Saturday, March 29, 2014

BAADA YA YULE MWANDISHI WA DAILY MAIL KUITWA TANZANIA,HATIMAYE AWAGEUKA WALIOMWITA,AANDIKA MAKALA NYINGINE YA KUKOSOA TENA JK NA NYALANDU JUU YA UJANGILI


Mwandishi huyo akitembelea hifadhi ya meno ya tembo
           



NA KAROL VICENT



          KILE kinachotafsriwa ni kugeukwa kwa serikali ya Tanzania na Mwandishi wa Gazeti la Sunday Mail la Nchini uingereza  Martini Fletcher baada ya kuandika makala nyingine ikihishutumu tena serikali ya Jakaya kikwete kwa kushindwa kuwachukilia hatua Majangili.

        Kugeukwa kwa Serikali ya Tanzania kumetokana na Serikali ya Tanzania kupitia Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu kutumia Garama kubwa ya  kumuita Mwandishi huyo kile kinachoonekana ni kujikosha kwa serikali baada ya mwandishi huyo kuandika makala ikiituumu serikali ya Tanzania kushindwa kuwachukulia hatua Majangili.



         Katika Makala yake hiyo ya Jumapili ya Tarehe 23 mwezi huu alimshutumu Rais Kikwete kwa kushindwa kuwachukulia Hatua Majangili huku akiwajua kabisa wanapokaa.

         
       Makala hiyo ilizidi kusema Chama cha Mapinduzi CCM ambacho ni Chama anachotoka Rais Kikwete ndio vinara wa Vitendo vya ujangili, ,vilevile Ndio sababu Rais kikwete kushindwa kuwachukulia hatua Majangili.

      
           Ikumbukwe Mwandishi huyo aliwasili nchini wiki mbili zilizopita na kufikia kwenye hoteli ya Kimataifa ya Serena na Baadae kutembelea pori la akiba Selous na Hifadhi ya Serengeti.na vilevile inasemekana alionana na Rais wa Jakaya kikwete ili Mwandishi huyo abadili kile alichokiandika kwenye makala yake.

        
          Makala ya Fltecher kwenye Gazeti hilo la Uingereza,yaliwakasirisha viongozi wa Tanzania hususan Rais Kikwete hasa kutokana na ujio wake ulilenga muda ambao viongozi wa mataifa zaidi ya 50 walikuwa wamealikwa kwenye mkutano maalum ulioitishwa na mwana wa Mfalme wa Uingereza,Prince Charles,mjini London


       Makala yake aliyoitoa Februali 8 mwaka huu na kuchapishwa kwenye Gazeti la Sunday Mail ambapo katika makala hiyo ilimtuhumu Rais kikwete kwa kushindwa kuwachukulia hatua vinara wa vitendo vya ujangili

Vilevile, Makala hiyo ikizidi kumtuhumu Kikwete kwa kumdharau aliyekuwa waziri wa Maliasili na Utalii Barozi Khamisi Kagasheki alipokuwa anamletea Orodha ya vinara wa vitendo vya ujangili.



       Baada ya kuandika Makala hiyo  Rais Kikwete wakati alipokuwa nchini uingereza anahojiwa kwenye kituo cha televishieni cha CCN alikanusha taarifa hiyo na kusema serikali yake imefanya kazi kubwa ya kukomesha vitendo vya ujangili hapa nchini.

       
         Duru za mambo zinasema kugeukwa kwa Serikali ya Tanzania na Mwandishi huyo,kunaonyesha udhaifu kwa serikali katika kusimamia mambo huku wengine wakisema Kuna haja gani ya Serikali kutumia pesa nyingi sana kumleta mwandishi huyo ili andike makala nyingine ya kuisafisha Serikali ya Tanzania,Badala ya kuwachukulia hatua majangili,

      
          Huu ni mwendelezo wa Serikali ya Jakaya Kikwete kuwadaa watanzania ikumbukwe wakati anahutubia Bunge Rais Kikwete aliwaikujinadi kuwa anaorodha ya Vinara ya wauza madawa ya Kulevya lakini alishindwa kuwachukulia hatua

No comments: