baba na mpendwa wao, katika wakati ambao tunaamini walikuwa bado wakimhitaji sana kama moja ya nguzo za familia.

HABARI INAYOTIKISA JIJI KWA SASA---VIJANA WA PANYA ROAD 149 WATIWA MIKONONI MWA POLISI KWA MASAA 24,KAMISHNA KOVA ASEMA HATOKI MTU,HADI WAKAMATWE WOTE,PICHA ZAO NA MAJINA YAKO HAPA

Hawa ndio viongozi wa panya road na mbwa mwitu ambao tayari wameshakamatwa
 Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limefanya msako wa nyumba kwa nyumba, mtaa na maeneo yaliyoathirika kwa hofu ya vijana ambao ni vibaka maarufu kama Mbwa mwitu au Panya Road.  Msako huu uliofanyika ndani ya masaa 24 hadi alfajiri ya tarehe 26/5/2014 kwa lengo la kuwaondolea hofu na uhalifu dhidi ya makundi ya vijana wadogo wasio na ajira ambao uliibuka hivi karibuni.

        Maeneo yaliyoathirika ni Kigogo, Magomeni, Tabata, maeneo yote yanayozunguka mto Msimbazi, maeneo ya Mbagala nk.  Msako huu unaendelea kufanywa na askari wa vikosi maalum ambao wamepewa kazi ya kuhakikisha kuwa vikundi hivyo haviibuki tena na vinatokomezwaa kabisa kwa  kuwakamata wale wote wanaojihusisha na vitendo vya kuvamia kwa mkundi wananchi ambao hawana hatia
Kamishna kova ambaye amezungumza na wanahabari muda mfupi uliopita
 Kati ya watuhumiwa 149 waliokamatwa mmoja amegundulika kuwa ni kiongozi aitwaye ATHUMANI SAIDI miaka 20, Mkazi wa Kigogo na amekiri anaongoza kundi la watu zaidi ya 15 ambao baadhi yao ni kati ya waliokamatwa.  

          Imegundulika pia kwamba vijana hawa wanatumia dawa za kulevya aina ya bangi na wengine hujichoma sindano na kuwafanya iwe rahisi kujihusisha na matukio ya uhalifu.  Vijana hao hupenda kushiriki katika ngoma kama Mnanda, Mchiriku, Kigodoro, Kanga moja nk. ambazo kwa kawaida huchezwa hadi usiku wa manane.  


         Wakitoka katika ngoma hizo hujikusanya pamoja na kufanya matukio ya uporaji kwa mtu wanayekutana naye, kufanya uvunjaji katika majumba na wakati mwingine wana mtindo wa kugema mafuta ya diesel au petrol katika matanki ya malori yanayosafirisha mafuta.  


         Operesheni kali inafanyika katika maficho ya wahalifu hao ikiwa ni pamoja na daraja la River side, Kigogo darajani, Manzese, maeneo ya Tandale pamoja na maeneo mengine ya maficho mkoa wa Kipolisi Temeke.


  Tunawasiliana na Maafisa utamaduni wa Wilaya zote za Mkoa wa D’Salaam kusimamisha utoaji wa vibali wa ngoma za usiku ambazo hazina tija.  Pia Jeshi la Polisi linafuatilia na kuwavizia vijana wanaopora  watu wanaotoka katika sherehe za usiku kama vile Harusi na wanaotoka katika mikesha ya Ibada na sehemu zozote zenye mikusanyiko. 

      Aidha Jeshi la Polisi wanapambana na vijana wanaowavizia watu katika vituo vya mabasi pindi wanapotoka alfajiri kwenda katika shughuli zao za kila siku.

Wanahabari
Zipo taarifa kwamba baadhi ya wazazi wasio waaminifu wamewasafirisha watoto wao wahalifu katika makundi haya kwenda mikoani ili kukwepa wasinaswe na msako huu mkali.  Hata hivyo Jeshi la Polisi lina mtandao wa kutosha kati yake na mikoa mingine na nchi jirani hivyo litawatafuta popote walipo na kuwakamata.

         Oparesheni hii ni endelevu na ya kudumu hadi kero hii ya vibaka itakavyokwisha kabisa. Baadhi ya majina waliokamatwa ni kama ifuatavyo:-
1.    DANIEL PETER @ MALUNDE, miaka 25, mkazi wa Yombo Kigunga
2.    MWISHEHE ADAM, miaka 35, mkazi wa Mtoni mashine ya maji
3.    MOHAMED SAID, miaka 32, mkazi wa Mtoni
4.    JAKAMA ALPHONCE, miaka 23, mkazi wa Mtoni Kilakala
5.    HAMADI MDUDU, miaka 25, mkazi wa Mbagala
6.    SALUM MUSA, miaka 25, mkazi wa Kiwalani
7.    ANTHONY DANIEL, miaka 20, mkazi wa Mashine ya maji
8.    FIDELIN ANTHONY, miaka 18, mkazi wa Kigogo
9.    HAMZA MAZUMA, miaka 19, mkazi wa Kigogo
10.           MGANGA ABEID, miaka 20, mkazi wa Kigogo
11.           SAID ABEID, miaka 19, mkazi wa Kigogo
12.           SALUM NYENJE, miaka 36, mkazi wa Chamazi
13.           DOMINICK PETER miaka 22, Mkazi wa Kigogo
14.           KULWA ABEID, miaka 20, mkazi wa Mabibo
15.           MUSA IBTRAHIM, Miaka 20, mkazi wa Magomeni
16.           HUSSEIN SHABAN, miaka 22, Mkazi wa Magomeni

S. H. KOVA
KAMISHNA WA POLISI KANDA MAALUM


DAR ES SALAAM

Sunday, May 25, 2014

KIINGILIO TAIFA STARS, MALAWI HIKI HAPA

Kiingilio cha chini cha mechi ya kirafiki kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Malawi (Flames) itakayofanyika Jumanne (Mei 27 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni sh. 5,000.

Washabiki watakaolipa kiingilio hicho ni kwa wale watakaokaa kwenye viti vya rangi ya chungwa, bluu na kijani. Kwa upande wa VIP B na C kiingilio kitakuwa sh. 10,000 wakati kwa VIP A itakuwa ni sh. 20,000.

MWENGE WA UHURU 2014 WAMALIZA MBIO ZAKE MKOANI RUKWA LEO, WAMMULIKA MLEMAVU WA NGOZI (ALBINO) ALIYEKATWA MKONO MWAKA JANA

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya (katikati) akishiriki mbio za Mwenge wa
Uhuru (2014) na viongozi wa mbio hizo kitaifa, viongozi na wafanyakazi wa
Serikali, vyama vya siasa Mkoani Rukwa na wananchi muda mfupi kabla ya
kukabidhi Mwenge huo kwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Abass Kandoro baada ya
Mwenge huo kukamilisha mbio zake Mkoani Rukwa leo tarehe
25-05-2014. Mwenge huo wa Uhuru mkoani Rukwa ulitembelea miradi ya
maendeleo 28 na vikundi 27 vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya Tsh. bilioni nne