![]() |
Msanii maarufu wa filamu tanzania ROSE NDAUKA katikati akizungumza na wanahabari leo jijini dar es salaam |
Na Karoli Vinsent
BAADA ya
kuwaacha Midomo wazi wakazi wa Jiji la Dar es Salaam katika kujitolea kufanya
usafi wa kufagia Barabara za jiji hilo,Staa filamu Nchini Rose Ndauka ameandaa
Tamasha kubwa litakalowafanya wapenzi wa burudani nchi kufurahia.
Hayo,yametangazwa leo Jijini Dar es Salaam na Rose Ndauka
wakati wa mkutano na waandishi Habari ambapo aliwataka wananchi wajitokeze kwa
wingi kwenye Tamasha hilo.
“Nawasihi wananchi hususani wa Dar es Salaam wajitokeze kwa
wingi kwenye Tamasha hili la Burudani ambalo litafanyika ijumaa ya Tarehe 28
mwezi huu saa kumi nambili jioni katika viwanja vya chuo cha utalii kilichopo
Posta karibu na wizara ya afya na kukaribiana na chuo cha usimamizi wa Fedha
IFM”
“Tamasha hili litakuwa na Burudani nyingi zitakazokufanya
ufurahi ikiwemo kutoka kwa msaniii Leah Muddy ambae ni mshindi wa shindano la
bongo star search pamoja na vikundi vya ngoma za asiri “alisema Ndauka
No comments:
Post a Comment